Monday, June 3, 2013

Gaddafi alificha mali Afrika Kusini piya



Wizara ya fedha ya Afrika Kusini inachunguza tuhuma kwamba mali ya thamani ya kama dola bilioni moja ya Libya ilifichwa nchini humo.
Rais Zuma na Gaddafi mwezi May mwaka 2011 walipokutana Tripoli, Libya
Wakuu wa Libya wamedai kuna dhahabu, almasi na fedha taslim ambazo kiongozi wa zamani wa Libya, Kanali Gaddafi na familia yake, waliziweka Afrika Kusini.
Serikali ya Libya imekuwa ikijaribu kuzipata mali za Kanali Gaddafi katika sehemu mbali-mbali za dunia tangu alipofariki mwaka 2011.
Mwandishi wa BBC mjini Johannesburg anasema watu wengine wamekisia kuwa mali ya hayati Gaddafi ilioko nchi za nje inaweza kufika dola bilioni 80.

No comments:

Post a Comment