Monday, June 3, 2013

Ajali ya ukuta wa tangi la maji yauwa watatu Pemba



Askari wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiwa katika zoezi la kuondoa miili ya Marehemu waliopoteza maisha katika ajali ya kuangukiwa na ukuta wa tangi la maji Machomanne Chake Chake Pemba
Askari wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiwa katika zoezi la kuondoa miili ya Marehemu waliopoteza maisha katika ajali ya kuangukiwa na ukuta wa tangi la maji Machomanne Chake Chake Pemba
Tangi la maji lilipo Machomane Chake Chake Pemba ambalo lilikuwa kwenye harakati za kuangushwa na kujengwa upya, limeanguka na kuelemea mafundi waliokuwa juu ya tangi hilo ambapo hadi jana watu watatu wameripotiwa wamefariki dunia na tisa kujeruhiwa.
Miongoni mwa waliofariki wametambuliwa kuwa ni Salumu Muhidini (35) Juma Rashid mkazi wa Chanjani, na mmoja aliyejulikana kwa jina la maarufu la Golo (35).
Kwa mujibu wa taarifa za watu wakaribu wanasema ajali hiyo imetokea kutokana na vifaa duni visyivokuwa na uwezo wa kufanyia kazi hiyo ambayvo walikuwa wakivitumia mafundi hao.
Wananchi mbali mbali wakiwa katika hospitali ya Chake Chake  Pemba, wakitizama miili ya ndugu zao waliopoteza maisha na majeruhi baada ya kuangukiwa na mnara wa tangi la maji Machomanne Pemba
Wananchi mbali mbali wakiwa katika hospitali ya Chake Chake Pemba, wakitizama miili ya ndugu zao waliopoteza maisha na majeruhi baada ya kuangukiwa na mnara wa tangi la maji Machomanne Pemba
Wananchi mbali mbali wakiuangalia mnara wa Tangi la maji Machomanne, ulioanguka na kupoteza maisha ya wananchi watatu jana asubuhi huko Machomnne, Chake Chake Pemba
Wananchi mbali mbali wakiuangalia mnara wa Tangi la maji Machomanne, ulioanguka na kupoteza maisha ya wananchi watatu jana asubuhi huko Machomnne, Chake Chake Pemba

Daktari Bingwa kutoka Quba anayefanya kazi zake kisiwani Pemba, (jina halikufahamika) akimtibu mmoja kati ya majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Chake Chake, kufuatia ajali ya kuangukiwa na ukuta wa mnara wa tangi la maji Mchomanne Pemba
Daktari Bingwa kutoka Quba anayefanya kazi zake kisiwani Pemba, (jina halikufahamika) akimtibu mmoja kati ya majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Chake Chake, kufuatia ajali ya kuangukiwa na ukuta wa mnara wa tangi la maji Mchomanne Pemba
Picha zote kwa hisani ya Voice of Zanzibar(VoZ) na Abdi Suleiman wa Pemba

No comments:

Post a Comment