Saturday, May 11, 2013

Pakistan yapiga kura kati ya ghasia

 11 Mei, 2013 - Saa 10:21 GMT

Wananchi wa Pakistan wanapiga kura kwenye uchaguzi mkuu baada ya kampeni zilizokuwa za fujo.
Wanawake wamepanga foleni kusubiri kupiga kura mjini Lahore
Na mauaji yameendelea siku ya upigaji kura; polisi mjini Karachi wanasema watu 11 wamekufa na zaidi ya 50 kujeruhiwa pale bomu liliporipuka nje ya ofisi ya chama cha Awami.
Na watu zaidi wamejeruhiwa kwenye shambulio katika mji wa Peshawar.
Lakini mwandishi wa BBC katika mji mkuu, Islamabad, anasema wapigaji kura wengi wamejitokeza na kukaidi vitisho vya Taliban kwamba watafanya fujo zaidi.
Vyama vinavyoongoza katika uchaguzi huo ni Pakistan Muslim League - cha waziri mkuu wa zamani, Nawaz Sharif - na Movement for Justice cha mcheza kriketi wa zamani, Imran Khan.

No comments:

Post a Comment