Thursday, July 25, 2013

Njama ya uasi yatibuka Ivory Coast


Gereza la Maca ambako wahalifu sugu wanafungwa
Njama ya uasi pamoja na jaribio la wafungwa kutoroka jela kubwa zaidi nchini Ivory Coast imetibuka na kusababisha vifo vya wafungwa wawili.
Polisi walilazimika kurusha gesi ya kutoa machozi pamoja na kufyatua risasi ili kutuliza hali katika gereza la Maca mjini Abidjan.
Maafisa wanasema kuwa walinzi wawili wa magereza walijeruhiwa vibaya.
Purukushani lilizuka Jumanne jioni wakati wafungwa kadhaa walipovunja milango ya magereza yao na kuwaachilia huru baadhi ya wafungwa.
Gereza hilo huwahifadhi wahalifu sugu na baadhi ya maafisa kutoka kwa iliyokuwa serikali ya rais wa zamani Laurent Gbagbo.

No comments:

Post a Comment