Friday, June 7, 2013

Waandishi wa habari wa Kenya watishia bunge kwa kuzuia vyombo vya habari

Waandishi wa habari walitishia kusimamisha kutoa habari za bunge Jumatano (tarehe 5 Juni) baada ya Ofisa wa bunge Justin Bundi kuwafukuza kwenye kituo cha habari katika bunge.
"Hatua kama hiyo haijawahi kutokea katika Kenya huru," Mwenyekiti wa chama cha Wahariri cha Kenya Macharia Gaitho alisema kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la Kenya. "Wamerudi kwenye zama za kale za kutwezwa, udikiteta na haitegemewi kabisa katika jamii ya kisasa, yenye maendeleo na yenye demokrasia."
Gaitho na wanachama wa chama hicho walitia saini taarifa inayosema watavitaka vyombo vya habari kusimamisha kuchukua matukio ya habari za bunge hadi ufikivu wa vyombo vya habari uliozuiliwa urejeshwe.
Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari Alphonce Shiundu alisema kuzuia vyombo vya habari kuchukua habari za matukio kutaipeleka Kenya "kwenye zama za siku za giza", kwa mujibu wa Capital FM ya Kenya. "Wakenya wanahitaji kuwasikiliza viongozi wao. Waandishi wa habari wanahitaji kuwaambia Wakenya nini viongozi wao wamesema katika bunge."

No comments:

Post a Comment