Baada ya kuwaomba wakaazi wa Mandera kusalimisha silaha zao, Inspekta
 Jenreali wa Polisi, David Kimaiyo, alitangaza siku ya Jumatatu (tarehe 
27 Mei) kwamba vikosi vya usalama vitaanza kampeni ya kuwanyang'anya 
silaha kwa nguvu, kiliripoti kituo cha Capital FM cha Kenya.
Wakaazi wa Mandera walitakiwa kusalimisha silaha zao kwa serikali mwezi huu au kunyang'anywa kwa nguvu. Hadi sasa polisi wamepokea silaha 12 tu, licha ya kuongezwa kwa muda wa mwisho.
"Tunachosisitiza ni kwamba wakaazi wote lazima wasalimishe silaha 
zao. Sote tumekubaliana na viongozi kutoka maeneo haya kwamba 
wakishindwa kufanya hivyo, tutawanyang'anya kwa lazima," alisema Kimaiyo
 baada ya mkutano na viongozi kutoka Wajir, Mandera na Garissa. "Ili 
maendeleo yapatikane kwenye maeneo haya, lazima usalama uwepo. 
Tunawatolea wito wakaazi kutupa taarifa ambazo zinaweza kusaidia 
kudhibiti uhalifu."
 
No comments:
Post a Comment