Monday, June 3, 2013

Gaddafi alificha mali Afrika Kusini piya



Wizara ya fedha ya Afrika Kusini inachunguza tuhuma kwamba mali ya thamani ya kama dola bilioni moja ya Libya ilifichwa nchini humo.
Rais Zuma na Gaddafi mwezi May mwaka 2011 walipokutana Tripoli, Libya
Wakuu wa Libya wamedai kuna dhahabu, almasi na fedha taslim ambazo kiongozi wa zamani wa Libya, Kanali Gaddafi na familia yake, waliziweka Afrika Kusini.
Serikali ya Libya imekuwa ikijaribu kuzipata mali za Kanali Gaddafi katika sehemu mbali-mbali za dunia tangu alipofariki mwaka 2011.
Mwandishi wa BBC mjini Johannesburg anasema watu wengine wamekisia kuwa mali ya hayati Gaddafi ilioko nchi za nje inaweza kufika dola bilioni 80.

Mapendekezo ya wagombea huru TZ


Mkuu wa tume ya marekebisho ya katiba Tanzania
Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania, imependekeza wawepo wagombea huru katika ngazi za uchaguzi mbalimbali nchini humo. Hayo ni miongoni mwa mapendekezo yaliyotangazwa jijini Dar es salaam na Mwenyeketi wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba wakati wa uzinduzi wa Rasimu ya Kwanza ya Katiba Mpya.
Jaji Warioba amesema pia wapo wananchi waliopendekeza kwamba, wagombea huru waruhusiwe kugombea nafasi zote isipokuwa nafasi ya urais. Jaji Warioba amesema tume ilipitia maoni hayo na kupendekeza kwamba, wagombea huru waruhusiwe kugombea nafasi zote kuanzia ngazi ya Mwenyekiti wa Mtaa hadi nafasi ya Urais.
Kadhalika Jaji Warioba amesema, Tume pia imependekeza kwamba, mgombea yeyote wa urais ili athibitike kuwa ni mshindi atalazimika kupata zaidi ya asilimia hamsini ya kura, na kwamba endapo mgombea hatafanikiwa kupata asilimia hamsini uchaguzi utarudiwa kwa kuangalia wagombea wawili waliopata kura nyingi.
Mapendekezo mengine yaliyotangazwa na Tume ni pamoja na kuwepo kwa serikali tatu yaani ya Bara,Zanzibar na ile ya Shirikisho.
Pia tume imependekeza kuwa, Bunge la Muungano liwe na jumla ya Wabunge 75, hamsini kutoka Bara, ishirini kutoka visiwani na watano wateuliwe na Rais kutoka makundi maalum ya walemavu.
Mapendekezo mengine ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ni pamoja na Rais kubakia na madaraka yake ya uteuzi wa viongozi wa ngazi za juu, lakini uteuzi wa ngazi za chini uachiwe Tume ya Utumishi.
Imeeleza kwamba, Rais mara baada ya kufanya uteuzi wa viongozi wa ngazi za juu wakiwemo, mawaziri, manaibu waziri, jaji mkuu na naibu jaji mkuu, viongozi hao watalazimika kuthibitishwa na Bunge.

Familia ya Pistorius yashtushwa na picha


Pistorius atafikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza tangu kuachiliwa kwa dhamana
Familia ya mwanariadha mlemavu nchini Afrika Kusini, Oscar Pistorius, wameshstushwa na picha zilizofichuliwa za bafu alimomuulia mpenzi wake mnamo mwezi Februari.
Shirika la habari la Uingereza la Sky, mnamo Ijumaa, lilionyesha picha za kuogofya zinazoshukiwa kuwa za bafu ambalo mpenzi wa Pistorius Reeva Steenkamp, aliuawa.
Polisi walisema kuwa wamechukizwa mno na kufichuliwa kwa picha hizo.
Bwana Pistorius mwenyewe anakanusha madai ya kumuua mpenzi wake, kupitia mlango wa bafu alimokuwa , alisema alidhani kuwa alikuwa mwizi aliyevamia nyumba yake.
Anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa hatua ya mahakama mwanzo kutathmini kesi siku yake Jumanne.
Pistorius ni mwanariadha mlevamu asiye na miguu yake miwili ingawa hukimbia kwa miguu bandia au vyuma. Alishiriki michezo ya Olimpiki mjini London mwaka jana.
''Familia ya Pistorius ilimuunga mkono alipokuwa anajiandaa kufikishwa mahakamani , alisema mjomba wake,'' Arnold Pistorius.
''Tunaamini maneno yake , tunampenda na tutamuunga mkono kwa kila hatua ya kesi hii,''alisema Mjombake Pistorius.
"tumeshtushwa na picha hizi za ajali iliyotokea nyumbani kwa Oscar."
Msemaji wa polisi ameelezea kuwa polisi wanachunguza nani aliyefichua picha hizo .
''Kitendo hiki hakikuhitajika na kimetuudhi kweli. Hatujui picha hizi zimetoka wapi,'' alisema polisi huyo.
Pistorius atafikishwa mahakamani Jumanne kwa mara ya kwanza tangu kuachiliwa kwa dhamana, kufuatia kukamatwa kwake, kuhusu mauaji ya Steenkamp.
Kesi hiyo inatarajiwa kuakhirishwa kwani uchunguzi wa polisi ungali unaendelea.
Pistorius ameajiri baadhi ya mawaklili shupavu nchini Afrika Kusini kumtetea.
Anasema kuwa alimpiga risasi Bi Steenkamp kupitia mlango wa choo kimakosa baada ya kudhani kimakosa alikuwa mwizi.
Hata hivyo, viongozi wa mashtaka wanasema kuwa alimuua kwa maksudi baada ya wawili hao kugombana.

Mamlaka ya Zanzibar Kwanza

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akiwahutubia wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti kusherehea “Umoja na mshikamano wa Wazanzibari”
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akiwahutubia wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti kusherehea “Umoja na mshikamano wa Wazanzibari”
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, ameunga mkono kauli iliyotolewa na Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Eddi Riyami ya kuwataka Wazanzibari wasiotaka mamlaka kamili ya Zanzibar wajitokeze hadharani kama wanavyofanya wale wanaodai mamlaka kamili ya Zanzibar.
Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF ameeleza hayo katika viwanja vya Kibanda maiti mjini Zanzibar katika mkutano wa hadhara uliolenga kusherehekea “Umoja wa Wazanzibari” ulioasisiwa kufuatia maridhiano ya kisiasa.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Amesema hatua ya Wazanzibari kudai mamlaka ni haki yao, na kwamba hakuna dhambi ya kudai jambo hilo.
Amefahamisha kuwa wazanzibari walio wengi wameungana kudai mamlaka ya nchi yao kwa njia ya amani na demokrasia, na kutoa wito kwa wale wasiotaka mamlaka ya Zanzibar wajitokeze hadharani.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti wakinyosha mikono na kucheza wakati wakisherehekea hotoba ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti wakinyosha mikono na kucheza wakati wakisherehekea hotoba ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Amewahakikishia wananchi kuwa hatorudi nyuma katika kuitetea Zanzibar kuwa na mamlaka yake, ili iweze kutambulika kimataifa na kuweza kuratibu na kushughulikia mambo yake ya nje.
Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Eddi Riyami,  akitoa salamu za Mwenyekiti wa Kamati hiyo Hassan Nassor Moyo katika viwanja vya kibanda maiti mjini Zanzibar.
Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Eddi Riyami, akitoa salamu za Mwenyekiti wa Kamati hiyo Hassan Nassor Moyo katika viwanja vya kibanda maiti mjini Zanzibar.
Kwa upande wake Katibu wa kamati ya maridhiano Ismail Jussa Ladhu, amewaomba viongozi wa vyama vyote kushirikiana na wananchi  katika kudai mamlaka ya nchi, ili wazanzibari waweze kujikomboa kutokana na kile alichokiita ukoloni wa Tanganyika.
Katibu wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Ismail Jussa Ladhu akizungumza na wananchi katika viwanja vya Kibanda maiti.
Katibu wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Ismail Jussa Ladhu akizungumza na wananchi katika viwanja vya Kibanda maiti.
Katika risala ya wananchi wa mikoa mitano ya Zanzibar iliyosomwa na Ameir bin Ameir kutoka Bwejuu, amesema pamoja na mambo mengine, katiba mpya izingatie uwepo wa Jamhuri ya Zanzibar na uraia wake.
Mambo mengine waliyotaka yatolewe katika orodha ya mambo ya Muungano ni pamoja na sarafu, benki kuu, mambo ya nje, vyama vya siasa, baraza la mitihani pamoja na mafuta na gesi.

Tuisaidie vipi Zanzibar itoke kwenye Muungano?

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Hassan Nassor Moyo (kushoto) na Mjumbe wa kamati hiyo Ismail Jussa Ladhu, wakibadilishana mawazo kabla ya ufunguzi wa kongamano la maridhiano lililofanyika hoteli ya bwawani.
Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Hassan Nassor Moyo (kushoto) na Mjumbe wa kamati hiyo Ismail Jussa Ladhu, wakibadilishana mawazo kabla ya ufunguzi wa kongamano la maridhiano lililofanyika hoteli ya bwawani.
June 3, 2013 By Inaonekana kina Seif Sharrif na kina Karume hawataki hasa Zanzibar iwe dola huru ikiwa na “mamlaka yake”. Kwa karibu miaka miwili sasa wameendelea “kudai” Zanzibar “huru” huku wakipuuzia njia zote rahisi za kuweza kufanya hivyo. Nimejaribu kwa kila namna kuwapa ushauri rahisi wa kuiondoa Zanzibar kwenye Muungano na ikawa nchi huru na tukakutana UN, SADC, na EA kama nchi huru majirani lakini ndugu zetu inaonekana hawataki kuchagua njia hata moja. Badala yake wameendelea na nina uhakika wataendelea kufanya mikutano mingine ya “kudai” Zanzibar huru.
Sasa najiuliza wanataka tuwasaidieje? Wanataka sisi tuwafukuze watoke ili waseme tumewafukuza? Suala la Zanzibar kuwa na mamlaka yake kamili liko mikononi mwa Wazanzibari peke yao.
1. Walipodai Bendera ya Zanzibar Tanzania bara hatukuulizwa; waliamua wakawa nayo
2. Walipotaka wimbo wa Taifa – Tanzania Bara hatukuulizwa; wakawa nao
3. Walipoamua kutangaza Zanzibar ni huru na kuainisha mipaka yake kupitia katiba yao walifanya hivyo bila Watu wa Bara kuulizwa.
Kuna ushahidi wa kutosha kabisa kuwa linapokuja suala la Zanzibar kudai “uhuru” na alama za kuwa bado wao ni dola Zanzibar wana rekodi ya kufanya hivyo bila kuomba kibali kutoka Dodoma au kwa watu wa bara. Sasa kwanini kwenye “mamlaka kamili” ni kama vile “wanataka hawataki”? Kabla sijaamua kuwapa pendekezo jingine naomba Wazanzibar wale asilimia 60 ambao wanaamini kutokana na wingi wao wanawakilisha msimamo wa Wazanzibari wote wafanya mambo yafuatayo ili waharakishe kuitoa Zanzibar kwenye “ukoloni” wa watu wa bara na kuirejesha kuwa ile nchi nzuri, ya heri, ambapo watu wake wote walikuwa wanaishi kwa furaha na maridhiano tangu enzi na enzi.
1. Chama cha CUF na wale wa CCM upande wa Zanzibar ambao wanaamini Zanzibar inakaliwa na Bara kama koloni watangaze kutoutambua Muungano huu kwa vile siyo halali.
2. Wakishafanya hilo la kwanza CUF na CCM Zanzibar wawaambie wabunge wao walioko kwenye Bunge la Muungangano kujiuzulu mara moja ili warudi Zanzibar
3. Wazanzibar wamuambie Makamu wa Rais wa Muungano Dr. Ghaib Bilali pamoja na watumisho wengine wote walioko kwenye Utumishi wa Jamhuri ya Muungano ambao ni Wazanzibari waachie nafasi zao zote ili kutekeleza hilo la 1. Hii itauthibitishia ulimwengu na marafiki zao kuwa kweli wako serious katika kutaka uhuru – huwezi kudai uhuru wakati huo huo unatumikia serikali ile ile!
4. Ili kufanikisha hayo mambo matatu ya kwanza hapo juu na kuwa yasionekane yamefanywa kiholela basi Baraza la Wawakilishi ambao lina wasomi lifanye mambo mawili. Kwanza lilete hoja rasmi ya kuitaka serikali kuandaa mswada wa Sheria ya kusimamia kura ya maoni (referendum) ya jinsi Zanzibar itajitoa, ijitoe lini na vipi na kwa mfumo gani. Na pili ni kuileta sheria hiyo ili ipitishwe na Wawakilishi.
5. Kwa vile inawezekana basi katika sheria hiyo ya No 4 hapo itahitaji Bunge la Muungano liliridhie basi Baraza la Wawakilishi lipitishe sheria hiyo na iridhiwe na Rais wa Zanzibar na hoja ya sheria hiyo iletetwe na hao wabunge wa Zanzibar kwenye Bunge la Muungano (kabla hawajatoka) ili Bunge la Muungano liipitishe na kuruhusu Zanzibar kuanza mchakato wa kutoka kwenye Muungano na ili kwamba Bunge la Muungano nalo liweke utaratibu wa kuhakikisha kuwa mali na haki za Watanganyika Zanzibar haziangukii mikononi mwa Nchi ya Zanzibar!
6. Wazanzibari waharakishe kuweka tarehe ya kutaka kutoka kwenye Muungano ili na sisi watu wa bara tuzidi kuwaombea ili matamanio yao na njozi zao za kuirudisha Zanzibar ambayo inatawaliwa na Tanganyika zitimie.
NB: Ikumbukwe kuwa watu wa bara hatutaki Muungano wa Mkataba. Tunataka Zanzibar watoke bila ya kufuatiwa na kitu kingine chochote zaidi ya mahusiano ya ujirani mwema wa nchi mbiili. Bila ya shaka kutokana na historia inawezekana katika mfumo ujao kutakuwa na makubalianao ya nchi mbili (bilateral agreements) ili kuhakikisha Zanzibar inaendelea kuwa huru n.k nk
Sasa kama njia hizi zote hazichukuliwi; tuwasaidie vipi Wazanzibar hawa wanaotaka kutoka kufunga virago?
LET ZANZIBAR GO!!!

Ajali ya ukuta wa tangi la maji yauwa watatu Pemba



Askari wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiwa katika zoezi la kuondoa miili ya Marehemu waliopoteza maisha katika ajali ya kuangukiwa na ukuta wa tangi la maji Machomanne Chake Chake Pemba
Askari wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiwa katika zoezi la kuondoa miili ya Marehemu waliopoteza maisha katika ajali ya kuangukiwa na ukuta wa tangi la maji Machomanne Chake Chake Pemba
Tangi la maji lilipo Machomane Chake Chake Pemba ambalo lilikuwa kwenye harakati za kuangushwa na kujengwa upya, limeanguka na kuelemea mafundi waliokuwa juu ya tangi hilo ambapo hadi jana watu watatu wameripotiwa wamefariki dunia na tisa kujeruhiwa.
Miongoni mwa waliofariki wametambuliwa kuwa ni Salumu Muhidini (35) Juma Rashid mkazi wa Chanjani, na mmoja aliyejulikana kwa jina la maarufu la Golo (35).
Kwa mujibu wa taarifa za watu wakaribu wanasema ajali hiyo imetokea kutokana na vifaa duni visyivokuwa na uwezo wa kufanyia kazi hiyo ambayvo walikuwa wakivitumia mafundi hao.
Wananchi mbali mbali wakiwa katika hospitali ya Chake Chake  Pemba, wakitizama miili ya ndugu zao waliopoteza maisha na majeruhi baada ya kuangukiwa na mnara wa tangi la maji Machomanne Pemba
Wananchi mbali mbali wakiwa katika hospitali ya Chake Chake Pemba, wakitizama miili ya ndugu zao waliopoteza maisha na majeruhi baada ya kuangukiwa na mnara wa tangi la maji Machomanne Pemba
Wananchi mbali mbali wakiuangalia mnara wa Tangi la maji Machomanne, ulioanguka na kupoteza maisha ya wananchi watatu jana asubuhi huko Machomnne, Chake Chake Pemba
Wananchi mbali mbali wakiuangalia mnara wa Tangi la maji Machomanne, ulioanguka na kupoteza maisha ya wananchi watatu jana asubuhi huko Machomnne, Chake Chake Pemba

Daktari Bingwa kutoka Quba anayefanya kazi zake kisiwani Pemba, (jina halikufahamika) akimtibu mmoja kati ya majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Chake Chake, kufuatia ajali ya kuangukiwa na ukuta wa mnara wa tangi la maji Mchomanne Pemba
Daktari Bingwa kutoka Quba anayefanya kazi zake kisiwani Pemba, (jina halikufahamika) akimtibu mmoja kati ya majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Chake Chake, kufuatia ajali ya kuangukiwa na ukuta wa mnara wa tangi la maji Mchomanne Pemba
Picha zote kwa hisani ya Voice of Zanzibar(VoZ) na Abdi Suleiman wa Pemba

Vijana amkeni wakati wenu ni huu

Youth_Summit1 

WIKI nzima iliyopita mamia ya Waafrika walimiminika Addis Ababa, Ethiopia. Wengi walikwenda kuhudhuria sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) ambao miaka 12 iliyopita uliuzaa Muungano wa Afrika(AU).
Baadhi yetu tulikwenda kuitathmini hiyo miaka 50, kuangalia tulikotoka, tuliko na tuendako.Tulitathmini kwa kiwango gani malengoya Umoja huo yametimizwa na nini cha kufanywa kuliendeleza Bara la Afrika katika kipindi cha miaka 50 ijayo.
Bahati mbaya katika kufanya tathmini hiyo kuna wenye kusahau tulikotoka. Hivyo inakua rahisi kwao kukosoa kila kitu na kuufananisha Muungano wa Afrika na debe tupu.
Tumekwisha wazoea wenye kuona raha kuugeuza Umajumui wa Kiafrika (Pan-Africanism) uwe kama punda kirongwe, wa kustahiki bakora tu. Na kila wapatapo fursa wanautandika na kuubeza Muungano huo.
Wana usahau mchango adhimu wa Umajumui wa Kiafrika katika ukombozi wa Afrika. Tukiiangalia historia ya Afrika ya tangu mwanzoni mwa karne iliyopita hadi sasa tunaona kwamba nguvu kubwa iliyolisukuma mbele bara hili kuelekea uhuru ni ile dhana ya Umajumui wa Kiafrika pamoja na vuguvugu lake.
Mavuguvugu ya Umajumui wa Kiafrika yalikuwa kama matufali ya kujengea lile vuguvugu kubwa la kuwania uhuru wa nchi za Kiafrika.
Miongoni mwa mavuguvugu hayo ni lile la Rassemblement Démocratique Africain (RDA), lililoasisiwa 1946 mjini Bamako, Mali, chini ya uongoziwa Félix Houphouët-Boigny.
RDA lilikuwa jumuiya ya mwanzo ya Umajumui wa Kiafrika katika nchi za Kiafrika zitumiazo lugha ya Kifaransa. Ilikuwa si chama kimoja bali mtandao wa vyama mbalimbali vilivyo kuwa na mwelekeo mmoja katika nchi tafauti za Kiafrika.
Kwa upande wa kanda zetu za Afrika ya Mashariki na ya Kati tulikuwa na jumuiya ya Pafmeca na baadaye Pafmecsa ikiijumuisha na nchi ya Afrika ya Kusini.
Halafu kulikuwako Mkutano wa Watu Wote wa Afrika (AAPC) uliofanywa mara tatu — Accra (1958), Tunis (1960) na Cairo (1961). Mikusanyiko yote hiyo ilisaidia kuleta uzinduzi wa kisiasa Afrika.
AAPC ulikuwa mkutano uliohudhuriwa na wawakilishi wa vyama vya kisiasa vya nchi zilizokuwa huru wakati huo pamoja na vile vya nchi zisizokuwa huru, vyama vya wafanyakazi pamoja na mavuguvugu mengine.
Lengo lilikuwa kupigania uhuru wa makoloni, kuziimarisha nchi zilizokuwa huru na kuupinga ukoloni mamboleo. AAPC ilikuwa na sekretariati yake mjini Accra na katibu mkuu wake wa kwanza alikuwa George Padmore mzaliwa wa Trinidad.
Tukiyaacha mavuguvugu hayo ya Umajumui wa Kiafrika kulikuwako pia na nchi za Kiafrika zilizoonyesha ari ya Umajumui wa Kiafrika katika jitihada zao za kuzisaidia nchi nyingine zijikomboe.
Hapa ndipo tunapoona mchango wa Tanzania wa kuisimamia Kamati ya Ukombozi ya Umojawa Nchi Huru za Kiafrika na pili msaada wake wa kuvisaidia vyama vya ukombozi vya Msumbiji, Angola na Namibia.
Zambia nayo kadhalika ilitoa mchango mkubwa kusaidia ukombozi wa nchi zilizo kusini mwa Afrika na Guinea-Conakry ilikisaidia chama cha ukomboziwa Guinea-Bissau na Cape Verde, PAIGC.
Nchi nyingine iliyokuwa huru na iliyojitolea kusaidia ukombozi wa Afrika ni Morocco ikiwa chini ya Mfalme Mohammed wa Tano.
Serikali ya Morocco, nikiutaja mfano mmoja tu, ilikisaidia sana chama cha KANU cha Kenya. Nakumbuka siku ambayo Joseph Murumbi, ambaye baadaye alikuwa makamu wa Rais wa Kenya, alivyokuwa akisafiria paspoti ya Morocco wakati Kenya ilipokuwa chini ya utawala wa Kiingereza.
Mbali ya nchi kuna na watu. Au tuseme ‘mijitu’, mashujaa wa ukombozi wa Afrika. Ninawadhukuru wachache tu hapa: Kwame Nkrumah, Ahmed Ben Bella, Gamal Abdel Nasser, Ahmed SekouTouré, Modibo Keita, Haile Selassie, Jomo Kenyatta, Julius Nyerere, Kenneth Kaunda, Patrice Lumumba, Agostinho Neto, Amilcar Cabral, Eduardo Mondlane na Samora Machel.
Nimewataja wanaume lakini kulikuwako na wanawake walioshika bunduki. Mfano mzuri ni Josi na Muthemba Machel wa Msumbiji.
Kweli sikatai kwamba baadhi ya hao mashujaa wa Kiafrika walizifuja nchi zao baada ya uhuru. Wengine waligeuka kuwa madikteta.
Lakini hayo ni mengine. Hayo ni ya hapo. Ya sasa ni mengine. Afrika ya leo si ya miaka 20 au 30 iliyopita. Imetoka mbali na imepiga hatua.
Sasa takriban nchi zote za Kiafrika ni huru (nchi 54) tukiziacha zile za Sahara ya Magharibi, Mayotte (kimoja kati ya visiwa vine vya Comoro ambacho bado kinatawaliwa na Ufaransa) na visiwa vya Chagos ambavyo ni vya Mauritius lakini vinavyokaliwa na Uingereza.
Sasa wakazi wa Afrika wanapindukia watu bilioni moja na idadi hiyo inaongezeka kwa kima cha watu wapatao milioni mbili na laki tatu kila mwaka.
La kutia moyo na ambalo wakati huohuo linatoa changamoto kubwa ni ujana wa wakazi hao wa Afrika. Kwa mujibu wa takwimu zilizopo asilimia isiyopungua 70 ya wakazi haoni vijana walio chini ya umri wa miaka 25.
Changamoto inayotukabili ni kwamba wengi wa vijana hao hawana ajira. Na hawa si vijana wasiona ujuzi, wasio na elimu. Ni vijana waliosoma kuwashinda wazee wao.Lakini hawana mbele hawana nyuma.
Takwimu zinaonyesha pia kwamba Afrika inainuka kiuchumi.Lakini kuna tatizo:wananchi wanazidi kuwa masikini na kwenye kaumu hiyo wamo hao vijana.
Miaka zaidi ya 50 tangu 1960, uliokuwa ukiitwa Mwaka wa Afrika, bado hatuna uwezo wa kujilisha wenyewe. Ni wazi kwamba ile ajenda yetu ya kiuchumi NEPAD, imeshindwa kutukwamua.Lazima tujiulize kwanini?
Kwa nini madaktari wetu wanakimbilia Ulaya na Marekani ilhali tuna ukosefu mkubwa wa madaktari barani Afrika?
Kwa nini mpaka leo hatukuweza kuifanya iwe haki ya kimsingi kila mtu barani humu kupata maji safi na huduma ya afya?
Kwa nini serikali zetu zina tabia ya kuwaonea raia na kwa nini wanaume tunawaonea wanawake?
Kwa nini Muungano wa Afrika uwe unagharimiwa na wengine? Kwa nini takriban asilimia 90 ya fedha zake zinatoka kwa wafadhili, taasisi za kibeberu? Kwa nini baadhi ya nchi wanachama hazilipi ada zao?
Ikiwa hali ni hiyo ile dhana ya Umajumui wa Kiafrika si itajiangamiza yenyewe?
Tuna mengi ya kuuliza, mengi ya kusema, mengi ya kutufanya tufoke.
Lazima tutambue kwamba maslahi ya Afrika si sawa na maslahi ya madola makubwa au ya mabara mengine. Na tukitambua hayo inafaa tujiandae kuwawezesha vijana wetu hasa kwa vile wakazi wa Marekani na wa bara la Ulaya wanazeeka.
Ili Afrika izidi kupata ufanisi miaka 50 ijayo Umajumui wa Kiafrika utapaswa uunganishe nguvu zake na zile za serikali za Kiafrika, za Waafrika walioughaibuni na zile za mavuguvugu ya umma pamoja na asasi za kiraia.
Vijana wa leo wana jukumu kubwa la kuifafanua Ajenda ya Kiafrika itayoweza kuungwa mkono na wengi barani humu. Ili Umajumui wa Kiafrika uwe na maana katika karne hii ya 21 vijana watabidi wanadi waziwazi kwamba lengo lao ni ukombozi wa pili wa Afrika.
Ajenda yao iwe ni ajenda ya ukombozi, ya kuyakomboa mawazo. Lazima wahubiri mapinduzi,mapinduzi ya mawazo, mapinduzi ya namna tunavyojiangalia, mapinduzi ya kubadili jinsi tunavyo yakabili na kuyatanzua matatizo yetu.
Mapinduzi hayo au ukombozi huo ni muhimu ikiwa tunataka tuwe na kizazi kipya cha viongozi kilichoroa ari ya Umajumui wa Kiafrika.
Wale wasemao kwamba hii ni karne ya Afrika hawajakosea. Lakini lazima tuhakikishe kwamba hivyo ndivyo ilivyo.
Ikiwa vijana wetu hawatoweza kuanza kuibadili hali ya Afrika basi tusahau; Afrika itaendelea kubwagwa chini mpaka litapolia baragumu la mwisho wa dunia.
CHANZO: RAIA MWEMA

WABUNGE WANASWA KATIKA DANGURO LA UCHI MJINI DODOMA....WALIKUWA WAKITOA PESA KWA KUZIWEKA MAKALIONI

Katika ukumbi maarufu wa muziki au kwa jina jingine ‘club’ (jina linahifadhiwa) uliopo mjini  Dodoma mengi yanatokea.

Watu wanaingia mmoja mmoja, wengine kwa makundi na baadhi wapo nje wakipunga kwanza upepo kabla ya kuingia.

Siku hizi wanawake wanaingia bure au kwa jina jingine ‘ladies free’ jambo linalosababisha ukumbi huu ufurike watu.

Katika ukumbi huu, yapo maeneo mawili. Kuna sehemu ya kawaida ambayo kiingilio chake ni kuanzia Sh5,000 hadi Sh10,000 kutegemeana na matukio au burudani ya siku hiyo.

Pia kuna eneo jingine ambalo ni kwa watu maalumu ama waweza kusema ni ‘VIP’ ambapo wateja wake hutakiwa kulipa Sh20,000.

Ukumbi wa VIP upo juu na ule wa kawaida upo chini. Hata hivyo maeneo yote haya hujaza watu kwa kiasi kikubwa.

Mwandishi wetu alifika katika ukumbi wa VIP saa tano usiku, hata hivyo bado watu ni wachache katika eneo hili ukilinganisha na kule kwa watu wa kawaida.


Ukumbi wa VIP si mkubwa kieneo . Kuna kaunta ya vinywaji, makochi madogo madogo aina ya sofa yenye meza mbele yake, viti vilivyoizunguka kaunta na katikati ya ukumbi huu kuna meza mbili za duara zenye mti wa chuma katikati.

Kadri dakika zinavyojongea, ndivyo watu wanavyoendelea kumiminika mmoja baada ya mwingine.

Saa saba za usiku ndipo Mwandishi wetu  aliposhuhudia kiongozi mmoja wa kitaifa ambaye hekima zake zinategemewa na Serikali na hata chama chake akiingia katika ukumbi huu akiwa na mabinti wadogo watatu.

Alipata nafasi ya kuketi, katika moja ya sofa zilizokuwa katika ukumbi huo, akaagiza vinywaji na kuendelea kunywa.

Muda wa saa saba, alitokea msichana aliyevaa sidiria na kisketi cha kujimwaga kifupi sana ambacho hata hivyo kiliuonyesha mwili wake waziwazi.

Msichana yule alipanda katika moja ya meza za duara zenye chuma na kuanza kucheza muziki uliosikika katika spika za ukumbi huo.

Baada ya kucheza kwa zaidi ya nusu saa, alivua kisketi cha rangi nyeusi alichokivaa na kukirusha… akabaki na nguo ya ndani aina ya ‘bikini’ ya rangi nyeupe, kisha akaendelea kucheza kwa kupandia vyuma katika meza hizo za duara. 

Baadaye alivua sidiria, akaendelea kucheza na kadri watu walivyokuwa wakimtunza fedha aliendelea kuonyesha ujuzi wake katika kucheza.

Baada ya muziki huo kukolea, msichana huyo alibadilisha mchezo, akalala kifudifudi na kuishusha nguo yake ya ndani hadi nusu ya makalio yake.

Wanasiasa waliokuwepo katika ukumbi huo pamoja na watu wengine walionekana kumpa fedha kwa kumwekea katikati ya makalio msichana huyo kadri walivyofurahishwa na uchezaji wake.

Wakati huohuo mwanasiasa mwingine kijana aliingia ukumbini hapo akiwa na rafiki zake na kuendelea kushuhudia dansi hiyo.

Baada ya kucheza kwa saa kadhaa, msichana yule alishuka katika meza, kisha akapanda msichana mwingine na kuendelea kucheza.

Aliposhuka, aliingia katika choo cha wanawake na kurudi akiwa amevaa suruali aina ya jeans na tisheti. Wanaume waliokuwa eneo hilo walimwita na kumpongeza, huku wakimnong’oneza maneno ambayo…yalikuwa siri yao.

Chanzo chetu cha habari kinaeleza kuwa wasichana hao ni raia wa Kenya ambao wanadaiwa kuwapo nchini kwa ajili ya kucheza dansi za aina hiyo.

“Wanafanya kazi ya kuhudumia wateja hapo kaunta, lakini unapofika wakati wa kucheza wanacheza,” kinasema chanzo hicho.

Kinaeleza kuwa pamoja na kulipwa kiasi cha fedha kama mshahara na wamiliki wa ukumbi huo, wasichana hao wanajipatia fedha wanazotunzwa wakati wa kucheza.

Chanzo kingine cha habari kinaeleza kuwa wasichana hao ni muunganiko au jumuiya ya vijana waliotoka nchi jirani kuja kufanya biashara hiyo ambayo imeshamiri nchini mwao.

Chanzo hicho kinaeleza kuwa, si wanasiasa hao waliokuwapo siku hiyo pekee, bali wanasiasa wa kiume kadhaa wenye majina nchini hufika hapo kutazama wanawake wachezao utupu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Hassan Ngwilizi, Mbunge wa Mlalo (CCM) anasema kwa kuwa wamefanya jambo hilo nje ya Ukumbi wa Bunge hivyo, hawastahili kuhukumiwa bali sheria inatakiwa kuwabana kama wananchi wa kawaida.

Hata hivyo, anasema kitendo hicho ni kinyume cha maadili na hakitakiwi kufanywa na viongozi kama hao.

Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe anasema sheria za nchi haziruhusu kumbi za starehe kuajiri watu wanaocheza utupu. Waziri Chikawe ambaye pia ni Mbunge wa Nachingwea anasema ni aibu kwa viongozi kutazama dansi za namna hiyo na baya zaidi kuwatuza fedha wachezaji.

“Wanapowatunza fedha, ni kama wanasifia hicho kitendo, ni kama wanasema hivi ndivyo inavyotakiwa” anasema Chikawe na kuongeza:

“Hata hivyo, wanapata wapi leseni za kuendesha huduma kama hizo?”

Anasema Tanzania ni nchi inayozingatia maadili ndiyo maana siku za karibuni Bunge lilipiga marufuku ‘kanga moko’ licha ya hao wacheza utupu.

Anaongeza: “Viongozi wanaotakiwa kuwa mfano wa kuigwa wanapoangalia dansi hizo, wanaendelea kumong’onyoa maadili”

Waziri Chikawe aliahidi kuzungumza na naibu wake, Angela Kairuki ili kuchukua hatua stahiki kwa klabu zinazoruhusu wasichana kucheza uchi.


USHAHIDI WA PICHA,MOTO ULIVYOTEKETEZA NYUMBA MKOANI MBEYA-MAKUNGURU

GARI LA KIKOSI CHA ZIMA MOTO MBEYA LIKIELEKEA ENEO LA TUKIO



KIKOSI CHA ZIMA MOTO CHAANZA KAZI


BAADHI YA VYUMBA VIKIENDELEA KUUNGUA

KIKOSI CHA ZIMA MOTO KIKIENDELEA KUZIMA MOTO HUO

MAMA AKILIA KWA UCHUNGU HUKU AKIANGALIA VYOMBO VYAKE VIKITEKETEA KWA MOTO








MWANDISHI WA HABARI WA RADIO YA BOMBA FM AKISAIDIA KUTOA VYOMBO KATIKA MOJA YA MADUKA KATIKA NYUMBA HIYO INAYOUNGUA









MAAJABU,SAMAHIKI HUYU AMEVULIWA HUKO UNGUJA..YAWEZEKANA NDIO KWANZA DUNIANI KUONEKANA

Samaki huyu alivuliwa maeneo ya ''mchangamle kizimkazi Unguja kusini, Watu wengi walikusanyika kumshangaa samaki huyu wa ajabu ambae wavuvi na wakaazi wa maeneo hayo hawakuwahi kumwona, Ndugu msomaji wa