Monday, June 10, 2013

Mbunge mahakamani kwa uchochezi TZ

 
Wananchi wa mtwara hawataki gesi asilia kusafirishwa popote
Mbunge wa jimbo la Mtwara, eneo ambalo limekumbwa na vurugu hivi karibuni kusini mwa Tanzania amefikishwa mahakamani leo akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi wa vurugu zilizo sababisha vifo vya watu watatu mwezi uliopita.
Hasnain Murji pamoja na watuhumiwa wengine 91 wamefikishwa kwenye mahakama ya wilaya ya Mtwara.
Kwa muda huu baadhi ya watuhumiwa wamepata dhamana huku wengine wakiendelea na taratibu za kukamilisha udhamini, wakati Mbunge huyo akisubiri kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayo mkabili.
Wananchi waliofika mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi zinazowakabili ndugu na jamaa zao wamelalamikia utaratibu wa kuwazuwia kuingia mahakamani hapo.
Mbunge huyo wa Chama kinacho tawala nchini humo CCM, alikamatwa na kushikiliwa na jeshi la Polisi mkoani humo siku ya Jumamosi.
Idadi kubwa ya wananchi wa Mtwara wamekuwa katika mvutano mkali na Serikali ya Tanzania ambayo imekusudia kujenga bomba la kusafirisha gesi asilia inayopatikana mkoani humo hadi Dar es Salaam , Hatua inayopingwa na wananchi hao ambao wanadai gesi hiyo isisafirishwe na kupelekwa popote.

Mbunge mahakamani kwa uchochezi TZ


Wananchi wa mtwara hawataki gesi asilia kusafirishwa popote
Mbunge wa jimbo la Mtwara, eneo ambalo limekumbwa na vurugu hivi karibuni kusini mwa Tanzania amefikishwa mahakamani leo akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi wa vurugu zilizo sababisha vifo vya watu watatu mwezi uliopita.
Hasnain Murji pamoja na watuhumiwa wengine 91 wamefikishwa kwenye mahakama ya wilaya ya Mtwara.
Kwa muda huu baadhi ya watuhumiwa wamepata dhamana huku wengine wakiendelea na taratibu za kukamilisha udhamini, wakati Mbunge huyo akisubiri kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayo mkabili.
Wananchi waliofika mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi zinazowakabili ndugu na jamaa zao wamelalamikia utaratibu wa kuwazuwia kuingia mahakamani hapo.
Mbunge huyo wa Chama kinacho tawala nchini humo CCM, alikamatwa na kushikiliwa na jeshi la Polisi mkoani humo siku ya Jumamosi.
Idadi kubwa ya wananchi wa Mtwara wamekuwa katika mvutano mkali na Serikali ya Tanzania ambayo imekusudia kujenga bomba la kusafirisha gesi asilia inayopatikana mkoani humo hadi Dar es Salaam , Hatua inayopingwa na wananchi hao ambao wanadai gesi hiyo isisafirishwe na kupelekwa popote.

Hali ya Mandela inasemekana kuwa tete


Mandela ndiye aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi
Rais mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela, angali katika hali mbaya ingawa imeweza kudhibitiwa. Mandela amelazwa katika hospitali moja mjini Pretoria.
"mzee Mandela yuko hospitalini na hali yake bado haijabadilika.''
Maombi yakekuwa yakifanywa makanisani kote nchini Afrika Kusini kumuombea Mandela ambaye anatibiwa kwa ugonjwa wa mapafu.
Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alipelekwa hospitalini mapema Jumamosi , ikiwa ni mara ya tatu kulazwa hospitalini mwaka huu.
Kwa mujibu wa duru za urais, Mandela amekuwa akiugua kwa muda mjini Johannesburg baada ya kukumbwa tena na ugonjwa wa mapafu.
Alilazwa hospitalini baada ya hali yake kuwa mbaya zaidi mnamo Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa za urais, Rais President Jacob Zuma, amerejelea wito wake kwa watu nchini Afrika Kusini kumuombea Madiba wakati huu anapougua.
Lakini mwandishi wa BBC mjini Pretoria, Karen Allen, anasema kuwa kuna matumaini amdogo kuwa Mandela aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, huenda kupona.
Anasema kuwa wengi walipata matumani baada ya bintiye Mandela Zindzi, kusema kuwa babake yuko salama na kuwa anaendelea kupata nafuu.
Mkewe Mandela Graca Machel, alifutilia mbali, ziara yake mjini London Jumamosi ili kuwa kando ya mumewe.
Mandela alikuwa Rais wa Afrika Kusini kati ya mwaka 1994 hadi 1999.
Alifungwa jela miaka 27 na anaaminika kuwahi kuugua ugonjwa wa mapafu alipokuwa akifanyishwa kazi ngumu katika machimbo ya mawe akiwa jela.
Sorry, there has been a problem displaying comments, we are working to fix this.

Winnie , amzuru Mandela hospitalini

 

Mandela na Winnie , katika siku za furaha
Mke wa zamani wa Nelson Mandela, Winnie amewasili katika hospitali nchini Afrika Kusini, ambako inaaminiwa rais huyo mstaafu anaendelea kupokea matibabu kwa ugonjwa wa homa ya mapafu.
Mtoto wao wa kike Zenani (mandela - Dlamini) pia amerejea nchini Afrika Kusini kutoka Argentina ambako anahudumu kama balozi wa Afrika Kusini, ili awe na babake.
Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alipelekwa hospitalini mapema Jumamosi , ikiwa ni mara ya tatu kulazwa hospitalini mwaka huu.
Kwa mujibu wa duru za urais, Mandela amekuwa akiugua kwa muda mjini Johannesburg baada ya kukumbwa tena na ugonjwa wa mapafu. Msemaji wa serikali Mac Maharaj amesema kuwa maafisa katika hospitali wanataka kudhibiti idadi ya watu wanaozuru hospitali hiyo ili wampunguzie bwana Mandela usumbufu.
risala za heri njema na afueni kwa rais mstaafu Nelson Mandela
Alilazwa hospitalini baada ya hali yake kuwa mbaya zaidi mnamo Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa za urais, Rais President Jacob Zuma, amerejelea wito wake kwa watu nchini Afrika Kusini kumuombea Madiba wakati huu anapougua.
Lakini mwandishi wa BBC mjini Pretoria, Karen Allen, anasema kuwa kuna matumaini madogo kuwa Mandela aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, huenda akapona.
Anasema kuwa wengi walipata matumani baada ya bintiye Mandela Zindzi, kusema kuwa babake yuko salama na kuwa anaendelea kupata nafuu.
Mkewe Mandela Graca Machel, alifutilia mbali, ziara yake mjini London Jumamosi ili kuwa kando ya mumewe.
Mandela alikuwa Rais wa Afrika Kusini kati ya mwaka 1994 hadi 1999.
Alifungwa jela miaka 27 na anaaminika kuwahi kuugua ugonjwa wa mapafu alipokuwa akifanyishwa kazi ngumu katika machimbo ya mawe akiwa jela.