Monday, April 22, 2013

Wasingizia umaskini kuwatumikisha watoto

 22 Aprili, 2013 - Saa 15:07 GMT

Katika nchi nyingi duniani wazazi hutumikisha watoto
Mkutano wa kimataifa kuhusu utumikishwaji wa watoto wa Kampala umetoa mapendekezo kadhaa mkiwemo kupinga dhana eti umaskini ndio sababu kuu ya utumikishwaji huo na pia kupinga dhana nyingine kuwa ndio kigingi muhimu cha kuweka elimu ya msingi kwa kila mtoto.
Mapendekezo hayo yalitolewa mwishoni mwa mkutano huo, mwishoni mwa juma.
Wajumbe kutoka mataifa 26 wametoa tamko la kuyaomba mataifa yote ambayo yalitia sahihi ya hali ya watoto ya Umoja wa Mataifa, kutekeleza wajibu wa kutoa elimu ya bure na ya lazima kwa watoto.
Aidha tamko hilo linazitaka nchi za kiafrika ambazo ziko chini ya kivuli cha Muungano wa Afrika kuchukua wadhifa kama unavyoambatanishwa katika mkataba wa Afrika kuhusu haki na maslahi ya watoto.
Miongoni mwa sababu nyingi za kuwatumikisha watoto ni umaskani wa kipato,lakini mmoja wa washiriki Christopher Luyenga kutoka Tanzania,akishughulikia sekta ya uzalishaji wa tumbaku analipinga hilo akitoa ufafanuzi kutokana na mkutano huo.
Yeye muwakilishi wa mashirika yanayohusika na watoto nchini Kenya na alietoa muhtasari wa yaliyojadiliwa katika mkutano huo, Timothy Ekesa, anasema kuwa mkutano wa Kampala ulikuwa wenye umuhimu mkubwa kwa maslahi ya watoto.
Moja wa kizungumkuti kwa jamii ni hali ya watoto kubaki mayatima na kuwabidi watoto hao kujitegemea.
Kutokana na mkutano huo imebaishiwa kuwa takriban watoto million 215 duniani baado wanatumikishwa na idadi hiyo inaweza kuwa imeongezeka katika kipindi cha miaka michache iliopita kutokana na migogoro sio tu ya kijamii lakini pia ya kiuchumi.
Barani Afrika chini ya jangwa la sahara inakisikiwa watoto wanaotumikishwa wanafikia million 65.Wajumbe wa mkutano wa kampala wamesema kuwa ni haki ya mtoto kupewa elimu na pia kusisitiza kuwa ajira ya mtoto pia ni elimu.


No comments:

Post a Comment