Wednesday, May 29, 2013

Jeshi la Kenya kuwanyang'anya silaha kwa nguvu wakaazi wa Mandera

Baada ya kuwaomba wakaazi wa Mandera kusalimisha silaha zao, Inspekta Jenreali wa Polisi, David Kimaiyo, alitangaza siku ya Jumatatu (tarehe 27 Mei) kwamba vikosi vya usalama vitaanza kampeni ya kuwanyang'anya silaha kwa nguvu, kiliripoti kituo cha Capital FM cha Kenya.
Wakaazi wa Mandera walitakiwa kusalimisha silaha zao kwa serikali mwezi huu au kunyang'anywa kwa nguvu. Hadi sasa polisi wamepokea silaha 12 tu, licha ya kuongezwa kwa muda wa mwisho.
"Tunachosisitiza ni kwamba wakaazi wote lazima wasalimishe silaha zao. Sote tumekubaliana na viongozi kutoka maeneo haya kwamba wakishindwa kufanya hivyo, tutawanyang'anya kwa lazima," alisema Kimaiyo baada ya mkutano na viongozi kutoka Wajir, Mandera na Garissa. "Ili maendeleo yapatikane kwenye maeneo haya, lazima usalama uwepo. Tunawatolea wito wakaazi kutupa taarifa ambazo zinaweza kusaidia kudhibiti uhalifu."

No comments:

Post a Comment