Saturday, May 4, 2013

Ghasia zaendelea mjini Conakry, Guinea

 4 Mei, 2013 - Saa 14:49 GMT

Watu kama watatu wameuwawa nchini Guinea katika mapambano baina ya polisi na waandamanaji waliodai uchaguzi huru na wa haki.
Maandamano ya mwezi March mjini Conakry
Ghasia zimekuwa zikiendelea kwa siku ya pili katika mji mkuu, Conakry.
Afisa mmoja wa upinzani alieleza kuwa waliokufa walikuwa wafuasi wa upinzani.
Upinzani nchini Guinea unasema Rais Alpha Conde hakuwashauri kabla ya kutangaza siku ya uchaguzi wa wabunge kuwa tarehe 30 Juni.
Upinzani unataka wafuasi wake wafanye maandamano hadi rais afute uchaguzi huo.
Rais Conde alishika madaraka mwaka wa 2010 baada ya uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia tangu mwaka 1958.
Lakini uchaguzi wa wabunge uliopangwa kufanywa mwaka wa 2011 umekuwa ukiahirishwa kwa sababu wanasiasa wameshindwa kuwafikiana.

Mpaka wa Afghanistan na Pakistan kumoto

 4 Mei, 2013 

Umoja wa Mataifa umeonya juu ya janga jipya liloanza upande wa Pakistan kwenye mpaka wake na Afghanistan, mpaka wenye mzozo.
Askari wa Afghanistan wako zamu kwenye mpaka na Pakistan
Katika miezi michache iliyopita kumezuka mapigano tena mpakani baina ya wanajeshi wa Afghanistan na Pakistan.
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi, UNHCR, limesema kuwa watu zaidi ya 70,000 wamekimbia majumbwani mwao tangu kati ya mwezi wa March.
Rais Hamid Karzai wa Afghanistan amesema serikali yake katu haitatambua mpaka huo ambao uliwekwa mwaka wa 1893 na wakoloni Waingereza - mpaka uloitenga maeneo ya makabila fulani ambayo kijadi yalikuwa pamoja.

Ghasia zaendelea mjini Conakry, Guinea

 4 Mei, 2013 - Saa 14:49 GMT

Watu kama watatu wameuwawa nchini Guinea katika mapambano baina ya polisi na waandamanaji waliodai uchaguzi huru na wa haki.
Maandamano ya mwezi March mjini Conakry
Ghasia zimekuwa zikiendelea kwa siku ya pili katika mji mkuu, Conakry.
Afisa mmoja wa upinzani alieleza kuwa waliokufa walikuwa wafuasi wa upinzani.
Upinzani nchini Guinea unasema Rais Alpha Conde hakuwashauri kabla ya kutangaza siku ya uchaguzi wa wabunge kuwa tarehe 30 Juni.
Upinzani unataka wafuasi wake wafanye maandamano hadi rais afute uchaguzi huo.
Rais Conde alishika madaraka mwaka wa 2010 baada ya uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia tangu mwaka 1958.
Lakini uchaguzi wa wabunge uliopangwa kufanywa mwaka wa 2011 umekuwa ukiahirishwa kwa sababu wanasiasa wameshindwa kuwafikiana.

Kazi za uokozi zasimamishwa Darfur

 4 Mei, 2013 - Saa 13:53 GMT


Kazi za uokozi zilizokuwa zikifanywa Darfur, Sudan, kutafuta wafanyakazi 100 walionasa kwenye mgodi wa dhahabu ulioporomoka Jumatatu zimesimamishwa.
Darfur
Walioshuhudia tukio hilo wanasema msako katika mgodi wa Jebel Amir umesimamishwa kwa sababu ni hatari kuendelea na kazi za uokozi.
Hapo jana waokozi tisa piya walinasa kwenye mgodi huo.
Hakuna aliyenusurika.
Inaarifiwa kuwa migodi midogo-midogo ya Sudan ilitoa dhahabu ya thamani ya zaidi ya dola bilioni-mbili mwaka jana.
Madini hayo yanaipatia Sudan sarafu za kigeni ambazo zilipungua sana baada ya Sudan Kusini kujitenga mwaka wa 2011 na kubaki na visima vingi vya mafuta.

Israel yashambulia ghala ya silaha Syria

 4 Mei, 2013 


Serikali ya Syria bado haikusema kitu kuhusu taarifa kutoka wakuu wa Marekani kwamba ndege za Israel zimefanya mashambulio katika ardhi ya Syria, ambako inaarifiwa ghala ya silaha imeshambuliwa.
Ndege ya Israel

Wakuu wanasema makombora yalifyatuliwa kutoka ndege za Israel ambazo ziliruka kwenye anga ya Libnan, nchi ya jirani.
Huku nyuma kuna taarifa za mauaji zaidi katika miji ya pwani ya Syria kukiwa na tuhuma kuwa raia wengi wamechinjwa na wanajeshi wa serikali na wanamgambo.
Wanaharakati wanaripoti kuwa mauaji ya pili yamefuatia yale ya kwanza katika eneo hilo-hilo la mwambao kaskazini-magharibi mwa Syria.
Wanasema mauaji ya kwanza yalifanywa kwenye kijiji cha al-Beida cha Wasunni, ambacho kilivamiwa na wanajeshi wa serikali siku ya Alkhamisi.
Wanaharakati wamewataja watu 50 ambao wanasema walichinjwa kati yao wakiwemo wanawake na watoto.
Sasa wanaeleza kisa kama hicho kutokea katika mtaa wa Ras an-Naba wa mji wa pwani wa Banias ulio jirani na al-Beida.
Wameonesha picha kwenye internet kama ushahidi, lakini hakuna njia ya kuthibitisha ukweli wa picha hizo.
Picha zinaonesha maiti za wanawake na watoto zimelala ndani ya nyumbao zao, miili mengine imekeketwa na mengine imechomwa.
Mamia ya familia zimekimbia Banias kuelekea kusini kwenye mji wa Tartous, lakini wanaharakati wanasema wakimbizi hao wamezuwiliwa kupata hifadhi katika mji huo.