Friday, June 7, 2013

Lishe bora duniani ipewe kipaombele

Utapia mlo ni tatizo ambalo linakumba sehemu nyingi duniani
Utapia mlo husababisha asilimia 45 ya vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kote duniani. Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa kwenye jarida la matabibu la Lancet.
Utafiti huo unasema kuwa , lishe duni husababisha vifo vya watoto milioni 3.1 walio chini ya umri wa miaka mitano kila mwaka
Kikundi cha kimataifa kilidurusu sababu mbali mbali zinazochangia kuwepo utapia mlo miongoni mwa akina mama wajawazito na watoto wachanga.
Wanasema kuwa siku za kwanza miamoja za maisha ya mtoto, huwa muhimu sana kwa maisha ya mtoto yule.
Utapia mlo ambao kwa upande mmoja unamaanisha kuwa uzani wa juu kupita kiasi au kukosa lishe bora, pia ina athari zake kiuchumi.
Kulingana na ripoti ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa, utapia mlo hugharimu dunia dola trilioni 3.5 hadi trilioni miatano kwa kila mtu upande wa matibabu na kazi.
''Upande wa afya ya uzazi na afya ya watoto, hali inaweza kuiamarishwa, matokeo mazuri yanaweza kukuza kizazi sababu ambayo inatupasa kushirikiana kuchukua nafasi hii nzuri,'' alisema daktari Richard Horton
Kikundi cha madaktari kilichoongozwa na Profesa Robert Black, kilidurusu utafiti kuhusu utapia mlo kwa watoto na akina mama wajawazito katika nchi maskini duniani tangu mwaka 2008.
Wataalamu hao pia walidurusu uimarishaji wa mipango ya kitaifa na kimataifa kuhusu lishe bora kwa watoto na akina mama wajawazito.
Aidha wanasema kuwa licha ya hatua kupigwa katika miaka ya hivi karibuni, wanakadiria kuwa zaidi ya watoto milioni 165, walikumbwa na utapia mlo pamoja na kudumaa.
Watoto 900,000, wanaweza kuokolewa katika nchi 34 ikiwa viwango vya lishe bora vinaweza kuboreshwa hadi asilimia 90 ya dunia nzima
Watafiti wanaonya kuwa Nchi hazitaweza kujiondoa kwa umaskini ikiwa dunia haiwezi kuweka swala la lishe bora kuwa kipaombele duniani.
Daktari Richard Horton, mhariri mkuu wa jarida la Lancet, alisema kuwa ikiwa viwango vya lishe bora vinaweza kuboreshwa , matokeo yake mazuri yanaweza kufaidi kikazi kijacho.
Wataalamu wanaofanya kazi katika nchi zinazokuwa wanakutaka wikendi hii mjini London, kwa mkutano unaoandaliwa na serikali za Uingereza na Brazil.
Mkutano huu utafuatwa na mkutano mwingine wa kila mwaka wa nchi zilizostawi kiuchumi duniani za G8.
Kampeini inayohamasisha chakula cha kutosha kwa kuchangisha dola bilioni moja kila mwaka kama pesa za ziada za msaada kuweza kutumika kwa miradi ya lishe bora ifikapo mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment