Friday, June 7, 2013

Wasomali Afrika.K walaani mashambulizi



Watu wa jamii ya wasomali nchini Afrika Kusini, wameandamana hadi bunge la la kitaifa mjini Cape Town kupinga mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni nchini humo.
Raia wawili wasomali, wameuawa mwezi huu na serikali ya Somalia imeiomba Afrika Kusini kuchukua hatua zaidi kuweza kuwalinda raia wake.
Takriban watu 200 waliandamana wakibeba mambango yaliyoandikwa: ''kila mtu ni raia wa kigeni katika sehemu fulani ya dunia''
Waandishi wa habari wanasema kuwa mashambulizi dhidi ya waafrika wasio raia wa Afrika Kusini yameanza kutekelezwa katika siku za hivi karibuni.
Baadhi ya waandamanaji waliwashtumu maafisa wa utawala kwa kutochukua hatua zaidi kuwalinda raia wa kigeni , hususan wasomali.
Kulingana na kitengo cha haki za bindamu katika chuo kikuu mjini Pretoria,raia wa Afrika Kusini hawajakuwa wakionywa dhidi ya kuwashambulia raia wa kigeni .
Mwandishi wa BBC Mohammed Allie mjini Cape Town wanasema kuwa ghasia hizo zinahusishwa na kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira, nchini Afrika Kusini.
Katika miaka ishirini iliyopita, maelfu ya wasomali wametoroka vita nchini Somalia na kuhamia Afrika Kusini ambako wameweza kuanzisha biashara ndogondogo katika sehemu za mijini.

No comments:

Post a Comment