Saturday, June 1, 2013

FACEBOOK WAMEKUJA NA "VERIFIED ACCOUNT " NA RAIS UHURU AWA WA KWANZA.

Facebook imefuata mkondo Twitter kwa kuanzisha akaunti na kurasa zilizothibitishwa (verified pages/accounts) ili kuwawezesha watu mashughuli kuthibitisha akaunti akaunti na fan page zao. Facebook wamesema wamefanya hivyo ili kusaidia watumiaji wa Facebook kuzitambua akaunti za kweli za mastaa na watu wengine mashughuli wanaotumia mtandao huo, pia ikiwemo biashara zenye majina makubwa.

Kurasa zilizothibitishwa zitakua na alama ya blue ya pata “check-mark” kama inavyoonekana kwenye picha hapo juu. Watu wataoruhusiwa kutumia huduma hiyo ni, viongozi wa serikali, waandishi wa habari maarufu, makampuni au bidhaa maarufu. Hivyo kuanzia sasa, utaweza kufahamu akaunti/pages zipi ni za kweli na zipi ni feki.

Ili mtu mashughuli kupata akaunti iliyohakikishwa, mhusika atahitaji kuwasilisha kitambulisho halali kinachotambuliwa kiserikali. Nadhani celebrities (mastaa) Wengi wa Afrika wataipenda hii. Kama mfano Wema, kuna page zaidi ya kumi zinazodai kuwa ni “Wema Sepetu”

No comments:

Post a Comment