Friday, June 7, 2013

Umoja wa Mataifa kuisaidiaTanzania kuanzisha benki ya wakulima

Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limekubali kuisaidia Tanzania kuanzisha benki teule ya wakulima, gazeti la Daily News la Tanzania liliripoti Jumatano (tarehe 5 Juni).
"Ahadi yangu kwenu ni kwamba FAO itawasiliana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuona jinsi tunavyoweza kusaidia kuanzisha benki," Mkurugenzi Mkuu wa FAO Jose Graziano da Silva alimwambia Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete.
Da Silva alisifu jitihada za Tanzania za kuwasaidia wakulima, lakini alisema mkazo unapaswa kuwa katika kutoa mikopo kwa wakulima kuliko ruzuku, ambazo aliziita si endelevu.

No comments:

Post a Comment