Wednesday, July 31, 2013

Mgomo wa wanafunzi wa sekondari ya Lutheran Junior seminari umeingia siku ya 2.




Mgomo wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lutheran junior Seminary inayomilikiwa na kanisa la kilutheri Tanzania umeingia siku ya pili baada ya wanafunzi  kugoma kutwa nzima kuingia madarasani na kuandamana katika barabara ya Morogoro Dar es Salaam na kulazimu jeshi la polisi kuingilia kati kuzuia maandamano.
 Wanafunzi hao wamesikika wakiimba wanataka kuonana na askofu mkuu wa KKKT Alex Malasusa huku wakiwa na mabango yenye jumbe mbalimbali ambapo wakiwa njiani katika barabara ya Morogoro Dar es Salaam jeshi la polisi walisitisha maandamano kwa madai ya kutofuata taratibu za kuomba kibali.
Wanafunzi hao walilazimika kurudi shuleni kwa maandamano wakisindikizwa na ulinzi wa jeshi la polisi lakini walipofika shuleni hapo mambo yalionekana kuwa magumu zaidi hata hivyo hawakutaka kusikiliza walimu na ikamlazimu mkuu wa wilaya Saidi Amanzi kufika shuelni hapo na kuzungumza na uongozi ni wa shule ambapo amesema inawalazimu kusubiri viongozi wa KKKT kutoka makao mjini Arusha .
Kwa upande wao wanafunzi wamesema wataendelea na mgomo huo kutokana na ahadi zilizotolewa kushindwa kutekelezeka na kushinikiza kutaka kuonana na askofu mkuu Alex Malalasusa ili awasaidie kutatua kero zao.

No comments:

Post a Comment