Friday, June 7, 2013

Kenya, Somalia yaanzisha kikundi kazi cha kurejesha nyumbani wakimbizi

Kenya na Somalia zimeunda kikundi kazi cha pamoja kuanzisha njia ya kuwarejesha nyumbani na upataji wa makaazi mapya kwa wakimbizi wa Somalia nchini Kenya, gazeti la Daily Nation la Kenya liliripoti Jumatano (tarehe 15 Juni).
Kikundi kazi, kilichoundwa kufuatia kikao cha Nairobi baina ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud, kitatoa vigezo kwa ajili ya majadiliano kwenye mkutano huo kuhusu wakimbizi uliopangwa kufanyika mwezi Agosti.
Kenyatta alitoa wito kwa jumuiya za kimataifa kusaidia jitihada za upataji wa makaazi mapya kwa wakimbizi, akisema uwepo wa idadi kubwa ya Wasomali nchini Kenya kumekuwa na athari hasi kwenye uchumi wa nchi, usalama na mazingira.
Mohamud aliishukuru Kenya kwa mchango wake kwenye Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia, akitoa salamu zake za rambirambi kwa vifo vya Wakenya na askari wengine.

No comments:

Post a Comment