Wednesday, May 22, 2013

NYUMBA YA MWANDISHI WA HABARI WA TBC YACHOMWA MOTO HUKU MABOMU YAKIRINDIMA HUKO MTWARA


Hali imezidi kuwa mbaya katika Mji wa Mtwara na hivi punde watu wanaendelea kufanya uharibifu katika maeneo mbalimbali ya mji huo.

Jengo moja ambalo linadaiwa kumilikuwa na CCM limechomwa moto katika eneo la Majengo na daraja linalounganisha Lindi na Mtwara limevunjwa.


Mbali na hayo pia nyumba ya mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC)imechomwa moto.

Katika Mji wa Mtwara milio ya mabomu na risasi ndio inayosikika kila kona. Jeshi la Polisi linajaribu kuwadhibiti vijana  na watu wengine ambao wanafanya vurugu hizo.

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DODOMA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUGONGWA NA TRENI



Mwanafunzi  wa chuo kikuu cha Dodoma  anayejulikana  kwa jina  la Boid Mwakitalima  amefariki dunia  baada  kugongwa na treni....Mwanafunzi huyo  alikuwa  mwaka  wa  tatu.

Taarifa zinaeleza  kuwa, mwanafunzi  huyo  alikuwa   anatembea pembezoni  mwa  reli huku  akiwa ameweka  "headphone"  sikioni, hali  iliyomfanya  ashindwe  kusikia ama  kuhisi  chochote  juu  ya  muungurumo  wa  treni  hilo  mpaka  lilipomsogelea  karibu  na  kumsukuma  pembeni  ambapo  aliangukia  chuma  na  kuaga  dunia  pale  pale...
 Makamu Mkuu wa Chuo kikuu  cha Dodoma Prof.Idrisa Kikula  akiwasili Collage ya Informatics

 Mbele  ni Mshauri wa wanafunzi ( dean of student) chuo kikuu cha dodoma, Nyuma ni mshauri wa wanafunzi, Pro.Anatory  ( dean of students)  collage ya informatics na Katikati ni Makamu mkuu wa chuo cha Dodoma...
------ Baada  ya  ajali  hiyo, mwanafunzi  huyo  alipelekwa  chumba  cha kuhifadhia  maiti  katika  hospitali  ya  Mkoa  wa Domoma, "General hospital" ambapo  leo  hii  ameagwa  na wanafunzi wenzake  wa  chuo  kikuu  cha Dodoma  na  kusafirishwa  kwenda  nyumbani  kwao Mbeya kwa  mazishi..
 Wanafunzi wakiuaga  mwili  wa  marehemu  kwa  huzuni
 Mkuu wa  collage ya Informatics, Prof. Mvuma,  akitoa  
nasaha  zake
 Rais  wa wanafunzi, collage ya informatics  akitoa  nasaha  zake

VURUGU ZA MTWARA ZASABABISHA BUNGE LIAHIRISHWE

Hivi ndivyo kunavyoendelea hadi sasa Mkoani Mtwara
Spika wa bunge , Anne Makinda ameahirisha Bunge kutokana na hali ya Mtwara na ameiagiza serikali kuwa kesho wawasilishe taarifa bungeni kuhusiana na hali hiyo.

Makinda ameitisha kamati ya uongozi ili kuona kama wanaweza kutuma kamati ya Bunge kesho kwenda huko.

MKENYA ANAYELIA BAADA YA OBAMA KUPANGA KUJA TANZANIA NA KUIKACHA KENYA



Rais wa Marekani Barack Obama na mkewe Michelle mwezi ujao atakuwa na ziara katika nchi tatu za Afrika zikiwemo Tanzania, Afrika Kusini na Senegal.
Ziara hiyo itaanza June 26 – July 3. Hata hivyo kitendo cha Obama kuiruka Kenya nchi anayotokea baba yake mzazi, kimewaumiza wakenya wengi hasa ukizingatia kuwa hajawahi kuitembelea nchi hiyo tangu aingie madarakani.

HII TENA IMEKUWA NI ZAIDI YA MAELEZO JAMANI, KAKA NA DADA WANASWA WAKIVUNJA AMRI YA SITA KATIKA MAPANGO YA UFUKWE WA COCO



Baada ya kuona kuwa wamevamiwa na askari, kaka mtu alichomoka na kutafuta silaha ili kuweza kujihami na wavamizi wake bila ya kujua kama ni askari.
 



UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni. Usemi huu unakamilishwa na tukio la kunaswa kwa vijana wawili wenye undugu wa damu wakifanya mapenzi   kando ya Ufukwe wa Bahari ya Hindi

Imefahamika kwamba vijana  hao, kaka na dada   wamenaswa ‘wakingonoka  katika mapango yaliyopo kando ya Ufukwe wa Coco, Oysterbay jijini Dar es Salaam.


Tukio zima lilitokea mchana kweupe wa saa 9 na kudhihirisha habari za mara kwa mara zinazoeleza kwamba Ufukwe wa Coco umekuwa ukitumika kwa ufuska usiku na mchana.

Risasi  lilinasa tukio hilo kwa kutumia mitambo maaalum iliyoelekezwa kando ya bahari.
 
Wawili hao walinaswa tangu walipokuwa wakiingia katika ufukwe huo na kuwafuatilia nyendo zao, hatua kwa hatua.



Haikufahamika mara moja kama wawili hao walikuwa na makubaliano ya kwenda kuduu katika ufukwe huo au la, lakini kwa mbali ilionekana kama vile dada mtu alikuwa akizingua kwenda kutenda dhambi hiyo.
 
Picha za video zilizonaswa, zinamuonesha dada huyo akionekana kutoa upinzani pale alipokuwa akishikwashikwa na kaka yake.

Alionekana kama vile hakuwa tayari kwa mchezo huo.
Hata hivyo, kaka mtu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23-26 alikuwa akilazimisha kitu fulani ambacho kilionekana dhahiri kupitia kamera zetu.

Ni kama vile hawakuwa na makubaliano na kile walichokuwa wakienda kukifanya.
 
Mara kadhaa dada huyo alionekana kumkwepa kaka yake na alikuwa akijiondoa karibu yake pale alipomlazimisha kutaka kumfanyia kitu kisichokuwa cha kawaida.



Kamera za Risasi ziliwafuatilia wawili hao kwa kuwa walionekana kuwa na kitu ‘spesho’.

 Mpaka wanazama katika mapango yaliyopo kando ya ufukwe huo wa Coco, kamera zilikuwa zikiendelea kuwachukua hadi walipozama ndani kabisa ya mapango hayo. 
 

Walipozama ndani ya mapango hayo, ghafla walitokea askari ambao nao walikuwa wakifuatilia nyendo za wawili hao.
 

Askari hao wa Kituo cha Oysterbay, wakiongozwa na kamanda wa oparesheni maalumu katika Wilaya ya Kinondoni, Kamanda Swai walifuatilia kwa umakini tukio hilo.
 

Wakiwa chini ya mapango, kaka na dada waliondoa vinguo vilivyokuwa maungoni mwao na kuanza kuduu kama vile walikuwa katika ufukwe unaoruhusiwa kufanya vitendo hivyo.
 
Kabla askari hawajawavamia, waliwashuhudia wawili hao wakiwa katika kilele cha sterehe yao huku dada mtu akionesha kutoa ushirikiano kwa shingo upande.


Ghafla, askari waliwavamia na kuwatibulia starehe yao kisha kuwatia mbaroni.

Katika hilo nusura zipigwe kati ya askari na kaka huyo ambaye alikuwa akitaka kupigana na watu asiowajua kwa kuwa walikuwa wametinga mavazi ya kiraia.
 

Hata hivyo, alitulizwa na kutakiwa kuvaa pensi yake ili aweze kutoa maelezo kwa kina. 
 

Wakati yote yakiendelea, dada mtu alikuwa amepigwa na butwaa na kutojua cha kufanya hadi aliporushiwa kitenge chake kilichokuwa pembeni ili ajisitiri mwili wake.

Katika mahojiano ya awali yaliyoongozwa na Kamanda Swai, ilibainika kwamba wawili hao ni ndugu wa damu yaani kaka na dada. 

Maelezo hayo yanasema kuwa dada mtu alitoka mkoani na alikuja kutembea jijini Dar es Salaam, ndipo kaka yake alipomtaka watoke kwenda kumuonesha vivutio vya jiji hilo.

“Nina miaka 19, nimetokea Iringa kuja Dar kutembelea familia lakini kaka akanileta huku na kunifanyia vile, siyo kama tulikuwa tumekubaliana,” alisema dada huyo kwa aibu.

Kaka mtu alikiri kile kilichosemwa na dada yake na kushindwa kujitetea kwa kuwa kila kitu kilikuwa hadharani.


Wawili hao walichukuliwa na kupelekwa katika Kituo cha Oysterbay kwa ajili ya kufunguliwa kesi ya uzembe na uzururaji na kusekwa rumande kabla ya kufikishwa mahakamani.