Saturday, August 3, 2013

Rais Kikwete amvaa Kagame, amshangaa kwa lugha za matusi na kejeli

???????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????
Na Fidelis Butahe, Mwananchi
Dar es Salaam: Kwa mara ya kwanza Rais Jakaya Kikwete amemtolea uvivu Rais wa Rwanda, Paul Kagame kutokana na kitendo chake cha kumtolea lugha za matusi baada ya kumshauri kukaa meza moja na vikundi vya waasi wa nchi yake (FDLR), huku akimtaka kuacha kukuza mgogoro usiokuwepo.
Rais Kikwete alitoa ushauri huo kwa Rwanda takribani miezi miwili iliyopita wakati akizungumza katika kikao cha Mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika mapema mwaka huu, mjini Addis Ababa, Ethiopia, ambao ulikuwa ukijadili suala la amani ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) pamoja na Ukanda wa Maziwa Makuu.
Ushauri huo pia uliwagusa Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Joseph Kabila (DRC), ambao aliwataka kufanya mazungumzo na waasi wanaopingana na Serikali zao. Akizungumza katika hotuba yake ya kila mwezi Rais Kikwete alisema: “Ushauri ule niliutoa kwa nia njema kabisa, kwani bado naamini kuwa kama jambo linaweza kumalizwa kwa njia ya mazungumzo njia hiyo ni vyema itumike,”
“Isitoshe, ushauri ule niliutoa pia kwa Serikali ya Congo , Serikali ya Uganda. Katika mkutano ule Rais Museveni wa Uganda aliunga mkono kauli yangu. Rais Kagame hakusema chochote pale mkutanoni. Baada ya kurudi nyumbani ndipo tukaanza kuyasikia maneno tuliyoyasikia na tunayoendelea kuyasikia.”
Alisisitiza, “Kwa upande wangu sijasema lolote kuhusu Rwanda pamoja na maneno mengi ya matusi na kejeli yanayotoka kwenye vinywa vya viongozi wa Rwanda dhidi yangu. Siyo kwamba siambiwi yanayosemwa au sijui kusema au sina la kusema, la hasha, sijafanya hivyo kwa sababu sioni faida yake.”
Rais Kagame alitoa lugha zisizostahili dhidi ya Rais Kikwete katika sherehe ya kuhitimu mafunzo ya kijeshi ya maofisa 45 wa jeshi lake Julai mwaka huu, ambapo alisema ushauri wa kufanya mazungumzo na waasi wa FDLR ni ujinga na haupo katika historia ya Wanyarwanda.
“Nilinyamaza kimya kwa sababu sikupenda kusikiliza ushauri kuhusu FDLR, kwa sababu nafikiri ni upuuzi ulioambatana na ujinga. Hatuwezi kuacha maisha yetu kama Wanyarwanda tunavyoishi sasa. Ushauri wa Kikwete ni sawa na kucheza na makaburi ya watu wengi ambao ni ndugu zetu,” alisema Kagame.
Katika hotuba ya jana Rais Kikwete alisema uhusiano wa Tanzania na Rwanda unapitia katika wakati mgumu na mtikisiko, baada ya yeye kutoa ushauri kwa Serikali ya Rwanda kuzungumza na mahasimu wao na kwamba hilo linadhihirika katika kauli zinazotolewa na viongozi wa Rwanda.
“Napenda kuwahakikishia Watanzania wenzangu na ndugu zetu wa Rwanda kuwa mimi, Serikali ninayoiongoza na wananchi wa Tanzania ,tunapenda kuwa na uhusiano mzuri na ushirikiano wa karibu na Rwanda kama ilivyo kwa nchi zote jirani” alisema Rais Kikwete.
Alisema nchi hizo ni jirani na kila moja inamuhitaji mwenzake, hivyo lazima ziwe na uhusiano mwema na ushirikiano mzuri.
“Nasisitiza kuwa mimi na Serikali ninayoiongoza tutakuwa wa mwisho kufanya kitendo au vitendo vibaya dhidi ya Rwanda au nchi yoyote jirani au yoyote duniani. Hatuna sababu ya kufanya hivyo, kwani ni mambo ambayo hayana tija wala masilahi kwetu” alisema.
Alisema nchi hizo mbili zimekuwa zikijihusisha na mambo ya kukuza na kujenga ujirani mwema, kusisitiza kwamba hiyo ni moja ya nguzo kuu ya Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania.
“Nawahakikishia ndugu zetu wa Rwanda kuwa kwa upande wetu hakuna kilichobadilika wala kupungua katika uhusiano na ushirikiano wetu,” alisema na kuongeza;
“Kwangu sioni kama kuna mgogoro wa aina yoyote. Busara inatuelekeza kuwa tusikuze mgogoro usiokuwepo ‘Two wrongs do not make a right’ (makosa mawili hayawezi kutengeneza usahihi). Tunashirikiana na kusaidiana kwa mambo mengi baina ya nchi zetu kitaifa na katika kanda yetu ya Afrika Mashariki na Nchi za Maziwa Makuu, katika Umoja wa Afrika na hata kimataifa.”
Alifafanua kuwa alitoa ushauri huo kwa kuzingatia mila na desturi za miaka mingi katika ukanda wa Afrika Mashariki.
“Tumekuwa tunakutana katika mikutano na vikao mbalimbali tunazungumza na kushauriana kwa uwazi juu ya njia za kushughulikia matatizo na masuala mbalimbali kila yanapotokea,” alisema Rais Kikwete.
Alisema wakati wote matatizo yanazozikabili nchi za Afrika viongozi wote huyachukulia kama mambo yanayowahusu na kupeana ushauri, jambo ambalo alisisitiza kuwa ni wajibu kwa viongozi.
“Iweje leo mtu kutoa ushauri ule ionekane jambo baya na la ajabu. Jambo la kushutumiwa na kutukanwa, siyo sawa hata kidogo, Ushauri si shuruti, ushauri si amri. Una hiyari ya kuukubali au kuukataa” alisema Rais Kikwete na kuongeza;
“Muungwana hujibu, “Siuafiki ushauri wako”. Hakuna haja ya kutukana wala kusema maneno yasiyostahili wala kusema yasiyokuwepo na ya uongo.”
Rais Kikwete alisema Serikali ya Tanzania haina ugomvi wala nia mbaya na Rwanda na inapenda kuendelea na uhusiano mzuri na nchi hiyo.
“Labda wenzetu wanalo lao jambo dhidi yetu ambalo sisi hatulijui. Sisi tunasikia mengi yanayozungumzwa na kudaiwa kupangwa kufanywa na Rwanda dhidi yangu na nchi yetu. Hatupendi kuyaamini moja kwa moja tunayoyasikia lakini hatuyapuuzi” alisema.
Ushauri wa Rais Kikwete kwa Rwanda pia uliungwa mkono na Rais wa Marekani, Barack Obama wakati wa ziara yake nchini Tanzania, alipoitaka nchi hiyo kumaliza mgogoro wake na waasi kwa njia ya mazungumzo.
Katika hotuba hiyo, Rais Kikwete alizungumzia jinsi nchi ilivyonufaika na ziara ya Rais wa Marekani, Barack Obama, Rais mstaafu wa nchi hiyo, George W. Bush, Waziri Mkuu wa Thailand, Yingluck Shinawatra.
Photo: Rais Kikwete amvaa Kagame, amshangaa kwa lugha za matusi na kejeli Na Fidelis Butahe, Mwananchi Dar es Salaam: Kwa mara ya kwanza Rais Jakaya Kikwete amemtolea uvivu Rais wa Rwanda, Paul Kagame kutokana na kitendo chake cha kumtolea lugha za matusi baada ya kumshauri kukaa meza moja na vikundi vya waasi wa nchi yake (FDLR), huku akimtaka kuacha kukuza mgogoro usiokuwepo. Rais Kikwete alitoa ushauri huo kwa Rwanda takribani miezi miwili iliyopita wakati akizungumza katika kikao cha Mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika mapema mwaka huu, mjini Addis Ababa, Ethiopia, ambao ulikuwa ukijadili suala la amani ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) pamoja na Ukanda wa Maziwa Makuu. Ushauri huo pia uliwagusa Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Joseph Kabila (DRC), ambao aliwataka kufanya mazungumzo na waasi wanaopingana na Serikali zao. Akizungumza katika hotuba yake ya kila mwezi Rais Kikwete alisema: “Ushauri ule niliutoa kwa nia njema kabisa, kwani bado naamini kuwa kama jambo linaweza kumalizwa kwa njia ya mazungumzo njia hiyo ni vyema itumike,” “Isitoshe, ushauri ule niliutoa pia kwa Serikali ya Congo , Serikali ya Uganda. Katika mkutano ule Rais Museveni wa Uganda aliunga mkono kauli yangu. Rais Kagame hakusema chochote pale mkutanoni. Baada ya kurudi nyumbani ndipo tukaanza kuyasikia maneno tuliyoyasikia na tunayoendelea kuyasikia.” Alisisitiza, “Kwa upande wangu sijasema lolote kuhusu Rwanda pamoja na maneno mengi ya matusi na kejeli yanayotoka kwenye vinywa vya viongozi wa Rwanda dhidi yangu. Siyo kwamba siambiwi yanayosemwa au sijui kusema au sina la kusema, la hasha, sijafanya hivyo kwa sababu sioni faida yake.” Rais Kagame alitoa lugha zisizostahili dhidi ya Rais Kikwete katika sherehe ya kuhitimu mafunzo ya kijeshi ya maofisa 45 wa jeshi lake Julai mwaka huu, ambapo alisema ushauri wa kufanya mazungumzo na waasi wa FDLR ni ujinga na haupo katika historia ya Wanyarwanda. “Nilinyamaza kimya kwa sababu sikupenda kusikiliza ushauri kuhusu FDLR, kwa sababu nafikiri ni upuuzi ulioambatana na ujinga. Hatuwezi kuacha maisha yetu kama Wanyarwanda tunavyoishi sasa. Ushauri wa Kikwete ni sawa na kucheza na makaburi ya watu wengi ambao ni ndugu zetu,” alisema Kagame. Katika hotuba ya jana Rais Kikwete alisema uhusiano wa Tanzania na Rwanda unapitia katika wakati mgumu na mtikisiko, baada ya yeye kutoa ushauri kwa Serikali ya Rwanda kuzungumza na mahasimu wao na kwamba hilo linadhihirika katika kauli zinazotolewa na viongozi wa Rwanda. “Napenda kuwahakikishia Watanzania wenzangu na ndugu zetu wa Rwanda kuwa mimi, Serikali ninayoiongoza na wananchi wa Tanzania ,tunapenda kuwa na uhusiano mzuri na ushirikiano wa karibu na Rwanda kama ilivyo kwa nchi zote jirani” alisema Rais Kikwete. Alisema nchi hizo ni jirani na kila moja inamuhitaji mwenzake, hivyo lazima ziwe na uhusiano mwema na ushirikiano mzuri. “Nasisitiza kuwa mimi na Serikali ninayoiongoza tutakuwa wa mwisho kufanya kitendo au vitendo vibaya dhidi ya Rwanda au nchi yoyote jirani au yoyote duniani. Hatuna sababu ya kufanya hivyo, kwani ni mambo ambayo hayana tija wala masilahi kwetu” alisema. Alisema nchi hizo mbili zimekuwa zikijihusisha na mambo ya kukuza na kujenga ujirani mwema, kusisitiza kwamba hiyo ni moja ya nguzo kuu ya Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania. “Nawahakikishia ndugu zetu wa Rwanda kuwa kwa upande wetu hakuna kilichobadilika wala kupungua katika uhusiano na ushirikiano wetu,” alisema na kuongeza; “Kwangu sioni kama kuna mgogoro wa aina yoyote. Busara inatuelekeza kuwa tusikuze mgogoro usiokuwepo ‘Two wrongs do not make a right’ (makosa mawili hayawezi kutengeneza usahihi). Tunashirikiana na kusaidiana kwa mambo mengi baina ya nchi zetu kitaifa na katika kanda yetu ya Afrika Mashariki na Nchi za Maziwa Makuu, katika Umoja wa Afrika na hata kimataifa.” Alifafanua kuwa alitoa ushauri huo kwa kuzingatia mila na desturi za miaka mingi katika ukanda wa Afrika Mashariki. “Tumekuwa tunakutana katika mikutano na vikao mbalimbali tunazungumza na kushauriana kwa uwazi juu ya njia za kushughulikia matatizo na masuala mbalimbali kila yanapotokea,” alisema Rais Kikwete. Alisema wakati wote matatizo yanazozikabili nchi za Afrika viongozi wote huyachukulia kama mambo yanayowahusu na kupeana ushauri, jambo ambalo alisisitiza kuwa ni wajibu kwa viongozi. “Iweje leo mtu kutoa ushauri ule ionekane jambo baya na la ajabu. Jambo la kushutumiwa na kutukanwa, siyo sawa hata kidogo, Ushauri si shuruti, ushauri si amri. Una hiyari ya kuukubali au kuukataa” alisema Rais Kikwete na kuongeza; “Muungwana hujibu, “Siuafiki ushauri wako”. Hakuna haja ya kutukana wala kusema maneno yasiyostahili wala kusema yasiyokuwepo na ya uongo.” Rais Kikwete alisema Serikali ya Tanzania haina ugomvi wala nia mbaya na Rwanda na inapenda kuendelea na uhusiano mzuri na nchi hiyo. “Labda wenzetu wanalo lao jambo dhidi yetu ambalo sisi hatulijui. Sisi tunasikia mengi yanayozungumzwa na kudaiwa kupangwa kufanywa na Rwanda dhidi yangu na nchi yetu. Hatupendi kuyaamini moja kwa moja tunayoyasikia lakini hatuyapuuzi” alisema. Ushauri wa Rais Kikwete kwa Rwanda pia uliungwa mkono na Rais wa Marekani, Barack Obama wakati wa ziara yake nchini Tanzania, alipoitaka nchi hiyo kumaliza mgogoro wake na waasi kwa njia ya mazungumzo. Katika hotuba hiyo, Rais Kikwete alizungumzia jinsi nchi ilivyonufaika na ziara ya Rais wa Marekani, Barack Obama, Rais mstaafu wa nchi hiyo, George W. Bush, Waziri Mkuu wa Thailand, Yingluck Shinawatra.

Dhana ya utawala bora ilipokosa meno


Jengo-la-uwanja-wa-ndege

Na A K Simai
Niliwahi kuandika takriban mwaka mmoja uliopita kwamba kulikuwa na matatizo katika ujenzi wa jengo jipya la uwanja wa ndege katika makala yangu ‘Jengo jipya la uwanja wa ndege kunaini?’
Hivi karibuni kupitia kwa Waziri mwenye dhamana ya Mawasiliano na Miundo mbinu alisema katika baraza la wawakilishi wakati akiwasilisha bajeti ya makadirio na mapato ya wizara yake na nanukuu:
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetoa ruhusa ya kuendelea kwa ujenzi wa Jengo jipya la Abiria katika Uwanja wa ndege wa Zanzibar lililosita kwa muda baada ya kuonekana kasoro za kiufundi zilizojitokeza hapo awali katika jengo hilo.
Amesema katika kutekeleza hilo ujenzi huo umeanza mara baada kukamilika kwa taratibu za Michoro mipya kwa baadhi ya sehemu za jengo baada ya kupata Mshauri elekezi kutoka Nchini Ufaransa.
“Mnamo mwezi wa Machi mwaka huu tulimpata mshauri elekezi na kuanza kazi mwezi April na kutoa ripoti yake mwezi Juni mwaka huu ambavyo ilionesha namna ya kasoro zilivyojitokeza na kuweza kutatuliwa haraka ipasavyo .”alisema Waziri Rashid Seif.
Nikiwa kama mwananchi na mkereketwa nimebakia tena na masuali yangu yale yale niliyoyaanika mwaka mmoja uliopita na si vibaya kama nitayakariri kwani maelezo ya Waziri hayajanipatia majibu ya kuridhisha.
Pia sikusikia waheshimiwa wawakilishi wakitishia angalau kuzuia shilingi katika bajeti hii mpaka wapate maelezo hatua gani zilichukuliwa dhidi ya watendaji waliopelekea dosari hizi kutokea.
1. Ni timu gani iliyokuwemo katika kuandaa plan ya jengo hili ni watu waliokuwa na uzoefu kwenye aviation au ni watu wa kuokoteza tu?
2. Hakukuwa na consultancy wakati wa kuandaa plan yenyewe na hakukuwa na kureview kuangalia kama kila kinachohitajika katika Airport ya kile kimewekwa?
3. Tulikurupuka katika kuingia mkataba huu ambao kwa sasa utaweza kutuingiza kwenye janga zito la deni lenye kuongezeka kwa riba pamoja na kuongezeka kwa gharama?
4. Kutakuwa na hatua zozote za kinidhamu au kuwajibika kwa waliotuingiza katika balaa hili au kulikuwa na mazingira ya ten percent?
Jengo lilisimamishwa mwezi July mwaka 2012 na tokea wakati huo Serikali ilikuwa ikihangaika kupata mshauri mwelekezi na katika hatua hii iliwachukua miezi 9 kumpata mshauri mwelekezi mwenye uweledi wa aina za kazi hizi. Well done Waziri kwa kulitatua hili haraka ipasavyo.
Maelezo ya Waziri hayaoneshi katika sehemu yoyote kwamba Serikali itawachukulia hatua za kinidhamu au kuwawajibisha wale wote ambao walihusika kwa njia moja au nyengine katika kuitia hasara kubwa Serikali hii na kuiongezea deni maradufu kwa kuombwa mkopo wa ziada zaidi ya ule wa wa US$ 70.4 milioni kutoka Exim Bank ya China.
Sijui interest rate yake ni kiasi gani ila kulilipa hili itakuwa shughuli pevu kwani nilitarajia mhe Waziri angalau angelitutajia ziada iliyoombwa kwenye mkopo huu ili nasi walipa kodi tuanze kujiandaa.
Serikali haioni haja ya kuwawajibisha watendaji waliomtia aibu hata Rais wetu wakati alipokuwa akikaguwa jengo hilo mwaka 2012 na kumhakikishia kwamba litakamilka katika muda wake uliopangwa.
Dhana ya utawala bora inayosimamiwa na serikali haionekani kutekelezeka kwa vitendo bali imebaki katika miongozo na kwenye semina elekezi tu?.
Mojawapo ya mipangilio ya utawala bora ni sera ya uwajibikaji kutekelezwa kikamilifu kwa kila aliyekwenda kinyume na malengo au maafikiano na dhamana alizokabidhiwa bila ya kuoneana muhali au kuchukuliana baada ya kuthibitika kwamba ni kweli uzembe ulikuwa umetendeka.
Tunataka ushahidi gani tena katika suala hili kama kulikuwa na uzembe?

'Uchaguzi Zimbabwe ulikuwa huru'Obasanjo


Masanduku ya kupigia kura
Mkuu wa ujumbe wa uangalizi kutoka Muungano wa Afrika nchini Zimbabwe, Olusegun Obasanjo amesema uchaguzi mkuu wa hapo Jumatano ulikua huru na haki. Matokeo ya awali yanaoyesha Rais Robert Mugabe na chama tawala cha Zanu PF wakiongoza kwa kura nyingi
Chama hicho tayari kimedai ushindi. Msemaji wa chama hicho Rugare Gumbo alisema chama hicho kilitarajiwa kushinda kiasi ya asilimia 70 ya kura hizo.
Lakini mpinzani wa Mugabe, Morgan Tsvangirai, amesema uchaguzi huo ni wa uongo na kusema udanganyifu uliofanyika una maana uchaguzi huo haukubaliki.
Waangalizi kutoka Umoja wa Afrika na jumuia ya maendeleo kusini mwa Afrika wanatarajiwa kutoa tamko rasmi hii leo kuhusu uchaguzi huo.
Bw. Obasanjo amesema kulikua na visa kadhaa wakati wa shughuli ya kupiga kura. Hata hivyo amesema visa hivyo haviwezi kutajwa kuwa na uzito wa kubatilisha au kufuta matokeo ya kura.
Msimamo wa Muungano wa Afrika unatofautiana na ule wa kundi la uangalizi la Zimbabwe Election Support Network.
Kundi hilo ambalo ndilo kubwa zaidi linalochunguza kura ya Zimbabwe limekashifu uchaguzi mkuu na kusema ulikuwa na dosari nyingi. Hii ni kwa sababu watu milioni moja walizuiwa kupiga kura.
Huku upande wa Rais Mugabe ulitangaza kushinda uchaguzi na Morgan Tsvangirai akipinga ni dhahiri kwamba Zimbabwe ingali na mgawanyiko mkubwa wa kisiasa..

Thursday, August 1, 2013

Uruguay kuhalalisha utumizi wa Bangi


Bangi
Bunge la Uruguay limepitisha mswada wa kuhalalisha bangi. Ikiwa mswada huu utapitishwa na Baraza la Senate, Uruguay itakuwa nchi ya kwanza kuhalalisha uzalishaji na utumiaji wa bangi.
Hatua hii inaungwa mkono na serikali ikisema itapunguza mapato na faida kubwa kwa walanguzi wa mihadarati pamoja na kuwafanya watumizi wa bangi kutotumia dawa kali za kulevya.Chini ya mswada huo ni serikali pekee itakua na kibali cha kuuza bangi.
Pia serikali itatoa utaratibu wa uzalishaji, mavuno, uhifadhi na mauazo ya nje. Wanunuzi wote watanakiliwa kwenye daftari maalum na sharti wawe wametimiza miaka 18 na zaidi. Mteja anaweza tu kununua kilo 40 kwa mwezi kutoka kwa maduka ya dawa au kukuza mimea sita ya bangi.Wageni hawatakubaliwa kununua bidhaa hii.
Wabunge 50 kati ya 96 walipitisha mswada huo. Wanaotetea kuhalalishwa kwa bangi wamesema vita dhidi ya mihadarati havijapiga hatua na ipo haja kuweka mbinu mpya.
Kwa miongo mingi kanda ya Latin America imekumbwa na ghasia za magenge ya mihadarati ambapo maelfu ya watu wamekufa. Matukio ya Uruguay yanatazamwa kwa karibu eneo hilo ikiwa yatasaidia kupunguza machafuko yanayotishia uthabiti wa mataifa mengi.

Uchaguzi 'Kichekesho Kikubwa'


 
Morgan Tchangirai
Waziri Mkuu Zimbabwe Morgan Tchangirai adai uchaguzi ni kichekesho kikubwa
Uchaguzi wa Rais nchini Zimbabwe ulikuwa ‘kichekesho kikubwa,’ Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai amesema, akituhumu udanganyifu wa kura uliofanywa na kambi ya mpinzani wake Rais Robert Mugabe.
Katika mkutano na waandishi wa habari, Bw Tsvangirai alisema uupigaji kura wa Jumatano ulikuwa ‘upuuzi na si halali’.
Kundi kubwa la waangalizi mapema lilisema kufikia hadi watu milioni moja walizuiwa kupiga kura.
Chama cha Bw Mugabe ambacho kinadai kushinda, kimekanusha tuhuma hizo kikisema upigaji kura ulikuwa shwari.
Kiongozi wa ujumbe wa Umoja wa Afrika, Rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo, alisemsa kwenye tathimini yao ya awali kuwa upigaji kura ulikuwa huru na haki.
Makundi mengine ya waangalizi yalisifia hali ya amani katika uchaguzi huo.
Kuhesabu kura ulianza kulianza usiku na Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe (ZEC) ina siku tano za kutangaza nani mshindi katika uchaguzi huo.
Tayari polisi wameonya kuwa watachukua hatua dhidi ya yeyote atakayejaribu kuvujisha habari za matokeo. Ni kinyume cha sheria kutangaza matokeo yasiyo rasmi.
Vikosi vya ziada baadhi vikiwa na vifaa vya kupambana na waandamanaji tayari viko mjini Harare.
Hatua za kisheria huenda zikafuata sasa, kwa mujibu wa mwandishi wa BBC Andrew Harding akiripoti kutoka Johannesburg.
Lakini megi yatategemea iwapo majirani wa Zimbabwe watapitisha uchaguzi huo, mwandishi wa BBC anaongezi.

'Uchaguzi umekumbwa na kasoro kubwa'

Akizungumza kwenye makao makuu ya chama chake cha Movement for Democratic Change (MDC) mjini Harare, Bw Tsvangirai alisema: "Hitimisho letu ni kuwa uchaguzi huu ni kichekesho kikubwa.’
"Uhalali wa uchgauzi huu umeharibiwa na ukiukwaji wa sheria na shughuli za kiutawala ambazo zimeathiri matokeo yake.”
"Ni utani ambao hauonyeshi matakwa ya watu."
Bw Tsvangirai alizungumza muda mfupi baada ya mtandao wa waangalizi (Zimbabwe Election Support Network-ZESN) kusema kuwa uchaguzi huo ‘umekumbwa na kasoro kubwa".
Katika taarifa yake rasmi ZESN limesema wapiga kura muhimu kufikia asilimia 82 walizuiwa katika vituo vya kupigia kura maeneo ya mijini ambako ni ngome ya Bw Tsvangirai.
Katika maeneo ya vijijini am, ambako ni ngome ya Rais Mugabe ni asilimia 38, kundi hilo limeongeza.
Jumatano wanavijiji, mawakala wa MDC kwenye vituo vya kupigia kura na ZESN walisema kumekuwa na kasoro kadhaa katika baadhi ya maeneo ya jimbo la Masvingo.
Walisema viongozi wa jadi na wakuu wa vijiji waliwapanga watu kwenye mistari na kuwalazimisha kutembea kuelekea vituo vya kupigia kura na kuwapa namba za kupigia kura kama vile kuwahakiki wamempigia kura nani.
Wanatuhumu kuwa kwenye maeneo haya baadhi ya watu wasomi walilazimishwa kujifanya hawajui kusoma na kuandika na wakasaidiwa kupiga kura ambazo zilikuwa ni kwa Zanu-PF.
Msemaji wa Zanu-PF Mtaalam wa Saikolojia Maziwisa alikanusha kuwa wapiga kura wengi wamezuiwa makusudi kujiandikisha.
Amekiri kuwa kulikuwa na kasoro kadhaa lakini akafafanua kuwa vyama vyote vimeathirika.
"Ni muhimu kumbuka kuwa hiyo kwa sehemu ilisababishwa na ukweli kuwa baadhi ya vifaa muhimu Waziri wa Fedha Tendai Biti, anayetoka chama cha MDC alikuwa," Bw Maziwisa aliiambia BBC.
"Ukiaangalia hali ya Zimbabwe utakuwa na hitimisho m
oja tu. Na hii ni juu ya zaidi ya miaka mine iliyopita tumefanya jitihada za kutosha kufanya mazingira ya Zimbabwe yawe mazuri inavyowezekana ili uchaguzi uwe huru na hali.."

Wednesday, July 31, 2013

Vifo kutokana na HIV vyapungua Afrika


UNAIDS inasema kuwa vifo vinavyotokana na 
HIV vimepungua Afrika kwa asilimia 40
Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba Afrika imepiga hatua kubwa katika vita dhidi ya maambukizi ya Ukimwi.
Vifo vinavyotokana na maradhi ya Ukimwi Mashariki na Kusini mwa Afrika vimepungua kwa asili mia 40.
Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na ukimwi- UNAIDS umehusisha hatua za sasa na kutolewa kwa dawa za kukabiliana na makali ya Ukimwi.
Umoja wa Mataifa umesema mataifa ya Botswana, Ethiopia, Kenya, Zambia na Zimbabwe yamepunguza idadi ya watu wanaokufa kwa ukimwi kwa zaidi ya nusu.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa Maradhi nyemelezi ya kifua kikuu pia yamepungua sana tangu mwaka 2005.

Mohammed Morsi yuko salama' Ashton

Ashton alikutana na Morsi ingawa anasema hajui aliko
Mwakilishi wa mambo ya nje katika Muungano wa Ulaya Catherine Ashton amekutana na Rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri Mohammed Morsi katika eneo lisilojulikana. Morsi amekuwa akizuiliwa na jeshi tangu kuondolewa madarakani mapema mwezi huu.
Ashton amewaambia waandishi wa habari mjini Cairo kwamba Bw. Morsi alikua salama na kwamba alikubaliwa kutazama habari kwenye runinga na kusoma gazeti.
Alisema walijadili haja ya Misri kuganga yajayo na kuweka amani.Baroness Ashton amesema mchakato wa utawala mpya sharti ushirikishe pande zote
Msemaji wa Bi Catherene Ashton, alisema kuwa mkutano ulifanyika katika eneo lisilojulikana ambako Morsi anazuiliwa na kuwa ulidumu kwa masaa mawili.
Hakutoa maelezo kuhusu walichokijadili.
Hata hivyo tayari ameshakutana na maafisa kadhaa wa serikali akiwemo rais wa muda Adly Mansour, mkuu wa majeshi, Generali Abdel-Fattah al-Sisi na makamu wa rais wa maswala ya kigeni,Mohamed ElBaradei.
Alisema kuwa atatoa wito kwa pande zote mbili kushirikishwa katika serikali. Ziara ya Ashton ambayo ni ya pili nchini Misri inakuja baada ya wafuasi zaidi ya sabini wa Morsi kuuawa kwenye makabiliano na vikosi vya usalama nchini Misri.
Wafuasi wa kiongozi huyo wamesema kuwa wanapanga kufanya maandamano Jumanne huku serikali ya muda ikiwatahadharisha dhidi ya kuhusika na ghasia na kuwa watakaovunja sheria watachukuliwa hatua.
Maafisa wa usalama pia wametishia kuvunja maandamano ya wafuasi hao waliopiga kambi nje ya medani iliyo karibu na msikiti wa Rabaa al-Adawiya mjini Cairo.