Saturday, June 1, 2013

FACEBOOK WAMEKUJA NA "VERIFIED ACCOUNT " NA RAIS UHURU AWA WA KWANZA.

Facebook imefuata mkondo Twitter kwa kuanzisha akaunti na kurasa zilizothibitishwa (verified pages/accounts) ili kuwawezesha watu mashughuli kuthibitisha akaunti akaunti na fan page zao. Facebook wamesema wamefanya hivyo ili kusaidia watumiaji wa Facebook kuzitambua akaunti za kweli za mastaa na watu wengine mashughuli wanaotumia mtandao huo, pia ikiwemo biashara zenye majina makubwa.

Kurasa zilizothibitishwa zitakua na alama ya blue ya pata “check-mark” kama inavyoonekana kwenye picha hapo juu. Watu wataoruhusiwa kutumia huduma hiyo ni, viongozi wa serikali, waandishi wa habari maarufu, makampuni au bidhaa maarufu. Hivyo kuanzia sasa, utaweza kufahamu akaunti/pages zipi ni za kweli na zipi ni feki.

Ili mtu mashughuli kupata akaunti iliyohakikishwa, mhusika atahitaji kuwasilisha kitambulisho halali kinachotambuliwa kiserikali. Nadhani celebrities (mastaa) Wengi wa Afrika wataipenda hii. Kama mfano Wema, kuna page zaidi ya kumi zinazodai kuwa ni “Wema Sepetu”

WANYARWANDA WANASWA LIVE WAKIJIUZA JIJINI DAR


POLISI Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam imeendesha oparesheni maalum ya kuwanasa machangudoa wanaofanya biashara hiyo haramu katika eneo lao na kufanikiwa kuwaweka ‘mtu kati’ makahaba kibao, wakiwemo raia wa Rwanda na Burundi...
Kamatakamata hiyo ilichukua nafasi usiku mnene wa Alhamisi ya Mei 23, mwaka huu kwenye danguro kubwa la makahaba lililopo Kariakoo, jijini Dar ambalo machangu hao hutegea mingo zao kwa ajili ya kuwanasa wateja.

Katika hali iliyowashangaza polisi, midume iliyokutwa na makahaba hao ilitimua mbio ili kujiokoa na mtego huo wa polisi uliodhamiria kusafisha eneo la Kariakoo kwa ukahaba uliopitiliza.
Baadhi ya wanaume wakati wakitimua mbio walisikika wakisema kuwa wakukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya dola ni wanawake hao kwa vile wanavaa kimitego huku wakijua binadamu anapitiwa na shetani wakati wowote.
“Sisi kosa letu nini? Wakamateni haohao machangudoa, watavaaje kimitego mbele yetu sisi wanaume? Shetani naye atakuwa wapi wakati huo?” alisikika akisema mmoja wa wanaume hao huku akichanganya miguu kupita kawaida.
 
Awali kabla ya zoezi la kuwanasa makahaba hao halijaanza, afande mmoja alipowauliza wanachofanya hapo, kahaba mmoja aliuliza: Una maswali mengi kwani we ni polisi?

Mei 24, mwaka huu, makahaba hao walipandishwa kwenye Mahakama ya Jiji na kusomewa mashitaka yao na mwendesha mashitaka, John Kijumbe mbele ya Hakimu Timoth Lyoni.
Waliosomewa mashitaka ni Natasha Bahati, 30 (Mrundi), Asma Athuman, 23 (Mrundi), Niyonkuru  Evelinde, 29 (Mnyarwanda), Zaimana Hawa, 20 (Mrundi) na Wabongo 35.
 
Wote walikana mashitaka lakini walipelekwa Gereza la Segerea, jijini Dar baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Chris Grayling: Only the highest earners will be denied legal aid under Government reforms

People will only be denied legal aid if they earn over £100,000, Chris Grayling has said, as he defended flagship Government reforms to the justice system. 

Mr Grayling, the Justice Secretary, insisted that his changes to the legal aid system will only hit the wealthiest following warnings from experts that they will leave middle-class families with huge fees.
He was responding to claims made by Alistair MacDonald QC, Vice Chairman of the Bar Council, who said that the reforms will create a two-tier justice system where only the wealthiest can afford to have the defence of their choice.
Mr McDonald warned that the legal aid reforms will hit thousands of "hard working people" who in cases because they "defend their homes against a burglar, clip a cyclist accidentally, they become involved in a dispute with their neighbour or their sons or daughters get into trouble".
Critics have said that people earning more than £37,500 will be denied legal aid under the new system, but sources in the Justice department pointed out that this figure is after people have paid tax, national insurance, their mortgage, council tax, childcare and paid for all of their living expenses.
“The changes to entitlement to legal aid are really designed only to affect people earning £100,000-a-year or more,” Mr Grayling said

Foreign Office warns against travel to parts of Turkey after protests

The Foreign Office has warned against all but essential travel to parts of Turkey after two days of fierce clashes between police and protesters.

Tear gas fired at protesters in Istanbul
 Protestors clash with Turkish riot policemen during a protest against the demolition of Taksim Gezi Park inIstanbul. Police reportedly used tear gas on a group standing guard in Gezi Parki to prevent the Istanbul metropolitan municipality from demolishing the last remaining green public space in the center of the city.

An environmental demonstration in Istanbul on Friday quickly spiralled into a wider, violent nationwide protests against Prime Minister Recep Tayyip Erdogan's increasingly authoritarian government.
The Foreign Office advised Britons to avoid the areas where protests were taking place in Istanbul, Ankara and several other cities, while it warned against all but essential travel to areas in the east and south-east of the country.
"Demonstrations are taking place in Istanbul and in other cities across Turkey, including Ankara. Police are using tear gas and water cannons in response. We advise British nationals to avoid all demonstrations," the Foreign Office said.
"Demonstrations occur regularly in major cities and have the potential to turn violent."
Tear gas and water canon were deployed against hundreds of people trying cross the Bosporus Bridge to reach Istanbul's central Taksim square on Saturday, while in Astana, protesters were blocked from marching on the parliament.

Maandamano yaendelea Uturuki

 1 Juni, 2013

Polisi wamepambana tena kwa ghasia na waandamanaji wanaopinga serikali ya Uturuki.
Uharibifu katika maandamano kwenye medani ya Taksim, Istanbul
Mapambano yaliyoanza Ijumaa yanaendelea kusambaa.
Kitovu cha maandamano ni medani ya Taksim mjini Istanbul ambako polisi wametumia moshi wa kutoza machozi na ambapo ghasia nyingi zilitokea Ijumaa.
Mkaazi mmoja wa Istanbul aliiambia BBC kwamba watu zaidi wanaelekea katika eneo hilo:
"Watu 40,000 wanavuka daraja ya Bosphorus kutoka upande wa Uturuki ulioko Asia kuja ng'ambo ya Ulaya kujiunga na maandamano katika medani ya Taksim.
Safari zote za treni zimesimamishwa ili kuzuwia watu wasije, lakini wanatembea kwa miguu - kila mtu anatembea - na hapa nilipo naweza kusikia ghasia kutoka medani ya Taksim.
Tuko kama mwendo wa dakika 5 tu kutoka medani.
Kwa hivo nafikiri maandamano yanaendelea na pengine kuwa ya ghasia zaidi kushinda Ijumaa."
Maandamano yalianza siku nne zilizopita kupinga mpango wa kujenga maduka katika bustani iliyo karibu na medani ya Taksim.
Waandamanaji, ambao wengi ni vijana, wanaishutumu serikali ya chama cha Kiislamu kwamba inakuwa ya kimabavu.

Waandamanaji wavamiwa kanisani Zambia

 31 Mei, 2013 
Serikali inaodnoa ruzuku ili kupunguza matumizi ya pesa zake
Wafuasi wa chama tawala nchini Zambia, wamevamia kundi la waandamanaji waliokuwa ndani ya kanisa katika mji mkuu Lusaka
Waandamanaji hao waliokuwa wamepanga kufanya maandamano kupinga kuondolewa kwa ruzuku kwa bidhaa muhimu, walikusanyika kanisani baada kuzuiwa na polisi kuandamana.
Aidha wawili kati yao wamelazwa hospitalini baada ya kujeruhiwa vibaya, kwa mapanga na silaha zengine za kijadi.
Hatua ya serikali kuondoa rukuzu kwa bidhaa muhimu , imepokelewa kwa ghadhabu na watu nchini Zambia.
Waandamanaji walikuwa wameomba kibali cha kuandamana lakini wakanyimwa na polisi kwa sababu za kiusalama.
Kwa hivyo walilazimika kuhamishia maandamano yao kanisani, kwa sababu hawahitaji kibali cha kukusanyika kanisani
Uamuzi wa serikali wiki mbili zilizopita kufutilia mbali ruzuku kwa Unga wa mahindi, imesababisha kilio kutoka kwa wananchi ambapo asilimia 60 ya wananchi ni maskini, wakiwa wanaishi kwa dola tatu kwa siku.
Hatua hiyo hata hivyo ilinuia kupunguza matumizi ya pesa za serikali.
Serikali pia imesema kuwa waliokuwa wanafaidika zaidi na ruzuku ni maajenti wala sio watu maskini.