Monday, July 1, 2013

Wanajeshi wa UN kuanza kazi Mali


Umoja wa mataifa hii leo umeanza kupeleka wanajeshi wake nchini Mali na kufikisha idadi ya wanajeshi wanaoshika doria nchini humo na ambao watakuwa chini ya UN hadi, 6,000.
Idadi ya wanajeshi inatarajiwa kufika 12,640 mwisoni mwa Disemba.
Umoja wa Mataifa utachukua jukumu la kushika doria kutoka kwa jeshi la Ufaransa ambalo lilisimamia operesheni ya kuwafurusha wapigananji wa kiisilamu kutoka Kaskazini mwa nchi mwezi Januari.
Jukumu lake la kwanza litakuwa kuhakikisha kuna usalama kabla ya uchaguzi wa urais kufanyika tarehe 28 mwezi huu.
Wapiganaji wa kiisilamu walianza kufanya harakati zao baada ya mapinduzi ya kijeshi yaliyomwondoa mamlakani rais wa taifa hilo huku wapiganaji wa kiisilamu wakitwa udhibiti wa eneo Kaskazini mwa nchi hiyo ikiwemo miji ya Gao, Kidal na Timbuktu ambako waliamuru kutumika kwa sheria kali za kiisilamu.
Ufaransa iliamua kuingilia mzozo huo, baada ya wapiganaji wa kisilamu kutishia kuvamia mji mkuu Bamako.
Tangu mwezi Januari, wanajeshi 4,000 wa Mali, wamechukua udhibiti wa sehemu kubwa ya miji mikubwa nchini humo, lakini wapiganaji kadhaa wamekuwa wakifanya mashambulizi ya kuvizia,
Jeshi la Umoja wa mataifa litajulikana kama Minusma na litahitaji kufanya kazi nzuri.
Harakati za jeshi la Ufaransa zimewafurahisha wengi kwa sababu wamekuwa wakitumia nguvu.
Lakini waasi wametoroka na wananchi wengi wa Mali wanahofia kuwa wanajeshi wa UN huenda wasitumie nguvu kama wanavyofanya wanajeshi wa Ufaransa.

George Bush na Obama wakutana uso kwa uso katika ardhi ya Tanzania leo


Rais wa Marekani, Barack Obama na mtangulizi wake, George W. Bush, leo wanakutana ana kwa ana kwenye ardhi ya Tanzania watakapoweka mashada kwenye Ubalozi wa zamani wa Marekani uliolipuliwa mwaka 1998.


Rais Obama ameweka rekodi ya kuwa mtu wa kwanza mweusi kuchaguliwa kuongoza Marekani, akipokea wadhifa huo kutoka kwa Rais Bush, ambaye aliiongoza taifa hilo kuanzia mwaka 2000-2008.


Kitendo cha vigogo hao kukutana nchini ni cha
kihistoria na kinadhihirisha jinsi Marekani ilivyoipa kipaumbele Tanzania kwa masuala ya diplomasia.

Viongozi hao wawili, wapo Tanzania wakati Rais Obama akimalizia ziara yake ya Afrika na Bush atakuwa na mkewe, Laura, watahudhuria mkutano wa wake za marais wa Afrika unaodhaminiwa na Taasisi ya Bush Foundation.

Pia, Michelle Obama, atahudhuria mkutano huo kabla ya kuondoka kurejea Marekani.

Balozi mbili za Marekani za Dar es Salaam na Nairobi, Kenya zilishambuliwa kwa wakati mmoja Agosti 7, 1998.

Obama ataweka shada kama sehemu ya kumbukumbu ya tukio hilo na Bush ataungana naye katika shughuli hiyo.
Hata hivyo, viongozi hao hawatahutubia wakati wa shughuli hiyo.


Rais Obama ametoa pongezi kwa sera za Bush Afrika hasa kwa kuongoza mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa Ukimwi.


Hata hivyo, utawala wa Rais Obama umejikita zaidi katika mapambano dhidi ya ugaidi.


Kuna kamandi ya Jeshi ya Africom, ambayo ina kazi kubwa ya kukabiliana na ugaidi barani humu.


Operesheni kubwa za Africom zipo nchi za Afrika Kaskazini, Somalia na Afrika ya Kati ambako wanamsaka kiongozi wa Kundi la Waasi la Lord Resistance, Joseph Kony.
Mwananchi

Makao ya chama kikuu yavamiwa Misri 1 Julai, 2013 - Saa 09:43 GMT



Maandamano dhidi ya rais Morsi watu wakimtaka aondoke mamlakani
Waandamanaji wanaopinga serikali nchini Misri, wamevamia makao makuu ya chama tawala cha Muslim Brotherhood mjini Cairo.
Inaarifiwa wamepora mali iliyokuwa kwenye ofisi hizo katika mji wa Moqattam wakitupa baadhi ya vitu nje ya madirisha kabla ya kuiteketeza ofisi yenyewe.
Rais Mohammed Morsi ni rais wa chama hicho cha kiisilamu chenye ushawishi mkubwa.
Awali, vuguvugu la upinzani lililoandaa maandamano hayo, ambayo yameshuhudia mamilioni ya watu wakijitokeza kuandamana nchini Misri, wametoa makataa kwa rais Morsi hadi Jumanne ajiuzulu.
Taarifa iliyotolewa na kundi hilo, Tamarud au (waasi) ilisema kuwa bwana Morsi huenda akakumbana na raia wasiotii sheria kama njia ya kumuonyesha kuwa wanampinga ikiwa hataondoka mamlakani na kuruhusu uchaguzi kufanyika.
Mamilioni ya watu walihudhuria maandamano, nchini kote Jumapili kumtaka Morsi kuondoka mamlakani.
Pande zote husika zilishangazwa na maandamano yanayofanywa dhidi ya Morsi.
Upinzani ni muungano wa vyama vingi, vikiwemo vianvyomuunga mkono rais aliyeng'olewa mamlakani Mubarak pamoja na watu waliojitolea maisha yao kumuondoa mamlakani.
Changamaoto kwano ni kutafuta njia ya kuendwel;eza maandamno yenyewe hadi wanachokitaka kitakapotimia.
Masemaji wa rais Morsi ameitisha mkutano kati ya pande husika.
Kwa hilo kufanikiwa, rais atahitajika kujitolea na kukubali matakwa yao, ikiwemo hata kufanyia katiba marekebisho.
Hakuonyesha dalili za kutaka mwafaka na wanaompinga, alipokuwa anatoa hotuiba yake wiki jana.
Kwa waandamanaji, wanataka aondoke mamlakani kwa kuitisha uchaguzi wa mapema. Kwa sasa vurugu inaonekana zitaendelea kwa muda.

Rais Barack Obama alipowasili Tanzania


Rais Barack Obama wakati wa ziara yake Afrika Kusini
Rais wa Marekani Barack Obama, amewasili nchini Tanzania katika mkondo wake wa mwisho wa ziara yake barani Afrika.
Ziara ya Obama inasemekana kulenga kuimarisha uhusiano wa kibiashara na Afrika huku kukiwa na wasiwasi kuwa Marekani inaachwa nyuma na China katika uhusiano wao na Afrika.
Obama amewasili Tanzania baada ya ziara yake ya Afrika Kusini ambako rais mstaafu Nelson Mandela anaugua.
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na familia yake pamoja na maafisa wake wa serikali na wacheza densi za kitamaduni walimkaribisha Obama na familia yake mjini Dar es Salaam.
Baadhi ya wananchi wa Tanzania kupitia mitandao ya kijamii wamekosoa ziara ya Obama katika nchi yao, wakisema kuwa ziara yake imeathiri shughuli za maisha yao ya kila siku.
Obama alitembelea Senegal kabla ya kupitia Afrika Kusini na kisha Tanzania ambako ziara yake ya Afrika inaishia kabla ya kurejea Marekani.
Obama ameambatana mamia ya wafanyabiashara na swala la uchumi linatarajiwa kupewa kipamboele kwenye ajenda.
Aidha Obama atatembelea kiwanda cha kuzalisha umeme kinachomilikiwa na Marekani kufuatia tangazo lake mwishoni mwa wiki wa mpango wa mabilioni ya dola kufadhili mradi wa uzalishaji wa kawi.
Mpango huo wa miaka mitano, unatarajiwa kuwezesha nchi nyingi Afrika kuweza kupata kawi kwa ushrikiano na nchi zingine za Afrika na sekta binafsi.
Wakati wa ziara yake, nchini Afrika Kusini, kiongozi huyo wa Marekani hakumtembelea Mandela ambaye anasalia kuwa mahututi hospitalini akiigua maradhi ya mapafu.
Duru zinasema kuwa barabara zimefungwa na usalama kudhibitiwa vilivyo, mjini Dar es Salaam.