Wednesday, May 29, 2013

Ulamaa wa Kenya ataka adhabu ya kifo kwa wanachama wa al-Shabaab wanaopinga uongozi

Watu wanaochochea mgawanyiko ndani ya al-Shabaab na wanaompinga kiongozi wa kundi hilo, Ahmed Godane, lazima wauawe, alisema ulamaa na muungaji mkono mkubwa wa al-Shabaab, Sheikh Hassan Hussein Aadan, iliripoti Redio RBC ya Somalia siku ya Jumanne (tarehe 28 Mei).
"Nimesikia kuwa kuna migawanyiko ndani ya wapiganaji wa jihadi. Anayetengeneza migawanyiko hiyo lazima auawe," alisema Aadan, ulamaa wa Kenya mwenye asili ya Somalia anayeishi Nairobi. "Naamini mtu anayejaribu kuzuia jihad lazima auawe."
Aadan amewahimiza watu kwenda mstari wa mbele na kujiunga na kile alichokiita "jihad" nchini Somalia.
Kauli ya Aadan imekuja baada ya kiongozi wa juu wa al-Shabaab, Hassan Dahir Aweys, kumkosoa vikali Godane katika mahojiano yaliyorushwa tarehe 16 Mei na televisheni ya Somali Channel, akimtuhumu kwa udikteta, kulitekaji nyara kundi hilo ili kutanua himaya yake na kupuuzia maoni ya viongozi wengine wa al-Shabaab.

No comments:

Post a Comment