Tuesday, May 14, 2013

MTUHUMIWA NAMBA MOJA WA BOMU LA ARUSHA AMEFIKISHWA MAHAKAMANI LEO NA KUSOMEWA MASHITAKA 21


Mtuhumiwa mmoja kati ya tisa waliotiwa mbaroni na jeshi la polisi baada ya kutokea mlipuko wa bomu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi amefikishwa mahakamani na kusomewa mashtaka 21 ya mauaji na kujaribu kuua.

Victor Ambrose Calist (20) ambaye ni dereva wa bodaboda na mkazi wa eneo la Kwa Mromboo jijini Arushai amesomewa mashtaka yake mbele ya Hakimu mkazi, Devotha Kamuzora.

Mtuhumiwa huyo anakabiliwa na mashtaka matatu ya mauaji ya watu watatu waliofariki dunia katika tukio ambalo lililotokea Mei 5, mwaka huu.

Mawakili wa serikali, Haruna Matagane na Zachariah Elisaria wanadai Calist pia anatuhumiwa kwa makosa 18 ya kujaribu kuua. Hata hivyo makosa mengine bado hayajatajwa..




Pia polisi imewaachia huru raia wanne wa kigeni waliokuwa wakishikiliwa kwa tuhuma za kuhusika katika tukio hilo baada ya uchunguzi uliofanywa na jeshi hilo kwa kushirikiana na FBI na polisi wa kimataifa (Interpol), kubaini hawakuhusika kurusha bomu katika kanisa hilo.

Wabunge wa Kenya walinganishwa na 'Nguruwe'

 
Nguruwe Waliofananishwa na Wabunge wa Kenya




Polisi nchini Kenya wamekabiliana na waandamanaji waliozingira majengo ya bunge kulaani jaribio la wabunge kutaka kujiongeza mishahara.
Polisi hao wametumia gesi ya kutoa machozi pamoja na maji kuwatawanya waandamanaji hao ambao wengi wao ni wanachama wa mashirika ya kijamii ambao wamesma katu hawaondoki katika majengo hayo ya bunge hadi wabunge watakapopata ujumbe wao.
Pia inaarifiwa kuwa wanawataka wabunge kutia saini na kuapa kuwa hawatatumia bunge kunyanyasa wananchi maskini kwa kujiongeza mishahara kinyume na sheria.
Mashirika ya kijamii yaliandaa maandamano hayo kuonyesha ghadhabu waliyonayo wakenya dhidi ya wabunge hao wanaotaka kuongezwa miashara, miezi miwili tu baada ya kufanyiika uchaguzi mkuu wa amani.
Aidha waandamanaji hao walipeleka Nguruwe kwenye mlango mkuu wa kuingia katika bunge pamoja na damu kama ishara kuwa wabunge ni watu walafi na wasiojali maslahi ya wakenya kwa kujitakia makubwa.
Maandamano haya yanakuja siku moja baada ya tume ya kitaifa ya mishahara ambayo wajibu wake ni kudhibiti mishahara ya wafanyakazi wa umma kusema kuwa katu haitawaongeza mishahara wabunge.
Tume hiyo ilisema siku ya Jumatatu kuwa haitaogopa vitisho vya wabunge kutaka kuivunjilia mbali tume hiyo ikiwa hawatawaongeza mishahara wabunge kama kikwazo.
Wabunge hao walijaribu kwa kutumia vitisho kuilazimisha tume hiyo kuwoangeza mishahara lakini hawakufua dafu.
Ni baada ya mbunge mmoja kuwasilisha hoja bungeni kuwa ikiwa tume hiyo haitawaongeza mishahara watafanyya kila hali kuivunja.
Hata hivyo tume hiyo ni ya kikatiba.
Wabunge wa Kenya wanataka kulipwa mshahara wa shilingi 850,000 wakati wakihudumu katika bunge la kumi ikipuuza mshahara waliowekewa na tume ya mishahara ambao ni shilingi 532,000. Wanasema pesa hizi ni kidogo sana.

Mgomo wazuka mgodini Afrika Kusini

 14 Mei, 2013 -

Kuna hofu kuwa huenda maandamano kama yaliyoshuhudiwa mwaka jana yakatokea
Kampuni ya uchimbaji madini ya Lonmin, nchini Afrika Kusini inasema kuwa maelfu ya wafanyakazi katika mgodi wake wa wa platinum wamefanya mgomo kinyume cha sheria baada ya afisa wa muungano wao kupigwa risasi katika baa moja mwishioni mwa juma.
Msemaji wa kampuni hiyo Sue Vey amesema kuwa shughuli zote za uzalishaji kwenye kiwanda hicho zimevurugika .
Mgomo huu umezua hofu ya vurugu zaidi kutokea baada ya sekta hiyo kukumbwa na migomo mwaka jana
Mwezi Agosti mwaka jana wafanyakazi thelathini na wanne waliuliwa na polisi katika mgodi wa Marikana na waandishi wa habari wanasema mgomo huo umesababisha hofu ya kutokea kwa ghasia kufuatia hali ya taharuki iliyopo juu ya kukatwa kwa kazi , mashauriano ya riba na uhasama ndani ya muungano wa wafanyakazi.
Lonmin, ambayo hisa zake,ziko katika soko la hisa la London na Johannesburg , ndiyo kampuni ya tatu kwa ukubwa katika kuzalisha madini ya platinum.
Taarifa za mgomo wa leo zimesababisha hisa za kampuni hiyo kushuka kwa asilimia 5% mjini London.
Msemaji wa kampuni hiyo, Sue Vey alisema kuwa migodi yote kumi na mitatu ya kampuni hiyo imefungwa kwa sasa.
"Wafanyakazi wa kampuni hiyo waliwasili kazini ingawa hawakuelekea katika shughuli zao kama ilivyo desturi yao
Huku akisema kuwa kampuni hiyo haielewi kwa nini wafanyakazi wameamua kugoma, msemaji wa chama cha wafanyakazi hao, alisema kuwa huenda mgomo huo unatokana na ghadhabu ya wafanyakazi hao, kuhusu mauaji yaliyotokea mwishoni mwa wiki ya kiongozi mmoja wa chama hasimu cha wafanyakazi.
Polisi walithibitisha kuwa kiongozi huyo aliuawa mwishini mwa wiki katika eneo Rustenburg.

KASHIFA YA NGONO YALITAFUNA BUNGE LETU....WABUNGE WADAIWA KUBEBANA NA KUPEANA MIMBA


SKENDO nzito inalitafuna Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikitawala madai kwamba kuna wabunge wawili wanawake, wamejazwa mimba na waheshimiwa wenzao wanaume.

Awali, ulitawala uvumi kuwa mmoja wa wabunge wa upinzani (viti maalum), akitokea Kanda ya Kaskazini, amepewa ujauzito na mheshimiwa mwingine ambaye ni kiongozi anayeshika nafasi za juu kwenye moja ya vyama vikuu vya upinzani nchini (wote majina yao tunayahifadhi kwa sasa).

Kashfa hiyo ya mtunga sheria huyo kupewa mimba na mheshimiwa mwenzake ambaye ni mume wa mtu, ilipata mbeleko na kuifanya ivume zaidi, baada ya Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde, kulipuka bungeni: “Humuhumu ndani kuna wabunge wanawake wenye mimba zisizotarajiwa.”
Lusinde, alitamka hayo Aprili, mwaka huu, wakati akichangia hotuba ya bajeti, Ofisi ya Waziri Mkuu, kipindi ambacho bunge lilikuwa limechafuka kutokana na wabunge kurushiana ‘mipasho’ wao kwa wao.
 

Kauli ya Lusinde, pamoja na kupokelewa tofauti na wabunge wengi wanawake, wakidai mheshimiwa mwenzao amewadhalilisha, upande mwingine, katika ‘vikao vya kwenye korido’, matukio ya vicheko na kugonga mikono yalitawala na kunena kwa msisitizo “message delivered”, yaani ujumbe umefika.
Wakati mwandishi wetu akifuatilia sakata lenyewe, mbunge mwingine wa Viti Maalum (CCM) ambaye jina lake tunaliweka kabatini, aliamua kufunguka: “Nashangazwa sana na haya madai, tunawasema wapinzani, wakati hata kwetu (CCM) kuna watu wamepeana mimba.”
 
Mbunge huyo alisema kuwa siyo siri mjengoni kuwa mmoja wa watunga sheria wa CCM, anayetokea moja ya majimbo ya Kanda ya Magharibi, amempa ujauzito mheshimiwa mwingine kutoka chama tawala, anayewakilisha viti maalum (majina yao yamehifadhiwa kabatini kwa sasa).
 
Kwa mujibu wa mtoa habari huyo, mbunge anayetajwa kupewa mimba, anatokea kwenye ukoo wa mmoja wa vigogo waliowahi kushika nafasi za juu kabisa kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wabunge mbalimbali waliozungumza na mwandishi wetu, walikiri kutambua uwepo wa wenzao wenye uhusiano wa kimapenzi kiasi cha kufikia kupeana mimba.
 
Mbunge mwingine alithubutu kutamka: “Nini hao kupewa mimba na zinaonekana, wapo ambao wanapata na wanatoa. Yote hayo tunayajua.”

Katika kufanyia kazi kila kinachozungumzwa, mwandishi wetu alizungumza na baadhi ya wabunge ambapo Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, alisema: Unajua madai ya mimba yanawahusu wanawake, kwa hiyo waulizwe wenyewe.
 

“Kama umenitafuta mimi kwa kigezo kwamba ni mbunge kijana, basi waulize wabunge vijana wanawake,” alisema Mnyika.
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, alikiri kufahamu kuwepo kwa tuhuma kwamba wapo wabunge wamepeana mimba lakini hawezi kuwa na uhakika kwa sababu uhusiano wa kimapenzi ni jambo la faragha.
 

“Hayo madai yapo, yanazungumzwa. Wapo wanaotajwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi, hayo ni mambo ya faragha. Sijui pengine walioanzisha haya madai wana vipimo vyao,” alisema Kafulila.
 


Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Morogoro, Sara Msafiri, alisema kuwa haiwezekani wabunge kupata mimba zisizotarajiwa kwa sababu ni watu wazima.
 

“Wabunge tunapata mafunzo ya uzazi, kwa hiyo kama ni mimba basi mtu anakuwa amepanga kuipata. Hakuna  kitu kama hicho. Hata hilo la kutoa mimba halipo kabisa, sijawahi kusikia mtu amefanya hivyo bungeni,” alisema Sara.

Kwa upande wa Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Grace Sindato Kiwelu, alisema: “Sitegemei upande huo wa wabunge kupata mimba zisizotarajiwa, kwani wanaofanya mapenzi ni watu wazima hivyo wanafanya wakijua kwamba wanatarajia kupata nini.”
 

Mbunge mwingine wa Viti Maalum (Chadema), Chiku Abwao, alisema: “Hakuna mbunge anayepata mimba isiyotarajiwa, kwanza nilimshangaa mbunge kutamka mambo kama hayo, alistahili kuwaambia watoto, lengo lake lilikuwa kudhalilisha wanawake.”
 

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Munde Tambwe, alisema: “Ile kauli ya Lusinde kwamba kuna wabunge wanapata mimba zisizotarajiwa, nadhani kuna mtu alikuwa anamlenga, kwa hiyo mimi siwezi kulizungumzia.”

Wapinga mishahara ya wabunge Kenya

 14 Mei, 2013 - Saa 11:09 GMT

Wananchi wa Kenya wanaopinga wabunge kuongezwa mishahara
Polisi nchini Kenya wamekabiliana na waandamanaji waliozingira majengo ya bunge kulaani jaribio la wabunge kutaka kujiongeza mishahara.
Polisi hao wametumia gesi ya kutoa machozi pamoja na maji kuwatawanya waandamanaji hao ambao wengi wao ni wanachama wa mashirika ya kijamii ambao wamesma katu hawaondoki katika majengo hayo ya bunge hadi wabunge watakapopata ujumbe wao.
Pia inaarifiwa kuwa wanawataka wabunge kutia saini na kuapa kuwa hawatatumia bunge kunyanyasa wananchi maskini kwa kujiongeza mishahara kinyume na sheria.
Mashirika ya kijamii yaliandaa maandamano hayo kuonyesha ghadhabu waliyonayo wakenya dhidi ya wabunge hao wanaotaka kuongezwa miashara, miezi miwili tu baada ya kufanyiika uchaguzi mkuu wa amani.
Aidha waandamanaji hao walipeleka Nguruwe kwenye mlango mkuu wa kuingia katika bunge pamoja na damu kama ishara kuwa wabunge ni watu walafi na wasiojali maslahi ya wakenya kwa kujitakia makubwa.
Maandamano haya yanakuja siku moja baada ya tume ya kitaifa ya mishahara ambayo wajibu wake ni kudhibiti mishahara ya wafanyakazi wa umma kusema kuwa katu haitawaongeza mishahara wabunge.
Tume hiyo ilisema siku ya Jumatatu kuwa haitaogopa vitisho vya wabunge kutaka kuivunjilia mbali tume hiyo ikiwa hawatawaongeza mishahara wabunge kama kikwazo.
Wabunge hao walijaribu kwa kutumia vitisho kuilazimisha tume hiyo kuwoangeza mishahara lakini hawakufua dafu.
Ni baada ya mbunge mmoja kuwasilisha hoja bungeni kuwa ikiwa tume hiyo haitawaongeza mishahara watafanyya kila hali kuivunja.
Hata hivyo tume hiyo ni ya kikatiba.
Wabunge wa Kenya wanataka kulipwa mshahara wa shilingi 850,000 wakati wakihudumu katika bunge la kumi ikipuuza mshahara waliowekewa na tume ya mishahara ambao ni shilingi 532,000. Wanasema pesa hizi ni kidogo sana.

Kitendo cha kula Moyo Syria chalaaniwa

 14 Mei, 2013

Hali imeendelea kuwa mbaya zaidi nchini Syria
Kanda ya video ambayo inaonekana kuonyesha muasi mmoja nchini Syria akila Moyo wa mwanajeshi aliyefariki, imelaaniwa vikali.
Shirika la Marekani la kutetea haki za binadamu, Human Rights Watch, limemtaja muasi huyo kama Abu Sakkar, muasi anayejulikana sana kutoka mji wa Homs, na kusema kuwa vitendo vyake ni vya uhalifu wa kivita.
Chama rasmi cha upinzani nchini Syria kimsema kuwa mshukiwa huyo lazima atakabiliwa na kesi mahakamani.
Kanda hiyo ambayo haiwezi kuthibitishwa , imeonyesha akikata moyo wa mwanajeshi huyo na kuula.
"naapa kwa Mungu, tutakula mioyo yenu na figo zenu , nyinyi wanajeshi wa Bashar,'' alisema muasi huyo akimtaja rais Bashar al-Assad wakati akiwa kando ya maiti ya mwanajeshi huyo.
Shirika la Human Rights Watch, linasema kuwa Abu Sakkar ni kiongozi wa kundi linalojulikana kama Omar al-Farouq Brigade.
"ukataji wa miili ya maadui ni uhalifu wa kivita, lakini la kuudhi zaidi ni swala la ghasia na vita kukithiri,'' alisema Peter Bouckaert wa shirika la HRW.
HRW limesema kuwa,wanaofanya uhalifu kutoka pande zote, lazima wajue kuwa watawajibishwa.
Aidha shirika hilo limesema kuwa Abu Sakkar aliwahi kunaswa kwa kanda ya video akirusha makombora katika maeneo yenye madhehebu ya Shia nchini Lebanon na kisha kusimama kando ya maiti ya wanajeshi waliouawa katika mashambulizi ya kuvizia.
Kanda hiyo iliyowekwa kwenye mtandao siku ya Jumapili, ni moja ya video inazoonyesha picha mbaya zaidi kuwahi kuonyeshwa tangu kuanza kwa vita vya Syria miaka miwili iliyopita.
Umoja wa mataifa unasema kuwa watu 70,000, wameuawa tangu kuanza mapinduzi ya kiraia dhidi ya utawala wa Rais Bashar al-Assad Machi 2011, ingawa baadhi ya mashirika yanasema idadi hiyo imefika watu 80,000.

Kenya kufufua askari wa akiba Garissa ili kupambana na al-Shabaab

Serikali ya Kenya inapanga kufufua askari wa akiba wa Kenya (KPR), programu ya kutoa mafunzo na kuwezesha vikosi vya raia, kusaidia kupambana na wanamgambo wa al-Shabaab kutoka ndani ya jamii huko Garissa.
  • Askari wa Kenya akiangalia mkutano wa hadhara wa chama cha Harakati za Demokrasia ya Njano huko Garissa tarehe 22 Februari. Askari polisi wa akiba ambao ni raia wenye silaha hivi karibuni watasaidia kulinda amani katika mji huo, wakilinda dhidi ya vitisho kutoka kwa al-Shabaab. [Will Boase/AFP]
Garissa imekuwa mahali pa mashambulio makubwa ya al-Shabaab nchini Kenya baada ya vikosi vya ulinzi vya Kenya kupeleka vikosi Somalia Oktoba 2011.
Iliongozwa na Inspekta Jenarali David Kimaiyo na Katibu Mkuu wa Usalama wa Ndani Mutea Iringo, Kamati ya Ushauri ya Taifa imekuwa ikichunguza mfululizo wa mashambulio kama hayo mwezi Aprili. Wakati wa mkutano wa tarehe 20 Aprili, kamati ilipendekeza kushirikisha raia katika mji wa Garissa kwa ajili ya operesheni za kigaidi.
KPR iliundwa mwaka 1948 kusaidia polisi kudumisha sheria na kanuni nchini Kenya kote.
Mwaka 2004, aliyekuwa kamishina wa polisi Meja Jenerali Mohammed Hussein Ali alivunja na kunyang'anya silaha KPR katika maeneo ya miji ya Kenya baada ya maofisa wake kuhusishwa na uhalifu wa kutumia nguvu na rushwa. Hata hivyo, aliendeleza jeshi hilo katika maeneo ya vijijini, kupambana na wizi wa ng'ombe na ujambazi.

Kufufua askari wa akiba wa Kenya

Raia katika KPR iliyofufuliwa watasaidia kulinda usalama katika vitongoji vya Garissa, Kamishina wa wilaya ya Garissa Maalim Mohammed aliiambia Sabahi. Watakuwa chini ya maofisa wanaosimamia askari kanzu wasio na sare wenye jukumu la kufichua shughuli za al-Shabaab zisizo na ujuzi kutoka katika maficho yao na kuzuia mashambulio ya kigaidi.
Kutoka vikosi vya raia vilipopewa silaha, Mohammed alisema serikali imekuwa ikichukua hatua kali kuepuka kutoa silaha kwa makosa kwa wahalifu.
"Tunapaswa kupata vitu mara tu tunapoanza ili tusiongeze silaha zaidi katika mzunguko, ambazo zitaongeza matatizo zaidi kwenye vitisho vilivyopo vya al-Shabaab," alisema.
"Kuna hitilafu kwenye kutoa silaha kwa raia, lakini kwa kunyoosha mambo kwa ufanisi na kuhakikisha kwamba silaha hazitolewi kwa wasiostahili, tunachagua watahiniwa kufanyiwa uchunguzi," Mohammed alisema.
Tunawaandikisha askari wale wanaofaulu uchunguzi wa awali ambao watapewa kozi ya mwezi mmoja kuhusu silaha za moto, mafunzo halisi, ukusanyaji wa taarifa kuhusu maadui na kukabili majanga ya msingi, alisema. Serikali kwa sasa inahakiki watahiniwa 100 kwa ajili ya kupewa nafasi katika kikosi cha maofisa wa akiba, ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara, wanawake na vijana.
Kwa mujibu wa mkuu wa polisi wa mkoa wa Kaskazini Mashariki Charlton Mureithi, viunga kumi ambavyo vilibainishwa kama vilikuwa vikiwahifadhi al-Shabaab vitakuwa na askari kumi wa akiba kila moja.
"Baada ya mafunzo yao maalumu, wataeneza katika viunga vya jirani, ambavyo wanavielewa vizuri, kuwafukuza magaidi na wale wote walio nyuma ya matukio ya upigaji risasi mjini," aliiambia Sabahi. "Hatuna tarehe maalumu watakapoenea, lakini tunatarajia kuwa itakuwa hivi karibuni kwa sababu ya vitisho vya muda mrefu."
Kuwahakikishia usalama polisi wa akiba, shughuli zao zitakuwa zikijulikana na viongozi wachache wa usalama. "Tunataka waongeze nguvu katika usalama wa mji bila kutambulika. Tunaamini watakuwa kiungo muhimu kati ya jamii na mamlaka hiyo," alisema Mureithi.
Zaidi ya kueneza jeshi la polisi wa akiba, mamlaka zitataka teksi zote zinazofanya kazi ndani na nje ya Garissa kuwa na namba za utambulisho zilizochorwa katika magari yao zikiwa kubwa na rahisi kusomeka, alisema Mureithi.
"Tumegundua kwamba teksi zimekuwa zikitumika kama njia ya kupitisha wahalifu, na ni vigumu kwa mashuhuda kushika namba kwa gari linalotembea," alisema.
Aidha, alisema magari yote yatazuiliwa kuwa na madirisha yenye vioo vya rangi ya giza.

Wananchi walisaidia jeshi kwa tahadhari

Sheikh Abdullahi Salat, mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu Kenya huko Garissa, alipongeza jitihada za usalama, lakini alitahadharisha kwamba serikali inapaswa kuwa makini kutoruhusu wanachama wa kitengo kipya kufanya mauaji mengine kwa jina la kukabiliana na ugaidi.
"Wananchi waliopata mafunzo wanapaswa kufikia viwango vya juu vya maadili ili kufanya operesheni zao ndani ya sheria zao za nchi," Salat aliiambia Sabahi. "Kama ikiwezekana, washukiwa wanapaswa kukabidhiwa kwa serikali kwa ajili ya hukumu ya kisheria kutawala."
Serikali inapaswa kuwajibika kama kikosi kitawadhuru watu wasiokuwa na hatia, alisema, akiongeza kwamba serikali inapaswa pia kufafanua jinsi inavyopendekeza kuwatuliza maofisa wa KPR mara vitisho vya ugaidi vitakapoondoshwa.
John Chege, anayemiliki Hoteli ya Holiday Inn huko Garissa, eneo ambalo lilitokea ghasia za mauaji mwezi uliopita, alisema alipenda kikosi kisambazwe haraka iwezekanavyo kusaidia jumuiya ya wafanyabiashara.
Wafanyabiashara wengi wanakimbia Garissa kwa sababu mashambulio ya mara kwa mara yameharibu biashara, aliiambia Sabahi. Kwa hiyo, serikali inapaswa kujaribu kila linalowezekana kurejesha ujasiri wa wafanyabiashara na kueneza kukua kwa uchumi, alisema.