Tuesday, May 28, 2013

Uingereza yaondolea Syria vikwazo

 28 Mei, 2013

Hali nchini Syria inaendelea kuwa mbaya kila kukicha
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza William Hague amesema kuwa vikwazo vya silaha ambavyo Muungano wa ulaya uliiwekea Syria vimeondolewa .
Akizungumza baada ya mkutano wa siku moja na mawaziri wengine wa mambo ya nje wa muungano wa Ulaya mjini Brassels, Bwana Hague alisema kuwa hakuna uamuzi wa moja kwa moja wa kutuma silaha kwa waasi wa Syria , na kwamba vikwazo vingine vitaendelea
Ni dhahiri kuwa uamuzi huo hautafanya mabadiliko makubwa mashinani kwa muda wa hivi karibuni. Hakuna hatua itakayochukuliwa hadi Agosti. Hapo ndipo Jumuiya ya Ulaya itakapochunguza upya hali ilivyo nchini Syria.
Inatarajiwa kuwa wakati huo Uingereza, Ufaransa na mataifa mengine yanayotaka kuchangia silaha kwa waasi wataruhusiwa kufanya hivyo.
Uamuzi huo utategemea mkutano mkubwa wa kibalozi utakaofanywa kati ya Marekani na Urusi mwezi ujao. Hata hivyo mkutano huo hauna uhakika wa kufanyika kwa sababu muungano wa makundi ya upinzani nchini Syria haujakubaliana kama wahudhurie au wasihudhuria mkutano huo licha ya utawala ya Rais Assad kusema kuwa unakubaliana na mkutano huo.
Mwandalizi mkuu wa mkutano huo, ambaye ni Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uingereza William Hague amesema kuwa tamko la Serikali ya Rais Assad kuwa huenda ukahudhuria mkutano huo ni la kutia moyo.
Ishara zote kutoka mashinani hadi sasa ni kuwa itachukua muda mrefu kabla ya wananchi wa kawaida kukubaliana na mapendekezo yanayotolewa na Jumuiya ya Ulaya.

Sudan yatisha kufungia Sudan.K mafuta

 28 Mei, 2013 

Rais Omar el Bashir
Rais wa Sudan Omar al-Bashir ametishia, kufunga kabisa bomba la mafuta ambalo husafirisha mafuta kutoka Sudan Kusini hadi pwani ya Sudan, Red Sea.
Alisema kuwa Sudan itasitisha usafirishwaji wa mafuta ikiwa Sudan Kusini haitakoma kuwaunga mkono waasi wanaoendesha harakati zao katika eneo la mafuta la Sudan.
Jeshi la Sudan linapambana na waasi katika angalao maeneo matatu ya nchi hiyo.
Licha ya Sudan Kusini kujitawala mwaka 2011, hali ya wasiwasi kuhusu mafuta na ardhi imekuwa ikiendelea.
''Na sasa natoa onyo la mwisho kwa ndugu zetu wa Sudan Kusini kuwa tutafunga kabisa bomba la mafuta ikiwa wataendelea kuunga mkono wasaliti katika jimbo la Darfur , Kordofan ya Kusini na Blue Nile'' alisema Bashir kupitia televisheni ya taifa huku akigusia waasi wanaoendesha harakati zao katika maeneo hayo.
Kundi la waasi lenye mirengo mingi, linalojulikana kama Sudan Revolutionary Front (SRF), limefanya mashambulizi katika miji kadhaa huku wakiteka mji mkubwa wa Um Rawaba , katikati mwa Sudan mwezi Aprili.
Kundi hilo linalonuia kuipindua serikali ya rais Bashir, lakini wakaendelea kudhibiti mji wa Abu Kershola, katika eneo jirani la Kordofan Kusini.
Waasi wa SPLM-North walijiunga na kundi la waasi la JEM kutoka Darfur pamoja na makundi mengine ambayo ni ya mrengo wa (SLA), kwa lengo la kubuni kundi la
Sudan Revolutionary Front mwaka jana.
Rais Bashir alitoa hotuba yake moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa nchini Sudan, kufuatia tangazo la jeshi kuwa limeweza kuteka tena mji wa Abu Kershola kutoka kwa waasi.
Wakati huohuo, msemaji wa waasi hao aliambia shirika la habari la AFP kuwa wapiganaji waliondoka kutoka, eneo la Abu Kershola ili kulegeza vikwazo vya serikali kwa wenyeji wa eneo hilo.
Uhusiano kati ya nchi hizo mbili umekuwa ukitetereka tangu mwaka 2011, wakati Sudan Kusini ilipoamua kujitawala.
Maswala muhimu kuhusu Uzalishaji wa mafuta, mizozo ya mipaka ynagali kutatuliwa.

Utapia mlo waathiri matokeo ya watoto shuleni

 28 Mei, 2013

Watoto wengi duniani wanakumbwa na tatizo la utapia mlo
Robo ya watoto wote duniani wako katika hatari ya kutofanya vyema shuleni kwa sababu ya viwango vya juu vya utapia mlo. Hii ni kwa mujibu wa shirika la kimataifa la misaada kwa watoto la Save the Children.
Watoto hao kwa kukosa lishe bora, uwezo wao wa kusoma na kuandika unaathirika sana.
Utafiti uliofanywa na shirika hilo uligundua kuwa watoto wenye utapia mlo hupata athari kubwa ambazo haziwezi kutibiwa , wao huwa wadogo na wasio na nguvu na hata ubongo wao haukomai vyema.
Shirika hilo linasema kuwa vingozi wa mataifa yaliyostawi kiviwanda yanapaswa kutoa kipaombele kwa tatizo la utapia mlo.
Watakutana Ireland ya Kaskazini mwezi ujao.
Ripoti hiyo,yenye mada 'Food for Thought' imetokana na utafiti uliofanyiwa maelfu ya watoto nchini, Ethiopia, India, Peru na Vietnam.
Utafiti huo unapendekeza kuwa watoto walio chini ya umri wa miaka minane, wanadumaa kutokana na utapia mlo, 19% ya watoto hao, wanaweza kwa urahisi kufanya makosa katika kuandika sentensi fupi, kama kama '' Jua ni kali'' au ''napenda Mbwa'' kuliko watoto wenye kupata lieshe bora.
"lishe mbovu kwa watoto linadunisha viwango vya uelewa katika nchi zinazostawi na pia ni kikwazo kikubwa katika kukabiliana na vifo vya watoto wachanga,'' alisema afisaa mkuu mtendaji wa shirika hilo.
Serikali ya Uingereza imeandaa mkutano mkubwa mjini London tarehe nane mwezi Juni, kabla ya mkutano wa G8 ambao unaratajaiwa kuangazia maswala kama uhaba wa chakula Afrika na haja ya nchi zinazostwi kuwa na mipangio yao ya lishe bora.

Je AU inahujumu mahakama ya ICC?

 28 Mei, 2013

Mwenyekiti wa tume ye Muungano wa Afrika Bi Nkosazana Dlamini Zuma
Baadhi ya Viongozi wa mataifa ya Afrika wanatarajiwa kupitisha azimio linaloitaka mahakama ya kimataifa ya jinai ICC kuruhusu kesi za washukiwa wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya kurejeshwa nchini humo
Azimio hilo linaitaka mahakama ya ICC kukubali kesi dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake Uhuru Kenyatta waliohusishwa na ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya mwaka 2007/08 zisikilizwe na mahama za nyumbani Kenya.
Viongozi hao wataitaka mahakama ya ICC kusitisha kesi hizo wakisema kuwa mahakama za Kenya zina uwezo wa kusikiliza kesi hizo.
Duru zinasema kuwa marais wa nchi za Afrika wataunga mkono azimio hilo, ambalo liliidhinishwa na mawaziri wa nchi za kigeni wa Afrika mjini Addis Ababa siku ya Ijumaa.
Rais Kenyatta na naibu wake William Ruto, walichaguliwa katika uchaguzi wa Machi mwaka huu huku wakikabiliwa na kesi ya junai katika mahakama ya ICC.
Wanahusishwa na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 ambapo watu 1,100, waliuawa na maelfu kuachwa bila makao.
Hata hivyo pendekezo la mataifa ya Afrika haliwezi kuathiri kisheria kesi hiyo ikiwa litapitishwa , lakini bila shaka litampa ushawishi mkubwa Rais Kenyatta barani.
Itakuwa mara ya kwanza kwa azimio kama hilo kupitishwa dhidi ya mahakama ya ICC licha ya Uhuru Kenyatta kuwa rais wa pili kukabiliwa na kesi katika mahakama ya ICC. Wa kwanza ni Rais wa Sudan,Omar al-Bashir anayekabiliwa na kesi ya jinai.
Shirika la kimataifa la Amnesty International, limekosoa hatua hiyo, likisema inatia wasiwasi kwani inanuia kuwakwepesha mkono wa sheria washukiwa hao.

Monday, May 27, 2013

Syria conflict: EU to discuss amending arms embargo

Rebel fighters in the northern Syrian city of Aleppo (21 April 2013)  
The rebels and their supporters say the EU arms embargo must be lifted
European Union foreign ministers are to discuss British and French calls for them to ease sanctions against Syria so weapons can be supplied to the rebels.
At a meeting in Brussels, UK Foreign Secretary William Hague is expected to argue that the current sanctions regime, which is due to expire at the end of this week, is no longer working.
He wants it amended so arms can be sent to "moderate" forces in the opposition.
However, several EU states are totally opposed to ending the arms embargo.
Earlier, Syria's foreign minister confirmed the government would "in principle" attend an international peace conference which the US and Russia hope will take place in Geneva next month.

Sunday, May 26, 2013

Viongozi wa AU waanza mazungumzo

 27 Mei, 2013 
Baada ya sherehe za Jumamosi mjini Addis Ababa kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Afrika, viongozi wa Afrika sasa wanajadili baadhi ya matatizo yanayokabili bara hilo.
Rais Joseph Kabila wa DRC katika mkutano wa viongozi wa AU mjini Addis Ababa
Vita vya muda mrefu katika Jamhuri ya Demokrasi ya Congo vilichukua nafasi kubwa mazungumzo yalipoanza.
Tena majadiliano yakahusu pendekezo la kuyafanya mahakama ya jinai ya kimataifa, ICC, yaache hatua za kumfikisha mahakamani rais mpya wa Kenya na makamo wake kwa mashtaka ya uhalifu dhidi ya binaadamu.
Wanabalozi wanasema viongozi wa Afrika wamegawika kuhusu swala hilo.
Mawaziri wa Mashauri ya Nchi za Nje walikubaliana Alkhamisi, kabla ya viongozi kukutana, kwamba AU iiombe ICC kupeleka jukumu la kesi za Rais Uhuru Kenyatta na makamo wake Wiliam Ruto kwa mahakama ya Kenya.

Angelina Jolie's aunt dies of breast cancer

Angelina Jolie in London (April 2013) 
 Angelina Jolie's uncle praised the actress for electing to have a double mastectomy

Related Stories

Angelina Jolie's aunt has died of breast cancer, nearly two weeks after the Hollywood star said she had had a double mastectomy to avoid such a fate.
Debbie Martin passed away at the Palomar Medical Centre in Escondido on Sunday, aged 61, the hospital said.
Mrs Martin was the sister of Jolie's mother Marcheline Bertrand, who died of breast cancer in 2007 at the age of 56.
Her husband, Ron Martin, said the sisters had both had the same mutated BRCA1 gene, which Jolie inherited.
"Angelina has been in touch throughout the week and her brother Jamie has been with us, giving his support day by day," he told E! News.
"They both loved Debbie very much and although Angie is not able to come right now she has sent her love and support which was very nice."
Mr Martin also praised the actress for electing to have a double mastectomy, telling the Associated Press: "Had we known, we certainly would have done exactly what Angelina did."
On 14 May, the 37 year old wrote in the New York Times that she had had the operation after doctors estimated she had an 87% risk of breast cancer and a 50% risk of ovarian cancer.
"I decided to be proactive and to minimise the risk as much I could," she explained, adding that her chances of developing breast cancer had now dropped to less than 5%.
The BRCA1 gene is present in everyone but only mutates in one in 1,000 people. Anyone with the mutation has a 50-80% chance of developing breast cancer.

facebook
google
like
other