Tuesday, April 16, 2013

Karim Wade atiwa nguvuni kwa ulaghai

 16 Aprili, 2013 - Saa 08:07 GMT

Karim Wade
Mwanawe rais wa zamani wa Senegal Abdoulaye Wade, ametiwa nguvuni kwa kujipatia dola bilioni 1.4 wakati wa utawala wa baba yake .
Karim Wade ambaye alihudumu katika serikali ya baba yake alikuwa na nyadhifa mbali mbali wakati huo .
Wade aliwasilisha waraka wa orodha ya mali zake katika mahakama maalum ya senegali iliyopewa jukumu la kuchunguza kesi za ufisadi jana asubuhi.
Alipewa muda wa mwezi mmoja kuthibitisha kuwa alichukua zaidi ya dola dola bilioni kihalali wakati baba yake alipokuwa madarakani.
Karim Wade alipewa jina la bandia waziri wa anga na dunia , alipokuwa waziri wa miundo mbinu , mipango ya miji , usafiri wa anga na ushirikiano wa kimataifa kwa wakati mmoja.
Wakati huo pia alikuwa mkuu wa theluthi moja ya matumizi ya taifa . Mahakama ya Senegali bado haijaeleza sababu ya kumtia rumande na mawakili wa Karim Wade wamesema alichukuliwa kwa nguvu .

Karim Wade atiwa nguvuni kwa ulaghai

 
 Mwanawe rais wa zamani wa Senegal Abdoulaye Wade, ametiwa nguvuni kwa kujipatia dola bilioni 1.4 wakati wa utawala wa baba yake .

Karim Wade ambaye alihudumu katika serikali ya baba yake alikuwa na nyadhifa mbali mbali wakati huo .
Wade aliwasilisha waraka wa orodha ya mali zake katika mahakama maalum ya senegali iliyopewa jukumu la kuchunguza kesi za ufisadi jana asubuhi.
Alipewa muda wa mwezi mmoja kuthibitisha kuwa alichukua zaidi ya dola dola bilioni kihalali wakati baba yake alipokuwa madarakani.
Karim Wade alipewa jina la bandia waziri wa anga na dunia , alipokuwa waziri wa miundo mbinu , mipango ya miji , usafiri wa anga na ushirikiano wa kimataifa kwa wakati mmoja.
Wakati huo pia alikuwa mkuu wa theluthi moja ya matumizi ya taifa . Mahakama ya Senegali bado haijaeleza sababu ya kumtia rumande na mawakili wa Karim Wade wamesema alichukuliwa kwa nguvu .

Students in N Korea

Students march at a camping site in Pyongyang as the first term of camping commences nationwide, to commemorate the 101st anniversary of the birth of North Korea's founder Kim Il-sung, in this photo distributed by North Korea's official Korean Central News Agency (KCNA) on April 15, 2013. North Korea celebrated the anniversary of its founder's birth on Monday and abandoned its shrill threats of war against the United States and the South, easing tensions in a region that had seemed on the verge of conflict. REUTERS/KCNA (NORTH KOREA - Tags: ANNIVERSARY MILITARY POLITICS EDUCATION) ATTENTION EDITORS - THIS PICTURE WAS PROVIDED BY A THIRD PARTY. REUTERS IS UNABLE TO INDEPENDENTLY VERIFY THE AUTHENTICITY, CONTENT, LOCATION OR DATE OF THIS IMAGE. THIS PICTURE IS DISTRIBUTED EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS. NO THIRD PARTY SALES. NOT FOR USE BY REUTERS THIRD PARTY DISTRIBUTORS




Watu 17 wauawa Jamuhuri ya Afrika ya Kati

 15 Aprili, 2013 - Saa 13:58 GMT
Waasi wa Seleka
Takriban watu kumi na saba waliuawa katika makabiliano yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati.
Hii ni kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu, Red Cross.
Mapigano yalizuka baada ya waasi wa zamani waliokuwa wanashika doria katika Ikulu ya rais aliyeondolewa mamlakani
Francois Bozize kushambuliwa.
Msemaji wa serikali mpya alisema kuwa kiongozi wa waasi, Michel Djotodia alitangazwa kuwa rais wa mpito mnamo Jumamosi.
Kundi lake la waasi lilichukua mamlaka wiki tatu zilizopita.
Mapambano yaliyotokea Jumamosi na Jumapili yalikuwa mabaya zaidi kuwahi kushuhudiwa mjini
Bangui tangu kung'olewa mamlakani kwa bwana Bozize.
Kombora liliangukia kanisa la Baptist siku ya Jumapili na kuwaua watu watatu.
Kasisi wa kanisa hilo alikatwa mkono wake baada ya kujeruhiwa vibaya kwenye shambulio hilo.
Kundi la waasi la Seleka lililoipindua serikali ya Rais Fracois Bozize

Kaimu msemaji wa serikali ,generali Moussa Dhaffane, alisema kuwa makabiliano yalizuka wakati vijana waliwashambulia wanajeshi waasi, katika eneo Boy-Rabe, eneo linalosemekana kuwa ngome ya bwana Bozize.
Maafisa wa shirika la Red Cross walisema kuwa watu 17 waliuawa katika sehemu mbali mbali za mji mkuu.
Wenyeji walisema kuwa vijana wengi wanataabika kufuatia hali mbaya ya usalama mjini Bangui.
Baadhi wakiwatuhumu waasi hao kwa uporaji.
Baraza la kitaifa la mpito, lililoundwa baada ya kupinduliwa kwa rais Bozize lilimteua bwana Djotodia kama rais wa muda siku ya Jumapili.
Taarifa iliyotiwa saini na Francois Bozize kutoka kwa idara ya mawasiliano ililaani vikali mapinduzi hayo.
Aidha bwana Bozize alikimbilia Cameroon wakati waasi walipowasili Bangui.
Bwana Djotodia alisema kuwa ataandaa uchaguzi katika kipindi cha miezi 18
Kundi la waasi la Seleka, lilitwaa mamlaka, baada ya mkataba wa amani waliotia saini na rais Bozize kusambaratika.


Lashukiwa kuwa shambulio la kigaidi

 16 Aprili, 2013 - Saa 06:41 GMT

Milipuko miwili mikubwa iliyotokea kwenye mstari wa mwisho wa kumalizia mbio za Boston Marathon nchini Marekani imewauwa watu watatu na kuwajeruhi wengine zaidi ya mia moja.
Mlipuko wa pili ulitokea sekunde chache tu baada ya ule wa kwanza kutokea wakati mamia ya wanariadha wakikamilisha mbio zao huku wakishangiliwa na umati. Waliojeruhiwa walikimbizwa hospitalini huku wengi wao wakitokwa na damu.
Duru zinasema kuwa majasusi wa FBI wameanzisha uchunguzi katika kile wanachosema huenda yalikuwa mashambulizi ya kigaidi.
Rais Barack Obama amesisitiza kuwa serikali serikali itakahikisha kuwa washukiwa wa mashambulizi hayo lazima atakamatwa.
Picha na video kutoka Boston zilionyesha watu wakiwa wamechanganyikiwa wasijue pa kwenda, huku magari ya huduma za dharura yakielekea katika eneo la tukio na watu waliojeruhiwa vibaya wakipelekwa kwenye hema la matibabu ya haraka.
"Kuna watu wengi wamelala chini," alisema mwanariadha mmoja akinukuliwa na chombo cha habari cha AP.
Tukio hilo linaripotiwa kutokea saa tatu baada ya washindi kuvuka mstari wa ushindi.
"Kulikuwa na mlipuko, polisi, moto na EMS kwenye eneo la tukio. Hatuna namna ya kufahamu namna watu walivyojeruhiwa," msemaji wa Polisi Boston alisema.
Shirika la habari la AP linasema kulikuwa na sauti kubwa ya mlipuko upande wa kaskazini mwa mtaa wa Boylston Street, karibu tu daraja linaashiria mstari wa kumalizia mashindano. Mlipuko mwingine ukasikika dakika chache baadaye.
Mike Mitchell wa Vancouver kutoka Canada, mwanariadha aliyemaliza kukimbia alisema alikuwa akiangalia nyuma ya mstari wa kumalizia mashindano ndipo aliposikia ‘mlipuko mkubwa’
Inataarifiwa kuwa moshi ulipanda juu hewani kiasi cha futi 50 (mita 15),' aliliambia shirika la habari la Reuters , na watu wakaanza kukimbia wakipiga mayowe baada ya kusikia
Wanariadha waliomaliza mbio za Boston Marathon
"Kila mtu alichanganyikiwa,’ alisema.
Waliokuwa wakimalizia mbio hizo waliongozwa kuepuka eneo lenye moshi kwenye mlipuko wakati huo huo eneo hilo likifungwa.
Tawi la Msalaba Mwekundu la Mashariki mwa Massachusetts limetenga kituo cha kusaidia majeruhi.