Saturday, May 18, 2013

MLINZI WA BAR ACHINJWA KIKATILI NA MAJAMBAZI USIKU WA KUAMKIA LEO



Mlinzi wa baa ya Darajani Stop Over iliyo kando kando ya barabara kuu ya Morogoro Dar es salaam jirani na daraja la Mzambarauni  Bw Mika Athumani amechinjwa na majambazi usiku wa kuamkia leo.


Habari zilizopatikana eneo la tukio zilidai kwamba majambazi hayo yalivamia baa hiyo iliyojitenga usiku wa manane na kumvamia mlinzi huyo na kumchinka kama kuku na baadae kuvunja baa hiyo na kuimba vitu mbali mbali.

Mwili wa marehemu ukiwa ndani ya gari, la polisi kufuatia mwili huo kutenganiswa vibande viwili..



Sehemu aliyochinjiwa mlinzi huyo aliyefahamika kwa jina Mika Athumani.
Akihojiwa na mwandishi wetu,  mmiliki wa baa hiyo Bw Salvatory Mushi alidai kwamba majambazi hao walimvamia mlinzi wake na kumchinja na baadae walivunja Counter ya baa hiyo pamoja na duka ililipojirani na baa hiyo na kuiba vitu mbali mbali.
 

Alipoulizwa kwamba kuna taarifa zinadai kwamba mlinzi huyo alikutwa akiwa amelala Bw Mushi alisema"  inawezekana lakini hakuna mtu mwenye uhakika na jambo hilo kwani sote hatukuwepo,wakti tukio hilo linatokea"
Mwananachi akishuhudia damu ya mlinzi huyo kwa hudhuni
Baskeli ya Mlizni huyo ikiwa imetapakaa damu ambapo inadaiwa mlinzi huyo alikuwa amelala kwenye eneo hilo
Redio ambayo majambazi hayo waliiangusha nje ya baa hiyo
Majaira ya saa 12 asubuhi ya leo wananchi walishuhudia maduka mawili ya baa hiyo yakiwa wazi huku mwili wa mlizni huyo umekutwa upande wa baa ukiwa umechinjwa na kutenganishwa kichwa na mwili
Umati wa watu ukishuhudia tukio hilo muda mfupi uliopita
Gari la polisi likiondoka eneo la tukio na mwili wa marehemu
Wananchi nao waliondoka eneo hilo la tukio
Mmiliki wa baa hiyo Bw Salvatory Mushi akihojiwa na waandishi wa 
habari eneo la tukio

Majirani wa eneo hilo wakihojiwa na waandishi wa habari
Baadhi ya watu waliokuwepo eneo hilo la tukio walidai kwamba mlinzi huyo alikuwa amelala hivyo majambazi hayo yalimvamia na kumpora siraha zake na kishi kumchinja shingoni..
Mwandishi wetu alishuhudia mtoto wa marehemu pamoja na mjukuu wa marehemu wakiangua vilio eneo la tuko baada ya kuuona mwili wa mazazi wao aliyeuwawa kikatili baadae wote wawili walipanda gari la polisi na kuondoka nao.

AIBU: MCHUNGAJI NA WANAKWAYA WATWANGANA NGUMI KANISANI

KATIKA hali isiyo ya kawaida, ugomvi mkubwa umetokea kwenye Kanisa la AICT, kati ya baadhi ya wanakwaya wa kanisa hilo linalofahamika kwa jina la “Bupandwa” na mchungaji wao Petro Masule.


Tukio hilo la aina yake, limetokea kwenye Kijiji Bupandwa,Kata ya Bupandwa, Wilaya ya Sengerema, mkoani  Mwanza.
 
Wanakwaya hao walisimamishwa kutoa huduma Kanisani kwa njia ya uimbaji kwa kosa la utovu wa nidhamu ambapo ugomvi huo, ulitokea Mei 12 mwaka huu, baada ya ibada.

Inadaiwakuwa , Mchungaji Masule hakutumia lugha nzuri baada ya kuwaita wanakwaya hao “watenda dhambi ambao hawapaswi kuingia katika hekalu la Bwana”.

Kauli hiyo inadaiwa kuwakera wanakwaya hao ambao kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, walisema Mchungaji Masule aliyasema hayo katika mahubiri ya ibada ya kwanza.

Mchungaji huyo alidai kuwa, kutokana na makosa waliyotenda wanakwaya hao, wanapaswa kutubu ili waweze kuingia kanisani.
Baada ya ibada hiyo kumalizika, baadhi ya wanakwaya waliokuwa wamesimamishwa ambao walihudhuria misa hiyo, waliamua kuungana na kumfuata Mchungaji huyo akiwa na wazee wa kanisa wakihesabu sadaka.

Wanakwayahao walimuomba Mchungaji huyo awape vyombo vya kuimbia ambavyo walidai kuvinunua kwa fedha zao ili wakaazishe kanisa lao wakidai kukerwa na mahubiri yake.

Kutokana na matakwa ya wanakwaya hao, ilitokea vurugu kubwa ndani ya kanisa hilo kati yao na Mchungaji Masule, ambapo katika ugomvu huo, inadaiwa muumini mmoja aliumia sehemu mbalimbali za mwili wake.

Gazeti hili lilipomtafuta Mchungaji Masule, alikiri kuzipiga na wanakwaya ndani ya kanisa hilo ambao walikiuka maadili na matakwa ya kanisa kwa kutokufuata sheria na kanuni.
Kwa upande wake, Mtendaji wa kijiji hicho, Bw. Vincent Ngidingi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, kulaani kitendo kilichotokea kanisani hapo na kuwaasa waumini kufuata sheria za kanisa.

HOFU YATANDA BUNGENI KUTOKANA NA TETESI ZA SHAMBULIO LA KIGAIDI MJINI DODOMA


Wabunge wa Taznzania wakiwa katika vikao vyao

Hali ya wasiwasi imelikumba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kuwepo kwa tetesi ya shambulio la kigaidi katika maeneo ya Bunge.


Hali hiyo inafuatia ujumbe mfupi wa maneno uliosambazwa, ukitaadharisha kuwa kuna tukio la kigaidi limepangwa kufanywa katika eneo la Bunge.

Ujumbe huo uliosambazwa kwenye simu za baadhi ya wabunge ulisomeka hivi:-

"Kuna kikundi kina mkakati wa kufanya shambulio la bomu bungeni Dodoma na msikiti wa Msavu Morogoro. Ni ndani ya muda mfupi wakati bado vikao vya Bunge,"ailisema sehemu ya ujumbe huo.


Habari zaidi zinasema kuwa tayari jeshi la polisi imefanikiwa kupata mtu aliyetuma ujumbe huo, ambaye anadaiwa kutuma kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini na wamefanikiwa kumleta mjini hapa kwa mahojiano zaidi ili kufanikisha upelelezi.



Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge, Mussa Azzan Zungu, juzi alilitangazia Bunge hali hiyo ya hatari  wakati wabunge wakiendelea na mjadala wa hotuba ya makadirio ya matumizi wizara ya Uchukuzi ya mwaka 2013/14, na kulazimika kurudia tangazo hilo wakati akiharisha Bunge.  


“Waheshimiwa wabunge wote mnaombwa kuanzia kesho tarehe 17, mwezi huu, mwaka huu, kutoegesha magari yenu pembezoni mwa uzio unaozunguka ofisi ya bunge hapa Dodoma…Badala yake magari hayo yaingizwe katika geti la eneo la maegesho ya waheshimiwa wabunge ndani ya viwanja vya Bunge” alisema Zungu

Alisema mbunge yeyote atakaye taka kuegesha gari lake nje ya ofisi, anaombwa aegeshe ng’ambo ya upande wa kaskazini wa barabara itokayo jijini Dar es Salaam.


Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alisema ulinzi umeimarishwa katika eneo lote la Bunge kuhakikisha hakuna chochote cha hatari kinachoweza kutokea.

“Vijana wangu wanafanya kazi yao vyema na iwapo kuna tishio lolote lile litafanyiwa kazi,” alisema Dk Nchimbi

Dk Nchimbi alisema ulinzi utaendelea kuimarishwa katika eneo hilo kuliko wakati wowote ambao Bunge limewahi kuwekwa katika usalama.

MAALIM SEIF AFUNGUA RASMI MRADI MPYA WA MAJI NUNGWI.


maji

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amewataka wananchi wa Nungwi kuulinda na kuuenzi mradi wa maji safi na salama katika eneo hilo ili uweze kuwa endelevu.

Amesema mafanikio ya mradi huo yatachangia maendeleo ya kiuchumi katika eneo hilo na kuwa mfano kwa maeneo mengine ya Zanzibar na Tanzania kwa jumla.

Maalim Seif ametoa wito huo katika sherehe za ufunguzi wa mradi wa maji safi na salama unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika shehia ya Nungwi, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Amesema mradi huo ambao ni wa kihistoria katika eneo hilo unapaswa kulindwa na kuenziwa ili usiharibiwe na n kuweza kudumu kwa muda mrefu.
Amefahamisha kuwa mradi huo ni mkombozi kwa wananchi wa vijiji vya Nungwi hasa wanawake, na kwamba umeondoa kero ya muda mrefu ya ukosefu wa maji safi na salama kwa wananchi wa maeneo hayo.
Aidha Maalim Seif amewata watendaji wa Mkoa huo kutowaone muhali waharibifu wa mazingira wakiwemo wale wanaochukua mchanga katika maeneo ya fukwe na maeneo mengine yasiyoruhusiwa, wanaofanya uvuvi haramu pamoja na ukataji wa miti ovyo.
Ameeleza kuwa zaidi ya maeneo 148 ya kilimo Zanzibar yameainishwa kuvamiwa na maji ya chumvi na kuathiri shughuli za kilimo katika maeneo mbali mbali sambamba na kupungua kwa eneo la ardhi ya visiwa vya Unguja na Pemba.
Mara baada ya kufungua mradi huo, Makamu wa Kwanza wa Rais aliukabidhi kwa Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati ili aweze kuundeleza kwa maslahi ya wananchi hao.
Kwa upande wake Mwakilishi wa UNDP Tanzania Njeri Kamau amewapongeza wananchi wa Nungwi kwa ushirikiano wao katika utekelezaji wa mradi huo, na kuwataka kuendeleza umoja na mshikimano katika kutekeleza miradi mengine ya maendeleo.
Amesema ametiwa moyo na mafanikio yaliyopatikana kutokana na mradi huo na kuahidi kuendelea kushirikiana na serikali pamoja na wananchi wa Zanzibar katika kutekeleza miradi mbali mbali.
Nae Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati Mhe. Ramadhan Abdallah Shaaban, amesisitiza kuwa mradi huo ni kwa ajili ya wananchi wa Nungwi na sio kwa shughuli za mahoteli.
Aidha amesema wanakusudia kuweka “stabilizers” katika vituo vya mradi huo ili kuepusha uunguaji wa pampu za maji unaotokea mara kwa mara, hali inayosababishwa na hitilafu za umeme.
Mapema akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt. Omar Dadi Shajak, amesema mradi huo ni mkubwa zaidi na umekuwa wa mwanzo kufunguliwa kati ya miradi minne unayotekelezwa chini ya mradi wa Mpango wa Mabadiliko ya Tabia nchi Afrika, African Adaptation Program AAP nchini Tanzania.
Amesema mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha lita thelathini elfu (30,000) kwa saa ambao umegharimu zaidi ya shilingi milioni mia tano (500), umefadhiliwa na serikali ya Japan kupitia ubalozi wake nchini Tanzania, UNDP chini ya usimamizi wa AAP.
Akisoma risala kwa niaba ya wananchi wa Nungwi, mwalimu Hassan Jani Massoud ameishukuru serikali kwa kuwapelekea mradi huo ambao utapunguza athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.
Amesema kabla ya kuja kwa mradi huo, miradi mbali mbali ya maji ilianzishwa lakini haikuleta ufanisi, lakini mradi huo umeonesha kuleta mafanikio, na kwamba wananchi wa Nungwi wataondokana na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji safi na salama iliyokuwa ikiwakabili kwa muda mrefu.

CD ZA UAMSHO NA ZILE ZA SHEIKH ILUNGA ZAPIGWA MARUFUKU....


Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar inayoongozwa na Dr Shein na Makamu  wake Maalim Seif kupitia Jeshi la Polisi wamepiga marufuku rasmi CD  zote za mawaidha ya Kiislam za UAMSHO,MUJAHID ABOUD ROGO na SHEIKH ILUNGA.
 

Agizo hilo lilitolewa na OCD  wa  zamani Murtad MKADAM ambae kwa  sasa yupo ofisi kuu ya polisi kitengo cha madawa ya kulevya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif.

Alisema cd hizo za kiislam ni chanzo cha uvunifu wa amani hapa nchini na ndio zinazosababisha uchochezi baina ya dini ya ukiristo na uislam.


OCD alibainisha kuwa mpaka sasa wameshawakamata watu kadhaa wanaojihusisha  na  kuuza cd hizo na kuwaonya wale wote ambao huweka kuzisikiliza maana watachukuliwa hatua kwani serikali ina mkono mrefu.
...

Akijibu baadhi ya maswali aliyoulizwa kwamba waliowakamata hawawaoni kuwa wamewadhulumu kwa kufanya biashara halali ya uzaji cd, Ocd alijibu cd zile za mawaidha ni Haram wala sio riziki ya halali kwa upande wa serekali kwani zinapelekea uvunjifu wa Amani katika nchi.

Ajali ya mgodi watu 20 wafariki Congo

 18 Mei, 2013 
Ramani ya DRC
Zaidi ya watu 20 wamefariki dunia wakati mgodi mmoja uliporomoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mamlaka za Congo zinasema mgodi huo ulioko karibu na kijiji cha Rubaye katika mji wa Masisi Kaskazini mwa jimbo la Kivu uliporomoka siku ya Alhamisi Asubuhi.
Meya wa Masisi, Dieudonne Shishuku ameiambia BBC kuwa idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka.
Amesema bado wanasubiri waokoaji maalumu wa vifaa vya kufukua ardhini waanze kazi ya ukoaji ambapo mgodi huo unakadiriwa kufikia mita 30 kwenda chini.
Shughuli zote za uchimbaji wa madini zimesimamishwa mjini humo.
Kumekuwa na shughuli za uchimbaji haramu wa madini kwenye mji huo ambao una utajiri mkubwa wa madini ya dhahabu, madini ya chuma na coltan yanayotumiwa kwa simu lakini eneo hilo limekuwa na mapigano ya muda mrefu.
Faida inayotokana na mauzo ya madini nchini humo, yanaaminika kuchangia pakubwa katika mzozo unaokumba Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, huku idadi kubwa ya raia wa nchi hiyo wakiwa masikini.

Wapenzi wa jinsia moja wabaguliwa Ulaya


18 Mei,

Wapenzi wa jinsia moja huhofia kuripoti kwa polisi visa vya dhulma dhidi yao
Muungano wa Ulaya umetoa ripoti kuonyesha kuwa zaidi ya robo ya wapenzi wa jinsia moja waliohojiwa wameshambuliwa ama kutishwa katika miaka mitano iliyopita.
Ripoti hiyo iliandaliwa na wataalamu wa muungano huo kuboresha sera zinazoelekea kutenga watu kutokana na hulka zao za mapenzi.
Watu elfu tisini na tatu wanaoishi Ulaya walihojiwa kuhusu namna wapenzi wa jinsia moja wanavyochukiwa na kutengwa. Majibu yao yaliyowasilishwa kwenye mtandao yalionyesha katika miaka mitano zaidi ya robo walishambuliwa ama kutishwa.
Na shuleni wanafunzi wawili kati ya watatu waliohojiwa walisema kuwa walificha kuwa wao ni wapenzi wa jinsia moja.
Kinachotia wasiwasi ni kuwa zaidi ya nusu yao hawako radhi kuripoti visa vya kushambuliwa kwa polisi kwa sababu wanaamini kuwa hakuna kitakachofanyika.
Wanasiasa na watunga sera mia tatu wanakutana Hague Uholanzi kujadili njia mpya za kuwalinda watu na kuhakikisha kuwa hawashambuliwi hata wakipendelea mapenzi ya jinsia moja.

Serikali yafuta kinyemela mtihani wa somo la Islamic


natoka Uk. 1
Afisa huyo akasemakuwa wao kama Bakwatawameshangaa na kushtukasana.Akasema kuwa pamojana kuwa hawakushirikishwawanakuja kupewa tu taarifa,lakini wanashangaa pia kwasababu hata walipopewataarifa na Kamishna waElimu, wameambiwa jambohilo liwe siri.Jambo hili linafanywa“SIRI, je Serikali inatakaWaislamu wasiambiwe?Kwanini? Kun                                                             agenda gani?Amehoji afisa huyo ambayehata hivyo hakutaka kutaja jina lake akisema kuwa yeyesio msemaji wa Bakwata.Awali taarifa juu ya kikaocha Wakristo na Wizara juu ya mitihani ya dini,zilianza kuvuja kupitia kwaWakristo waliohudhuriaambao walipokutana nawadau kutoka upande waWaislamu waliwalaumu nikwa nini hawakuhudhuriawakasaidiana kupinga uamuzihuo wa Serikali.Hata hivyo, wadau haokutoka Islamic EducationPanel waliwafahamishawadau hao wa Kikristo kuwa Ni rai yetu kwamba,madhali serikali imeonyeshania ya dhati katika kuletaumoja na upendo kwawananchi wake kidini, basifursa hiyo pia itumike kwakuwaacha Waislamu. Iachekurasimisha kuwa msemajiwa Waislamu ni Bakwata.Kama kuna jambo linahitajimawazo ya Waislamu, basimawazo yao hayawezikuwasilishwa na BAKWATA pekee. Lazima taasisi nyinginezinazowakilisha Waislamuzisikilizwe.Tunayasema hayatukizingatia kauli za baadhiya Wabunge hivi karibuniambao kauli zao zinaonyeshakuwa hueda Muislamu akiwanje ya Bakwata, anatafsiriwakama muhalifu au kavunjasheria za nchi.Lakini tunayasema haya pia tukizingatia kauli zawale waliosema kuwa hatuaya Serikali ya kuwadhibitiWaislamu chini ya Bakwata,na kwa namna moja aunyingine, kuingilia utendajiwa Baraza hilo, ikiwa ni pamoja na kuhusika katikakuweka viongozi wa ngaziza juu, ni ukandamizaji nakinyume cha sheria kwasababu haifanyi hivyo kwataasisi za dini nyingine.Wakataka Waislamuwaachwe.