Monday, June 3, 2013

Mamlaka ya Zanzibar Kwanza

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akiwahutubia wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti kusherehea “Umoja na mshikamano wa Wazanzibari”
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akiwahutubia wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti kusherehea “Umoja na mshikamano wa Wazanzibari”
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, ameunga mkono kauli iliyotolewa na Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Eddi Riyami ya kuwataka Wazanzibari wasiotaka mamlaka kamili ya Zanzibar wajitokeze hadharani kama wanavyofanya wale wanaodai mamlaka kamili ya Zanzibar.
Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF ameeleza hayo katika viwanja vya Kibanda maiti mjini Zanzibar katika mkutano wa hadhara uliolenga kusherehekea “Umoja wa Wazanzibari” ulioasisiwa kufuatia maridhiano ya kisiasa.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Amesema hatua ya Wazanzibari kudai mamlaka ni haki yao, na kwamba hakuna dhambi ya kudai jambo hilo.
Amefahamisha kuwa wazanzibari walio wengi wameungana kudai mamlaka ya nchi yao kwa njia ya amani na demokrasia, na kutoa wito kwa wale wasiotaka mamlaka ya Zanzibar wajitokeze hadharani.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti wakinyosha mikono na kucheza wakati wakisherehekea hotoba ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya kibanda maiti wakinyosha mikono na kucheza wakati wakisherehekea hotoba ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Amewahakikishia wananchi kuwa hatorudi nyuma katika kuitetea Zanzibar kuwa na mamlaka yake, ili iweze kutambulika kimataifa na kuweza kuratibu na kushughulikia mambo yake ya nje.
Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Eddi Riyami,  akitoa salamu za Mwenyekiti wa Kamati hiyo Hassan Nassor Moyo katika viwanja vya kibanda maiti mjini Zanzibar.
Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Eddi Riyami, akitoa salamu za Mwenyekiti wa Kamati hiyo Hassan Nassor Moyo katika viwanja vya kibanda maiti mjini Zanzibar.
Kwa upande wake Katibu wa kamati ya maridhiano Ismail Jussa Ladhu, amewaomba viongozi wa vyama vyote kushirikiana na wananchi  katika kudai mamlaka ya nchi, ili wazanzibari waweze kujikomboa kutokana na kile alichokiita ukoloni wa Tanganyika.
Katibu wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Ismail Jussa Ladhu akizungumza na wananchi katika viwanja vya Kibanda maiti.
Katibu wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Ismail Jussa Ladhu akizungumza na wananchi katika viwanja vya Kibanda maiti.
Katika risala ya wananchi wa mikoa mitano ya Zanzibar iliyosomwa na Ameir bin Ameir kutoka Bwejuu, amesema pamoja na mambo mengine, katiba mpya izingatie uwepo wa Jamhuri ya Zanzibar na uraia wake.
Mambo mengine waliyotaka yatolewe katika orodha ya mambo ya Muungano ni pamoja na sarafu, benki kuu, mambo ya nje, vyama vya siasa, baraza la mitihani pamoja na mafuta na gesi.

No comments:

Post a Comment