Thursday, April 25, 2013

Maelfu ya watoto kuchanjwa Somalia


Somalia ina idadi kubwa ya vifo vya watoto duniani
Mpango wa kutoa chanjo kwa zaidi ya watoto milioni moja nukta tatu umezinduliwa nchini Somalia.
Chanjo hiyo itakuwa ya kukinga watoto dhidi ya aina tano ya magonjwa ikiwemo Homa ya mapafu, Hepatitis na ugonjwa wa uti wa mgongo.
Shirika la afya duniani ndilo linatoa chanjo hizo kwa ushirikiano na shirika la kuwahudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF.
Somalia ni moja ya nchi zenye mpango duni wa kutoa chanjo kwa watoto pamoja na kuwa nchi yenye idadi kubwa ya vifo vya watoto duniani.
Wataalamu wansema kuwa mmoja kati ya watoto watano, hufariki kabla ya kufikisha miaka mitano hali inayotokana na mfumo mbaya wa afya ambao umezoroteshwa na otovu wa usalama.

No comments:

Post a Comment