Monday, April 22, 2013

Waziri wa sheria ajiuzulu Misri

 22 Aprili, 2013 - Saa 12:57 GMT

Wananchi wa Misri wamekuwa wakifanya maandamano kutaka mageuzi ya kisheria
Waziri wa sheria wa Misri, amejiuzulu kufuatia kilio cha wafuasi wa kiisilamu kwa rais Mohammed Morsi kutaka idara ya sheria kufanyiwa mageuzi makubwa
Ahmed Mekky alionekana kama mwenye kuunga mkono uhuru wa idara ya mahakama wakati wa utawala wa zamani wa Hosni Mubarak.
Alitishia kuondoka serikalini mwaka jana baada ya rais kujilimbikizia mamlaka makubwa zaidi.
Maelfu ya wafuasi wa Morsi, waliandamana siku ya Ijumaa wakitaka wale waliokuwa katika utawala wa Mubarak kuondolewa katika nyadhifa za kisheria.
Maandamano yalikumbwa na ghasia wakati waandamanaji walipokabiliana na polisi

Mswaada tatanishi.

Katika barua yake ya kujiuzulu, bwana Mekky, alisema kuwa mikutano ya hadhara iliyofanywa mapema wiki hii ndiyo iliyochangia uamuzi wake.
Rais Morsi kwa sasa bado hajatamka lolote kuhusu tangazo hilo.
Aidha Rais Mohammed Morsi, amekabiliwa na matatizo chungu nzima, tangu kuingia mamlakani mwezi Juni mwaka 2012
Bwana Mekky, pia alielezea wasiwasi kuhusu juhudi zake kupitisha mswaada mpya ambao wakosoaji wanasena unaweza kupatia chama tawala cha muslim brotherhood udhubiti zaidi wa idara ya mahakama.
Mswaada huo unataka umri wa majaji kustaafu kupunguzwa , hatua ambayo itaamanisha kustaafishwa kwa lazima kwa majaji elfu tatu.
Hatua ya kujiuzulu kwa jaji huyo inakuja siku moja baada ya rais Morsi kutangaza mipango ya kufanyia mageuzi baraza la mawaziri.
Pamoja na mgogoro kutokoka katika idara ya mahakama, maandamano ya mageuzi yamekuwa yakifanyika kama vile yale ya kumpinga rais Morsi wakati wa kuadhimisha miaka miwili ya utawala wake tangu kung'olewa kwa Mubarak.


Wasingizia umaskini kuwatumikisha watoto

 22 Aprili, 2013 - Saa 15:07 GMT

Katika nchi nyingi duniani wazazi hutumikisha watoto
Mkutano wa kimataifa kuhusu utumikishwaji wa watoto wa Kampala umetoa mapendekezo kadhaa mkiwemo kupinga dhana eti umaskini ndio sababu kuu ya utumikishwaji huo na pia kupinga dhana nyingine kuwa ndio kigingi muhimu cha kuweka elimu ya msingi kwa kila mtoto.
Mapendekezo hayo yalitolewa mwishoni mwa mkutano huo, mwishoni mwa juma.
Wajumbe kutoka mataifa 26 wametoa tamko la kuyaomba mataifa yote ambayo yalitia sahihi ya hali ya watoto ya Umoja wa Mataifa, kutekeleza wajibu wa kutoa elimu ya bure na ya lazima kwa watoto.
Aidha tamko hilo linazitaka nchi za kiafrika ambazo ziko chini ya kivuli cha Muungano wa Afrika kuchukua wadhifa kama unavyoambatanishwa katika mkataba wa Afrika kuhusu haki na maslahi ya watoto.
Miongoni mwa sababu nyingi za kuwatumikisha watoto ni umaskani wa kipato,lakini mmoja wa washiriki Christopher Luyenga kutoka Tanzania,akishughulikia sekta ya uzalishaji wa tumbaku analipinga hilo akitoa ufafanuzi kutokana na mkutano huo.
Yeye muwakilishi wa mashirika yanayohusika na watoto nchini Kenya na alietoa muhtasari wa yaliyojadiliwa katika mkutano huo, Timothy Ekesa, anasema kuwa mkutano wa Kampala ulikuwa wenye umuhimu mkubwa kwa maslahi ya watoto.
Moja wa kizungumkuti kwa jamii ni hali ya watoto kubaki mayatima na kuwabidi watoto hao kujitegemea.
Kutokana na mkutano huo imebaishiwa kuwa takriban watoto million 215 duniani baado wanatumikishwa na idadi hiyo inaweza kuwa imeongezeka katika kipindi cha miaka michache iliopita kutokana na migogoro sio tu ya kijamii lakini pia ya kiuchumi.
Barani Afrika chini ya jangwa la sahara inakisikiwa watoto wanaotumikishwa wanafikia million 65.Wajumbe wa mkutano wa kampala wamesema kuwa ni haki ya mtoto kupewa elimu na pia kusisitiza kuwa ajira ya mtoto pia ni elimu.


Wa Maasai watetea ardhi yao Tanzania

 22 Aprili, 2013 - Saa 08:57 GMT

Katika kijiji kimoja Kaskazini mwa Tanzania, ndege aina ya Boeing 747 zinatua kwenye kiwanja binafsi, magari yenye nambari za usajili za milki za kiarabu, zikiendeshwa katika eneo hilo na yeyote mwenye simu ya mkononi anapotua hapo hupokea ujumbe ambao haukutarajiwa
''Hujambo mgeni na karibu UAE.''
Kwa karne nyingi, (Savanna) katika eneo la Arusha lilikuwa makao kwa watu wa jamii ya wamaasai lakini siku hizi mtu sasa anaweza kudhania yuko Dubai moja ya nchi za milki za kiarabu.
Hii ni kwa sababu sehemu kubwa ya ardhi mjini Arusha hasa katika eneo la Loliondo karibu na mbuga ya kitaifa ya wanyama ya Serengeti imekodishwa kwa kampuni ya uwindaji ya Emirati iitwayo Ortello
Tangu mwaka 1992, kampuni hiyo imekuwa ikiwapeleka kwa ndege watalii matajiri zaidi kuwinda simba na wanyama wengine hali iliyowaghadhabisha wenyeji wa eneo hilo ambao ni wamaasai ambao wamezuiwa kuwalisha mifugo wao katika maeneo ya kuwinda.
Sasa serikali ya Tanzania inataka kutoa ardhi zaidi kwa wawindaji hao kwa lengo la kujenga barabara ya umbali wa kilomita 1,500 ambako wanyamapori watakuwa wakipita kwa manufaa ya kampuni hiyo ya uwandaji.
Mpango huo utawaathiri takriban watu 30,000 watakaoachwa bila makao na pia kuwaathiri maelfu ya wengine, ambao huwalisha mifugo wao katika maeneo hayo wakati wa msimu wa kiangazi.
Wamaasai wameghadhabishwa mno na hata kufanya maandamano, wakisema kuwa maisha yao yataathirika pakubwa.
Zaidi ya asilimia ya 90 ya wakaazi wa Loliondo ni wa Maasai ambao hutegemea kuwalisha mifugo wao nyasi kutoka eneo ambalo serikali inanuia kuwakodishia waarabu.
"bila Ardhi hatuwezi kuishi,'' anasema mama Naishirita Tenemeri, mwenye watoto watatu.
Bi Tenemeri anafuga Ng'ombe na Mbuzi eneo la Loliondo, ili kuwanunulia chakula na kuwalipia karo ya shule wanawe.

Wa Maasai wana historia ya kupoteza ardhi yao nchini Tanzania tangu wazungu walipowahamisha kutoka mbuga ya Serengeti mwaka 1959.

Mapema mwezi huu, Bi Tenemeri, akiwa amejifunga shuka yake nyekundu, alijiunga na watu 1,000 wengi wao wakiwa wanawake chini ya miti ya mivule, katika kijiji cha Olorien kupinga mipango ya serikali kuuza ardhi yao.
Wengine walitembea kwa siku nyingi kuonyesha ghadhabu yao kwa kujiondoa katika chama tawala cha CCM kama wanachama.
"ikiwa sina ardhi, sina mahala pa kujifungulia watoto wangu,'' alisema Bi Morkelekei Gume,akitupa kadi yake ya uwanachama wa CCM chini .
"mwanangu yuko katika shule ya upili, kwa sababu ya nyasi zinazotoka hapa.''
''Ikiwa wanataka ardhi yangu wanaweza kuniua.''
Mwanamke mmasaai anashikia bango linalosema "tutapigania ardhi yetu hadi mwisho wake.'' Wanawake hapa ndio wamekuwa wakisikika zaidi katika maandamano yao.
Wanawake wamekuwa wakisikika zaidi, wameathirika zaidi kutokana na hatua ya serikali kuwafukuza, wakiachwa bila kazi kuwalea watoto wao kwa hali ngumu wakati wanaume wakienda katika sehemu za miji ambako wanapata kazi kama walinzi.
Pia wameongoza maandamano tangu viongozi wao wa kisiasa waliopinga mpango wa ujenzi wa barabara waliokuwa wamesema wataondoka katika chama tawala kukosa kutimiza ahadi zao.
Eneo la Loliondo lina wanyama wengi wa porini na hivyo kuvutia watalii ingawa sio wengi. Linapakana na mbuga ya wanyama ya Maasai Mara iliyoko Kenya pamoja na hifadhi ya wanyama ya Ngorongoro.
Waziri wa utalii Khamis Kagasheki anatetea hatua ya serikali kutaka kuwaondoa wamasaai katika eneo hilo akisema kuwa mradi huo utasaidia katika kuendeleza uhifadhi kwani Maasai wametumia ardhi hiyo vibaya.

Lakini wasomi wanasema kuwa jamii ya wamaasai kawaida hawaathiri wanyamapori.

"nina swali moja kubwa kwa wanaosema kuwa wamaasai ni tisho kubwa kwa wanyamapori kuliko kampuni hiyo ya kiarabu ya OBC," alisema Benjamin Gardner wa chuo kikuu cha Washington na ambaye amesomea maswala ya ardhi miongoni mwa wamaasai kwa miongo miwili.
Wamaasai hutegemea sana mifugo wao kwa chakula
Ni nadra kwa wamaasai kuwinda wanyama na hutumia ardhi kuzuia baadhi ya wanyama kujifungulia huko kwani ni tisho kwa mifugo wao.
Mashirika 13 ya kijamii kutoka kote nchini Tanzania, yamesema kuwa wamaasai, wana vibali vichache sana vya kumiliki ardhi, na kuwa serikali inawapotosha watu
Viongozi wa jamii hiyo wanapanga kwenda mahakamani kuishtaki serikali, lakini wanahofia kuwa huenda swala hilo likakosa kutatuliwa haraka kwani kuna kesi moja iliyowasilishwa mwaka 2009 na haijapata ufumbuzi hadi wa leo.

New U.S. rocket blasts off from Virginia launch pad


The Orbital Sciences Corporation Antares rocket is seen as it launches from Pad-0A of the Mid-Atlantic Regional Spaceport (MARS) at the NASA Wallops Flight Facility in Virginia, April 21, 2013. REUTERS/Bill Ingalls/NASA 
By Irene Klotz
(Reuters) - A privately owned rocket built in partnership with NASA to haul cargo to the International Space Station blasted off on Sunday for a debut test flight from a new commercial spaceport in Virginia.
The 13-story Antares rocket, developed and flown by Orbital Sciences Corp, lifted off at 5 p.m. EDT from a Virginia-owned and operated launch pad at NASA's Wallops Flight Facility on Wallops Island, Virginia.
"Beautiful view," said NASA launch commentator Kyle Herring as live video from the rocket, broadcast on NASA TV, showed the booster riding atop a bright plume of fire above the Atlantic Ocean.
Ten minutes later, the rocket deposited its payload - a 8,380-pound (3,800-kg) dummy capsule - into an orbit 158 miles above the planet, fulfilling the primary goal of the test flight.
Orbital Sciences and privately owned Space Exploration Technologies, or SpaceX, hold NASA contracts worth a combined $3.5 billion to fly cargo to the space station, a $100 billion research outpost that flies about 250 miles above Earth.
On its next flight, scheduled for late June or early July, another Antares rocket will carry a Cygnus cargo ship on a demonstration mission to the station.
California-based SpaceX completed three test flights and last year began delivering cargo to the station under its $1.6 billion contract.
The debut of Orbital Sciences' Antares rocket was delayed by the construction of its launch pad at the Mid-Atlantic Regional Spaceport, located on the southern end of NASA's Wallops Island facility. NASA has flown thousands of smaller suborbital rockets, high-altitude balloons and research aircraft from Wallops over the past 68 years.
Standing 130 feet tall and packing 740,000 pounds of thrust at liftoff, Antares is the largest rocket to fly from Wallops Island. In addition to station cargo runs, Orbital Sciences has a separate contract to launch a NASA moon probe aboard a Minotaur 5 rocket from Wallops in August.
(Reporting by Irene Klotz in Cape Canaveral, Florida; Editing by Eric Beech)

Mapigano Nigeria 185 wafariki dunia

 22 Aprili, 2013 - Saa 22:39 GMT

Wapiganaji wa kundi wa Kiislamu la Boko Haramu

Mapigano ya wapiganaji wa kiislamu na vikosi vya usalama nchini Nigeria yameripotiwa kutokea tangu usiku wa Ijumaa na kuendelea kwa muda mrefu ambapo jumla ya watu 185 wanaripotiwa kufariki dunia katika mapigano hayo yaliyotokea Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Serikali ya mji wa Baga na Ofisa Serikali hiyo Bwana Lawan Kole.
Inasemekana kuwa watu wengi zaidi wamefariki dunia ambapo bado juhudi za kutafuta maiti nyingine zinaendelea. Brigedia Jenarali Austin Edokpaye amewaambia maafisa wakuu wa serikali kuwa,wapiganaji walitumia silaha kali na maroketi yenye mabomu mazito kupambana na vikosi vya jeshi.
Aidha bwana Edokpaye aliongeza kuwa,wapiganaji hao walikuwa wakitumia raia kama kinga yao kwa kujibanza karibu na makazi ya watu ambapo walijua vikosi vya jeshi visingeweza kujibu mapigo.
Nigeria imekuwa ikikabiliwa na vifo vya raia wengi tangu kuibuka kwa vikundi vya wapiganaji wa kiislamu mwaka 2010 ambapo vingi vimejikita Kaskazini mwa nchi hiyo.

Kesi yaandaliwa dhidi ya mshukiwa Boston


 22 Aprili, 2013 - Saa 09:34 GMT

Maombolezi kwa waathiriwa wa mashambulizi ya Boston
Vyombo vya habari nchini Marekani vinasema kuwa mshukiwa wa mashambulizi ya Boston Marathon, Dzhokhar Tsarnaev, ambaye yuko hospitalini katika hali mbaya, amekuwa akijibu maswali ya majasusi kwa kuandika.
Hata hivyo hilo bado halijathibitishwa, lakini ripoti zinasema kuwa maswali hayo yanahusiana na mabomu mengine pamoja na wale alioshirikiana nao.
Ripoti za awali zilionya kuwa Dzhokhar Tsarnaev, ambaye ana majeraha ya risasi kwenye shingo lake, huenda asitoe ushahidi kwa kuongea na majasusi hao.
Wakati huohuo, viongozi wa mashtaka wanaanda kesi dhidi ya mshukiwa wa pili wa mashambulizi ya Boston Marathon Dzhokhar Tsarnaev huku maelezo zaidi kuhusu kukamatwa kwake yakijitokeza.
Ikiwa atashtakiwa kwa kutumia silaha za maangamizi kwa lengo la kuwaua watu, huenda akakabiliwa na hukumu ya kifo.
Tsarnaev yuko hospitalini akiwa hawezi kuongea kwa sababu ya jeraha katika shingo lake.

Serikali imesema kuwa majasusi hao watamhoji mshukiwa bila ya kumweleza haki zake ambazo zinamruhusu akae kimya hadi atakaposhauriana na wakili wake. Hata hivyo majasusi walikanusha ripoti kuwa walimhoji.

Awali meya wa Boston, Tom Menino, alisema kuwa hawana uhakika ikiwa wataweza kumhoji mshukiwa
"Tuna maswali mengi na yote yanahitaji kujibiwa," alisema gavana wa Massachusetts Deval Patrick,akinukuliwa na shirika la habari la Reuters.
Mshukiwa alikamatwa jioni Ijumaa baada ya msako mkali dhidi yake wakati ambapo nduguye mkubwa na mshukiwa mwingine waliuawa.
Polisi wanaamini kuwa Dzhokhar huenda alimuua nduguye mwenyewe kwa kumgonga na gari alipokuwa anatoroka polisi Alhamisi usiku.
Shambulizi hilo lilisababisha vifo vya kijana mmoja mwenye umri wa miaka minane na wanawake wawili na kisha kuwajeruhi wengine wengi ikikisiwa kuwa walikuwa zaidi ya 180.

Officials identify firefighters killed in deadly Texas blast

Texas Department of Public Safety Sergeant Jason Reyes walks past the site of a housing complex which was destroyed by a deadly fertilizer plant explosion in the town of West, near Waco, Texas April 21, 2013. REUTERS/Michael Ainsworth/Pool
Reuters/Reuters - Texas Department of Public Safety Sergeant Jason Reyes walks past the site of a housing complex which was destroyed by a deadly fertilizer plant explosion in the town of West, near Waco, Texas April 21, 2013. REUTERS/Michael Ainsworth/Pool

By Tim Gaynor and Colleen Jenkins
WEST, Texas (Reuters) - Texas officials released the names of four volunteer firefighters on Sunday killed in a deadly blast in this close-knit Texas town, as authorities identified the center but not the cause of last week's deadly fertilizer plant blast.
Among the dead named at a news conference outside city hall in West, Texas, were brothers Doug and Robert Snokhous, remembered by their family as "lifelong best friends" who lived half a mile from each other and worked together at an ironworks in nearby Waco.
"Doug and Robert could always be seen together, whether they were hunting, working on cars, golfing or cooking barbecue at the volunteer fire departments cook-off," their family said in a statement read to reporters.
"They were always together and we were always comforted that they were together at the end."