Tuesday, June 4, 2013

Uzinduzi Wa Rasimu Ya Katiba Mpya Ya Tanzania

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akionesha Rasimu ya Katiba mpya ya Tanzania
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akionesha Rasimu ya Katiba mpya ya Tanzania.
62.-(1) Kila Mshirika wa Muungano atakuwa na mamlaka na haki zote juu ya mambo yote yasiyo ya Muungano, na katika utekelezaji wa mamlaka hayo, kila Mshirika wa Muungano atazingatia misingi ya ushirikiano na mshirika mwingine kwa kuzingatia haki na usawa kwa ajili ya ustawi ulio bora kwa wananchi wa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad akipokea nakala ya rasimu ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Makamu wa Rais Muungano Dkt Gharib Bilal, huku Jaji Mstaafu Joseph Warioba akishuhudia
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad akipokea nakala ya rasimu ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Makamu wa Rais Muungano Dkt Gharib Bilal, huku Jaji Mstaafu Joseph Warioba akishuhudia.
62.-(2) Bila ya kuathiri mipaka iliyowekwa na Katiba hii, kila Mshirika wa Muungano atakuwa na uwezo na uhuru wa kuanzisha mahusiano au ushirikiano na jumuiya au taasisi yoyote ya kikanda au kimataifa kwa mambo yaliyo chini ya mamlaka yake kwa mujibu wa Katiba ya Mshirika wa Muungano.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Idd  akipokea nakala ya rasimu ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Makamu wa Rais Muungano Dkt Gharib Bilal, huku Waziri Mkuu Mizengo Pinda akishuhudia  akishuhudia
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Idd akipokea nakala ya rasimu ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Makamu wa Rais Muungano Dkt Gharib Bilal, huku Waziri Mkuu Mizengo Pinda akishuhudia akishuhudia.
62.-(3) Mshirika wa Muungano anaweza, wa kati wa kutekeleza majukumu yake chini ya Ibara ndogo ya (2), kuomba mashirikiano kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa ajili ya kufanikisha mahusiano na jumuiya au taasisi ya kimataifa au kikanda, na Serikali ya Jamhuri Muungano inaweza kutoa ushirikiano kwa mshirika huyo kwa namna itakavyohitajika. - Mamlaka ya Washirika wa Muungano
Pata nakala kamili ya Rasimu ya Katiba mpya hapa: Rasimu

No comments:

Post a Comment