Thursday, April 18, 2013

BREAKING NEWS: MILIONI 2 000,000 ZATOLEWA NA SERIKALI KUGHARAMIA MAZISHI YA BI KIDUDE

Mhe. rais wa zanzibar Dr Shein na viongozi wengine wakitoa heshima zao za mwisho mbele ya marehemu Bi Kidue kabla ya kuhifadhiwa kwenye jeneza.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika dua ya pamoja kumuombea Gwiji la sanaa Zanzibar Bi. Fatma Binti Baraka (Bi. Kidude) nyumbani kwake Rahaelo nyuma ya Studio ya ZBC Redio.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa pamoja na baadhi ya Familia ya Bi. Kidude wakati alipofika kutoa mkono wa pole kwa ndugu na jamaa wa msanii huyo. Kushoto kwa Balozi  ni Ndg. Haji Ramadhani Suwed na kulia ni Bw. Abdullrahman Saleh.
Umati mkubwa wa Wananchi walioshiriki mazishi ya Msanii Gwiji wa sanaa kanda ya Afrika Mashariki na Mipaka yake  Bi. Fatma Binti Baraka (Bi Kidude) nyumbani kwake Rahaleo nyuma ya Studio ya ZBC Redio.

No comments:

Post a Comment