Tuesday, May 14, 2013

Kenya kufufua askari wa akiba Garissa ili kupambana na al-Shabaab

Serikali ya Kenya inapanga kufufua askari wa akiba wa Kenya (KPR), programu ya kutoa mafunzo na kuwezesha vikosi vya raia, kusaidia kupambana na wanamgambo wa al-Shabaab kutoka ndani ya jamii huko Garissa.
  • Askari wa Kenya akiangalia mkutano wa hadhara wa chama cha Harakati za Demokrasia ya Njano huko Garissa tarehe 22 Februari. Askari polisi wa akiba ambao ni raia wenye silaha hivi karibuni watasaidia kulinda amani katika mji huo, wakilinda dhidi ya vitisho kutoka kwa al-Shabaab. [Will Boase/AFP]
Garissa imekuwa mahali pa mashambulio makubwa ya al-Shabaab nchini Kenya baada ya vikosi vya ulinzi vya Kenya kupeleka vikosi Somalia Oktoba 2011.
Iliongozwa na Inspekta Jenarali David Kimaiyo na Katibu Mkuu wa Usalama wa Ndani Mutea Iringo, Kamati ya Ushauri ya Taifa imekuwa ikichunguza mfululizo wa mashambulio kama hayo mwezi Aprili. Wakati wa mkutano wa tarehe 20 Aprili, kamati ilipendekeza kushirikisha raia katika mji wa Garissa kwa ajili ya operesheni za kigaidi.
KPR iliundwa mwaka 1948 kusaidia polisi kudumisha sheria na kanuni nchini Kenya kote.
Mwaka 2004, aliyekuwa kamishina wa polisi Meja Jenerali Mohammed Hussein Ali alivunja na kunyang'anya silaha KPR katika maeneo ya miji ya Kenya baada ya maofisa wake kuhusishwa na uhalifu wa kutumia nguvu na rushwa. Hata hivyo, aliendeleza jeshi hilo katika maeneo ya vijijini, kupambana na wizi wa ng'ombe na ujambazi.

Kufufua askari wa akiba wa Kenya

Raia katika KPR iliyofufuliwa watasaidia kulinda usalama katika vitongoji vya Garissa, Kamishina wa wilaya ya Garissa Maalim Mohammed aliiambia Sabahi. Watakuwa chini ya maofisa wanaosimamia askari kanzu wasio na sare wenye jukumu la kufichua shughuli za al-Shabaab zisizo na ujuzi kutoka katika maficho yao na kuzuia mashambulio ya kigaidi.
Kutoka vikosi vya raia vilipopewa silaha, Mohammed alisema serikali imekuwa ikichukua hatua kali kuepuka kutoa silaha kwa makosa kwa wahalifu.
"Tunapaswa kupata vitu mara tu tunapoanza ili tusiongeze silaha zaidi katika mzunguko, ambazo zitaongeza matatizo zaidi kwenye vitisho vilivyopo vya al-Shabaab," alisema.
"Kuna hitilafu kwenye kutoa silaha kwa raia, lakini kwa kunyoosha mambo kwa ufanisi na kuhakikisha kwamba silaha hazitolewi kwa wasiostahili, tunachagua watahiniwa kufanyiwa uchunguzi," Mohammed alisema.
Tunawaandikisha askari wale wanaofaulu uchunguzi wa awali ambao watapewa kozi ya mwezi mmoja kuhusu silaha za moto, mafunzo halisi, ukusanyaji wa taarifa kuhusu maadui na kukabili majanga ya msingi, alisema. Serikali kwa sasa inahakiki watahiniwa 100 kwa ajili ya kupewa nafasi katika kikosi cha maofisa wa akiba, ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara, wanawake na vijana.
Kwa mujibu wa mkuu wa polisi wa mkoa wa Kaskazini Mashariki Charlton Mureithi, viunga kumi ambavyo vilibainishwa kama vilikuwa vikiwahifadhi al-Shabaab vitakuwa na askari kumi wa akiba kila moja.
"Baada ya mafunzo yao maalumu, wataeneza katika viunga vya jirani, ambavyo wanavielewa vizuri, kuwafukuza magaidi na wale wote walio nyuma ya matukio ya upigaji risasi mjini," aliiambia Sabahi. "Hatuna tarehe maalumu watakapoenea, lakini tunatarajia kuwa itakuwa hivi karibuni kwa sababu ya vitisho vya muda mrefu."
Kuwahakikishia usalama polisi wa akiba, shughuli zao zitakuwa zikijulikana na viongozi wachache wa usalama. "Tunataka waongeze nguvu katika usalama wa mji bila kutambulika. Tunaamini watakuwa kiungo muhimu kati ya jamii na mamlaka hiyo," alisema Mureithi.
Zaidi ya kueneza jeshi la polisi wa akiba, mamlaka zitataka teksi zote zinazofanya kazi ndani na nje ya Garissa kuwa na namba za utambulisho zilizochorwa katika magari yao zikiwa kubwa na rahisi kusomeka, alisema Mureithi.
"Tumegundua kwamba teksi zimekuwa zikitumika kama njia ya kupitisha wahalifu, na ni vigumu kwa mashuhuda kushika namba kwa gari linalotembea," alisema.
Aidha, alisema magari yote yatazuiliwa kuwa na madirisha yenye vioo vya rangi ya giza.

Wananchi walisaidia jeshi kwa tahadhari

Sheikh Abdullahi Salat, mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu Kenya huko Garissa, alipongeza jitihada za usalama, lakini alitahadharisha kwamba serikali inapaswa kuwa makini kutoruhusu wanachama wa kitengo kipya kufanya mauaji mengine kwa jina la kukabiliana na ugaidi.
"Wananchi waliopata mafunzo wanapaswa kufikia viwango vya juu vya maadili ili kufanya operesheni zao ndani ya sheria zao za nchi," Salat aliiambia Sabahi. "Kama ikiwezekana, washukiwa wanapaswa kukabidhiwa kwa serikali kwa ajili ya hukumu ya kisheria kutawala."
Serikali inapaswa kuwajibika kama kikosi kitawadhuru watu wasiokuwa na hatia, alisema, akiongeza kwamba serikali inapaswa pia kufafanua jinsi inavyopendekeza kuwatuliza maofisa wa KPR mara vitisho vya ugaidi vitakapoondoshwa.
John Chege, anayemiliki Hoteli ya Holiday Inn huko Garissa, eneo ambalo lilitokea ghasia za mauaji mwezi uliopita, alisema alipenda kikosi kisambazwe haraka iwezekanavyo kusaidia jumuiya ya wafanyabiashara.
Wafanyabiashara wengi wanakimbia Garissa kwa sababu mashambulio ya mara kwa mara yameharibu biashara, aliiambia Sabahi. Kwa hiyo, serikali inapaswa kujaribu kila linalowezekana kurejesha ujasiri wa wafanyabiashara na kueneza kukua kwa uchumi, alisema.

No comments:

Post a Comment