Wednesday, June 5, 2013

FAHAMU KUHUSU BOTI MPYA YA KAMPUNI LA S.S.B ILOSHUSHWA LEO ZANZIBAR


Boti mpya ya kisasa ya Azam Marine, Kilimanjaro IV ikiwa imeshushwa katika bahari ya Hindi eneo la Zanzibar  mchana wa leo tayari kuanza kazi kwa safari za Dar es Salaam na Zanzibar.

Mmiliki wa Makampuni ya S.S. Bakhresa, Alhaj Said Salim Awadh Bakhresa (katikati) akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Maji Zanzibar (ZMA) na kushoto ni mmoja wa wafanyakazi wa kampuni yake, Jaffar Iddi 

Kilimanjaro IV kabla ya kushushwa kwenye Meli iliyoileta nchini

Inashushwa...

Inateremshwa majini

Azam Marine wamekarabati pia eneo la abiria kupumzika wakisubiri usafiri na mfumo mzima wa huduma hadi ofisi za kisasa

Ofisi mpya za Idara ya Uhamiaji Azam Marine

Ofisi mpya ya Polisi

Abiria wanastarehe sasa

Burudani kwenye Luninga kubwa wakati unangoja boti

Meneja Mkuu wa Azam Marine, Omar Mohamed Said kushoto akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Kilimanjaro IV

Mzee Bakhresa alikuwa bize mpaka basi leo

Anatazama Meli inavyoshushwa

Mwonekano wa Nje unapoelekea kupanda boti za Azam Marine

Mzee Bakhresa na Jaffar Iddi nyuma

Mzee Bakhresa akifuatilia uteremshwaji wa Meli 

Mzee Bakhresa akitoa maelekezo

Namna hiyo, kila kitu kinakwenda sawa

Mzee Bakhresa

Mzee Bakhresa pembeni ya Abdulrazak, moja kati ya majembe ya Azam Marine(SANTE BIN ZUBERY )

Baaas, iwekeni hapo hapo na mtie nanga; Mzee Bakhresa akitoa maelekezo

Shirdon atoa wito kwa Afrika Kusini kuwalinda raia wa Somalia

Somalia Abdi Farah Shirdon alielezea wasiwasi wake kuhusu usalama wa Wasomali nchini Afrika Kusini, na kutaka serikali ya huko kuingilia kati ili kuzuia vurugu dhidi ya watu wa Somalia baada ya mashambulizi ya mauaji huko Pretoria na Port Elizabeth wiki iliyopita.
"Ninaiomba serikali ya Afrika Kusini kama suala la dharura kuingilia kati na kuzuia vurugu zisizokuwa za lazima na za bahati mbaya dhidi ya jamii za wafanyabiashara wa Somalia ili kudumisha amani na utulivu, kwa hivyo kuimarisha na kukuza mahusiano ya kidugu baina ya watu wetu na serikali zetu," Shirdon alisema katika barua kwa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma siku ya Jumatatu (tarehe 3 Juni).
Matamshi hayo ya waziri mkuu yanakuja baada ya mfululizo wa mashambulizi dhidi ya wafanyabiashara wa Somalia nchini Afrika Kusini wiki iliyopita, ikiwemo mashambulizi ya kikatili dhidi ya Abdi Nasir Mahmoud mwenye umri wa miaka 25.
Mahmoud alipigwa mawe hadi kufa na kundi la watu huko Port Elizabeth siku ya tarehe 30 Mei na video ya simu ya mkononi ya shambulio hilo ilitolewa katika intaneti hivi karibuni. Polisi wanachunguza tukio hilo, lakini hakuna mtu aliyekamatwa bado.
Shirdon alituma rambirambi zake kwa familia za wahanga waliouliwa, kujeruhiwa au kupoteza mali zao wakati wa vurugu za hivi karibuni huko Pretoria na Port Elizabeth.
"Kwa upande mwengine, pia ninawataka Wasomali walioko Afrika Kusini kuheshimu na kufuata kikamilifu sheria na mila za huko, kufanya kazi na Ubalozi wa Somalia mjini Pretoria, kudumisha utulivu, kuelewa kwamba serikali yangu itafanya kazi kikamilifu na serikali ya Afrika Kusini ili kushughulikia matatizo haya yanayotokea," alisema waziri mkuu. "Mawazo yetu yako pamoja na Wasomali ambao wameteseka katika kipindi hiki cha huzuni."
Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia ilitangaza hapo Jumanne kwamba ilikuwa inapeleka ujumbe huko Afrika Kusini katika juhudi za kutatua mzozo huu wa kiusalama ambao unaiathiri jamii ya Wasomalia.
Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje Abdisalam Haji Ahmed Liban alilaani mashambulizi hayo dhidi ya wananchi wa Somalia na kuelezea kusikitishwa kwake na njia ya kikatili ambayo Mahmoud aliuawa.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari Liban aliitaka serikali ya Afrika ya Kusini kuwalinda Wasomalia na kuharakisha kuwakamata waliotenda uovu.

Wakaazi wa Mogadishu wapokea kwa furaha, waahidi kulinda taa za barabarani za nguvu ya jua

Kadiri utawala wa mkoa wa Benadir unavyojiandaa kufunga taa za barabarani zinazotumia nguvu ya jua kwenye barabara 30 katika wilaya nne za Mogadishu, maofisa walizindua kampeni ya kuuelimisha umma kwa wakaazi kutunza taa hizo.
    Mafundi wakifanya kazi ya kufunga taa za nguvu ya jua katika barabara ya Maka al-Mukarama huko Mogadishu. Wakaazi wasema taa hizo zinawakumbusha fahari ya zamani ya mji mkuu wa Somalia. [Mustafa Abdi/AFP]
  • Mafundi wakifanya kazi ya kufunga taa za nguvu ya jua katika barabara ya Maka al-Mukarama huko Mogadishu. Wakaazi wasema taa hizo zinawakumbusha fahari ya zamani ya mji mkuu wa Somalia. [Mustafa Abdi/AFP]
Manispaa ya Mogadishu inapanua programu yake ya kuweka mwanga katika mji mkuu kwenye barabara kubwa nyakati za usiku, kutoa fursa kwa biashara kuendelea kuwa wazi nyakati za usiku na kusaidia raia kuhisi salama.
Barabara zilizolengwa kuwekewa taa mpya ni zile za upili katika maeneo ya wakaazi ya wilaya za Warta Nabada, Hodan, Howlwadag na Yaqshid. Kipaumbele kitatolewa kwa wilaya nne kutokana na usalama ulioboreshwa kwani sehemu kubwa ya wakaazi wanarudi nyumbani kwao katika maeneo hayo, kwa mujibu wa maofisa.
Kabla ya kufungwa, maofisa wa Benadir walikuwa na mikutano ya kupeana taarifa ya wiki moja na wakaazi kuwaelimisha kuhusu kwa nini taa za barabarani ni muhimu kwa usalama wa umma katika viunga vyao.
"Tunafanya kampeni hii ya mwamko kabla hatujafunga taa ili watu waelewe umuhimu wa kufanya kazi kwa usalama na kuchukulia kwamba ni wamiliki na kuzilinda kama mali yao, badala ya kuziona taa kama mali ya wengine," Gavana Msaidizi wa Benadir Iman Ikar Nur aliiambia Sabahi.
Wakaazi wanapaswa kuwa waangalifu na kufuatilia kwa karibu magenge ya vijana na wanaoshukiwa kuendesha al-Shabaab ambao wangetaka kuziharibu taa ili waweze kufanya shughuli zao kwenye giza, Nur alisema.
Serikali ya Uingereza imetoa mchango wa taa za umeme jua zaidi ya 100, na ufungaji utaanza mapema ambao utafanywa na Chama cha Msaada wa Kimataifa cha Nordic, Nur alisema.
"Jitihada za utawala wa Benadir ni jambo la kufurahia, kwa kuwa utatupa uwezo wa kutoka nje [usiku] na kubainisha watu wakati kuna tukio ambalo linatishia usalama," alisema Sahra Abdi Nur, mama wa watoto wanne mwenye umri wa miaka 28 ambaye alihudhuria programu ya mwamko katika Kituo cha Utafiti na Mjadala katika wilaya ya Hodan.
"Kwa sasa kila mtaa katika maeneo ya jirani yetu kuna giza usiku na huthubutu kutembea katika giza," aliiambia Sabahi.
Amina Yasin, raia wa Howlwadag mwenye umri wa miaka 32, alisema taa za barabarani zitakuwa kama zana katika kuhakikisha usalama.
"Katika matukio mengi, wanachama wa kundi la kupinga amani la al-Shabaab wanafanya kazi kwa siri wakati wa usiku, wakati mwingine wanafanya mashambulizi ya kivita kwa wakazi wa maeneo ya jirani," aliiambia Sabahi. Hata hivyo, ufungaji wa taa hizi utasaidia kuzuia operesheni za al-Shabaab na kufuta uwezo wowote uliobaki kupigana na majeshi ya serikali, alisema.
Kwa Mumin Ahmed, mkazi wa wilaya ya Warta Nabada mwenye umri wa miaka 54, taa zitasaidia wananchi kukumbuka ufahari wa zamani wa Mogadishu.
"Kweli, siwezi kukumbuka mara ya mwisho nilipoiona Mogadishu ikiwa na mwanga wa kutosha," aliiambia Sabahi. "Mbali na umuhimu wa kuimarisha usalama, tutakuwa na thamani katika kuanzisha upya uzuri ambao mji mkuu ulikuwa nao. Pia, ni vizuri kufuatilia wale ambao wanaofanya uchafuzi kama vile migahawa ambayo inatumia fursa ya giza kutupa taka mitaani."
Wakazi watazilinda taa za barabarani dhidi ya wahalifu, alisema Mohamed Ali, mzee wa Kiyaqshid mwenye umri wa miaka 65.
"Hatutakubali yeyote ambaye anapinga amani au kupinga kujengwa kwa taa za barabarani katika mitaa ya viunga vinavyotuzunguka, iwapo ni wahalifu au magaidi [wanaojulikana] -- wote wanaofaidi kutokana na giza la barabarani huko Mogadishu," aliiambia Sabahi.
"Ninauambia utawala wa mkoa wa Benadir, mtatosheleza majukumu yenu kama mtafunga taa kwa ajili yetu na tutawajibika kuzilinda, hivyo tuachieni," alisema.

Wasomali watafakari juu ya kuwepo kwa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia

Kwa kumbukumbu ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) iliyoadhimishwa mwaka huu 2013, Wasomali wengi walitoa shukrani kwa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) -- kikosi kilichosaidia kuwaondoa al-Shabaab Mogadishu na kudhoofisha udhibiti wa kikundi hicho cha wanamgambo kwenye nchi hiyo.
    Askari wa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) akisimamia sheria za barabarani katika barabara ya Mogadishu wakati wa operesheni tarehe 25 Mei ambayo ililenga kuboresha usalama katika mji mkuu huo wa Somalia. [Tobin Jones/AU-UN IST/AFP]
  • Askari wa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) akisimamia sheria za barabarani katika barabara ya Mogadishu wakati wa operesheni tarehe 25 Mei ambayo ililenga kuboresha usalama katika mji mkuu huo wa Somalia. [Tobin Jones/AU-UN IST/AFP]
"Tunawashukuru sana AMISOM kwa sababu walituokoa kutoka kwa al-Shabaab," Mkaazi wa Mogadishu Aweys Isse, mwenye umri wa miaka 26, aliiambia Sabahi. "Kwa hakika, wameleta amani na kutuwezesha kupumzika; mji mkuu wetu haukuwahi kuwa katika amani kama ilivyo sasa katika miaka 22."
Vikosi vya Afrika vilifanya jukumu kubwa la kurejesha amani nchini Somalia na kufanikisha misheni ambayo hakuna kikosi kingine cha kigeni kingeweza kufanya, alisema.
"Jiji hili limekuwa na matatizo mengi, lakini leo hii ninaweza kuhisi utulivu," alisema Nadifa Ali, mwenye umri wa miaka 50 mama wa watoto 11 ambaye anauza mirungi huko Beledweyne. "Ninafanya kazi kwa ajili ya watoto wangu na sina hofu kuhusu watoto wangu [usalama] kama ilivyokuwa wakati al-Shabaab walipokuwa wanatawala hapa."
Vikosi vya AMISOM viliingia kwa mara ya kwanza Somalia mwaka 2007. Kimsingi kazi ya misheni hiyo ilijikita katika kulinda amani, lakini vilianza shughuli Mogadishu wakati al-Shabaab ilipokuwa katika kukaribia kuishinda serikali ya mpito ya Somalia. Vikosi vya Afrika vilivisaidia vikosi vya Somalia kuwaondoa al-Shabaab kutoka katika mji mkuu mwezi Agosti 2011 na kuendelea kufanya kazi ya kupunguza ushawishi wake katika majimbo.
Mahi Sufi, mwenye umri wa miaka 32, mwangalizi wa msikiti huko Baidoa, alikumbuka miaka kabla vikosi vya AMISOM na Somalia kuukomboa mji wake kutoka utawala wa al-Shabaab.
"Al-Shabaab ilitutishia na kutufanya kukosa uhuru," aliiambia Sabahi. "Walilazimisha mtazamo wao wa Uislamu kwetu bila ya kuelekeza tabia zao katika kanuni halisi za Uislamu."
"Sasa hivi tuko huru kusoma vitabu vya dini yetu bila ya kumhofia yeyote isipokuwa Mungu," alisema.
Hata hivyo, Abdiaziz Dayah, mwenye umri wa miaka 49, mwalimu wa sekondari ya juu Mogadishu, alisema baadhi ya shughuli za AMISOM zimesababisha matatizo pamoja na mazuri. Tukirejea mashambulizi dhidi ya raia katika mapambano dhidi ya al-Shabaab, alisema AMISOM lazima "wawajibike kwa watu waliowauwa".

Suluhisho la Afrika kwa matatizo ya Afrika

Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Somalia Hussein Farah alisema nchi za Afrika zimepata uzoefu mkubwa kwa kupeleka vikosi vyake Somalia, na kufaulu kwa misheni ya kulinda amani ya AMISOM ni mfano ambao unaweza kuigwa katika sehemu nyingine za bara, kama vile nchini Mali.
"[Nchi za Afrika] lazima zitafute ndani yake suluhisho kwa matatizo ya Afrika na nchi zilizobakia duniani kutoa msaada tu," Farah alisema.
Mwakilishi Maalumu wa Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika kwa ajili ya Somalia Mahamet Saleh Annadif alitathmini operesheni ya AMISOM ya sasa kuwa ni mafanikio.
"[Ushiriki wa AU huko Somalia] ulikuwa ni uamuzi uliofanywa na Afrika kutatua tatizo barani Afrika, na tumefanikiwa katika operesheni hii ambayo iliendeshwa na vikosi vya Afrika tu bila kuvihusisha vikosi vya Umoja wa Mataifa kama zilivyo operesheni nyingine za AU," aliiambia Sabahi.
Kimsingi, Somalia, ilikuwa ni miongoni mwa nchi wanachama waanzilishi wa Shirika la Umoja wa Afrika -- jina asilia la Umoja wa Afrika -- ambalo lilianzishwa huko Addis Ababa, Ethiopia, tarehe 25 Mei, 1963.
Huku ikiingia katika miaka yake ya 51, AU ina matumaini ya kutimiza hata zaidi kushughulikia matatizo yanayoikabili Afrika.
Lakini wachambuzi kama vile Abdikarim Daud, profesa wa sayansi ya siasa katika Chuo Kikuu cha Mogadishu, alikuwa na wasiwasi kama umoja huo una uwezo wa kutimiza malengo makubwa.
"Umoja wa Afrika bado hauna uwezo wake binafsi wa operesheni za kusimamia uletaji amani katika nchi kama vile Somalia," alisema, akiongeza kwamba gharama za uendeshaji za AMISOM zinalipwa na Umoja wa Mataifa.
"Hata hivyo, [nchini Somalia] wametimiza jambo walilokuwa hawawezi kulifanya kabla kwa kushughulikia kwa mafanikio tatizo ndani ya Afrika kwa kuzingatia uamuzi wa AU," Daud, aliyekuwa kanali katika Jeshi la Taifa la Somalia, aliiambia Sabahi.
"[AU] ilikuja kuisaidia Somalia wakati ambapo dunia nzima haikuizingatia Somalia na ilifanikiwa katika kurejesha kwa kiasi fulani utulivu," alisema.

Uhalifu wa hivi karibuni wa al-Shabaab unaonyesha upuuzaji wa sharia

Wanamgambo wa al-Shabaab wamefanya mfululizo wa mashambulio ya ukatili na uhalifu dhidi ya raia katika wiki za hivi karibuni -- utekaji, kukata vichwa na kupora Wasomali katika kupuuza kabisa sheria za sharia ambazo kundi hilo linadai kuzitetea.
  • Askari polisi wa Somalia akisimamia sheria za barabani kwa shughuli zinazoshukiwa za magaidi kwenye eneo la ukaguzi huko Mogadishu. [Tobin Jones/AU-UN IST/AFP] Askari polisi wa Somalia akisimamia sheria za barabani kwa shughuli zinazoshukiwa za magaidi kwenye eneo la ukaguzi huko Mogadishu. [Tobin Jones/AU-UN IST/AFP]
Tarehe 30 Mei, al-Shabaab waliagiza kuachiwa kwa wapiganaji wake sita, waliotuhumiwa kwa kupora dola 6,000 kutoka katika duka la dawa huko Baardheere na kuhukumiwa kukatwa mikono yao ya kuume.
"Nilikusanyika na kundi kubwa kutoka mjini kushuhudia adhabu ambayo ingetolewa kwa wapiganaji sita wa al-Shabaab, kwani tulitarajia mikono yao ya kuume kukatwa," alisema Yusra Nur Abdirahman, mwenye umri wa miaka 28 na mkaazi wa Baardheere. "Cha ajabu, mwakilishi kutoka katika kundi hili [aliyekuwa anahusika kutoa hukumu] Shekhe Aadan Nuh alitangaza kwa kutumia kipaaza sauti kwamba wajahidina hao sita wangepigwa viboko 39 kama adhabu ya kosa lao."
Alisema Nuh aliagiza dola 4,900 kurudishwa kwa mfamasia huyo, ambaye ni muungaji mkono al-Shabaab .
"Uamuzi huu wa aibu na wa kuchekesha ambao kwa hakika ulinishangaza na niliuchukulia kama uliokusudiwa kudanganya na kupotosha watu na kuhimiza wanachama wa kikundi hiki kupora mali binafsi na mali za familia," Abdirahman aliiambia Sabahi.
Huu ni mfano tu wa hivi karibuni wa jinsi adhabu za al-Shabaab zisivyo na msingi maalumu na za kinafiki, kwa kuwa wapiganaji walikutwa na hatia ya makosa hawapaswi kuumia na adhabu zilizoagizwa, alisema, akiongeza kwamba wapiganaji pia wameanzisha ulipizaji kisasi dhidi ya raia wa Somalia, ikiwa ni pamoja na utekaji nyara au kuwakata vichwa ndugu wa viongozi kutoka Gedo na Hiran.
Abdirahman aliviomba vikosi vya serikali ya Somalia kukomesha vitendo vya kutisha vya al-Shabaab vya kuteka nyara, kuua, kutesa na kupiga.

Kukiuka sheria ya sharia

Huko Hiran, al-Shabaab imekuwa ikitoa amri ambazo hazina uhusiano na sharia hivyo wanachama wake wanaweza kuepukana na ujambazi na uasherati, alisema mkuu wa poilisi wa Hiran kanali Isaaq Ali Abdullahi.
Majaji wa Al-Shabaab hawaelewi kikamilifu falsafa ya sheria ya kiislamu na kanuni za msingi za mfumo wa sheria wa haki na usiopendelea, alisema. Uamuzi wao sio halali kwa sababu unachochewa kisiasa, una kisasi na kuzingatia mfumo wa sheria wa kula njama, alisema.
Abdullahi aliishutumu al-Shabaab kwa kumkata kichwa mzee mwanaume na kijana wa kiume tarehe 22 Mei huko Dudumo Qaris, kilometa 45 kaskazini magharibi mwa Beledweyne. Wapiganaji pia waliiba dazeni za ngamia kutoka vijijini, alisema.
"Muda umefika kuwasaka hao wasaliti kutoka al-Shabaab, ambao wanahusiana na al-Qaeda, na kuwaondoa kutoka katika miji mbalimbali na vijiji katika mkoa ili kukomesha uonevu, ukandamizaji, ubaguzi na kudharau [raia]," Abdullahi aliiambia Sabahi.
"Tumefikia katika hali ambapo tunahitaji kutambua matamanio yetu, kwa sababu hivi karibuni utambuzi wa uhuru utakuwa kwetu, ambao watu wetu wanastahili kwa sababu ya kujitoa kwa kiasi kikubwa," alisema.
Ahmed Abdullahi Osman Inji, aliyekuwa kaimu mkuu wa usalama wa Hiran, alisema waathirika wawili walikuwa mjomba wake mwenye miaka 90, Hussein Aadan Toore, na mtoto wa kiume wa Toore. Wauaji waliwakata vichwa kwa kutumia jambia kali na kuwaacha kuvuja damu hadi kifo.
Muda wowote utakaochukua, al-Shabaab siku moja watapigwa na viongozi wao watatakiwa kwenda mbele ya mahakama ya kijeshi kujibu makosa ya gizani, alisema Inji.
"Ulipuaji wa mabomu na ukataji vichwa hauwezi kuendelea," alisema Inji. "Vikosi vya serikali vinachelewa kutekeleza operesheni zao za kijeshi kuzuia njia [za al-Shabaab] zisizo na heshima zinazosababisha maumivu na ugumu kuhusu watu wa Somalia, ambao walilazimishwa kumeza machungu ya mateso na kunyimwa maisha ya kisasa."

Majaaliwa ya Wasomali 6 waliotekwa nyara bado hayajulikani

Mahali walipo wananchi hao sita bado haijulikani kwa karibia wiki mbili baada ya wapiganaji washukiwa wa al-Shabaab waliwatorosha kutoka katika Gedo tarehe 23 Mei.
Utekaji nyara ulifanyika kilometa 40 kati ya El Waq na Bu Sar, alisema mkuu wa wilaya wa El Waq Sahal Malim Ali. Mamlaka baadaye zilirejesha mabaki ya gari na pikipiki iliyoungua, ambayo wanamgambo watuhumiwa walitumia katika operesheni hiyo kabla ya kuungua na kuwaacha, alisema.
Ali alisema utawala wake bado unawasaka watekaji nyara.
Al-Shabaab hawajadaiwa kuhusika na utekaji nyara huo, lakini Ali alisema njia ya mashambulizi imekuwa ni mbinu ya hivi karibuni ya al-Shabaab, ambayo inatumia utoroshaji, ukataji vichwa, na utekaji nyara wa wananchi na mali binafsi kukabiliana na woga wa wakaazi wa maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa serikali ya Somalia.
Kuyumba kutokana na kushindwa kwa jeshi, al-Shabaab inajaribu kugawanya umaarufu kwa kuanzisha mapigano na machafuko ya kikabila dhidi ya serikali, alisema, akiongeza kwamba watu wa Somalia hawatakubali kutishiwa.
Hakuna sheria za sharia wala sheria za kimataifa zinazoruhusu utekaji nyara, alisema Ali. Katika migogoro, sheria za ushirikishwaji wa muda wa vita zitatumika kukamata maadui, lakini kuwashikilia raia kama mateka ni kinyume cha sheria na ni mbinu zisizokubalika kwa kushurutisha, alisema.