Saturday, May 4, 2013

Ghasia zaendelea mjini Conakry, Guinea

 4 Mei, 2013 - Saa 14:49 GMT

Watu kama watatu wameuwawa nchini Guinea katika mapambano baina ya polisi na waandamanaji waliodai uchaguzi huru na wa haki.
Maandamano ya mwezi March mjini Conakry
Ghasia zimekuwa zikiendelea kwa siku ya pili katika mji mkuu, Conakry.
Afisa mmoja wa upinzani alieleza kuwa waliokufa walikuwa wafuasi wa upinzani.
Upinzani nchini Guinea unasema Rais Alpha Conde hakuwashauri kabla ya kutangaza siku ya uchaguzi wa wabunge kuwa tarehe 30 Juni.
Upinzani unataka wafuasi wake wafanye maandamano hadi rais afute uchaguzi huo.
Rais Conde alishika madaraka mwaka wa 2010 baada ya uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia tangu mwaka 1958.
Lakini uchaguzi wa wabunge uliopangwa kufanywa mwaka wa 2011 umekuwa ukiahirishwa kwa sababu wanasiasa wameshindwa kuwafikiana.

Mpaka wa Afghanistan na Pakistan kumoto

 4 Mei, 2013 

Umoja wa Mataifa umeonya juu ya janga jipya liloanza upande wa Pakistan kwenye mpaka wake na Afghanistan, mpaka wenye mzozo.
Askari wa Afghanistan wako zamu kwenye mpaka na Pakistan
Katika miezi michache iliyopita kumezuka mapigano tena mpakani baina ya wanajeshi wa Afghanistan na Pakistan.
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi, UNHCR, limesema kuwa watu zaidi ya 70,000 wamekimbia majumbwani mwao tangu kati ya mwezi wa March.
Rais Hamid Karzai wa Afghanistan amesema serikali yake katu haitatambua mpaka huo ambao uliwekwa mwaka wa 1893 na wakoloni Waingereza - mpaka uloitenga maeneo ya makabila fulani ambayo kijadi yalikuwa pamoja.

Ghasia zaendelea mjini Conakry, Guinea

 4 Mei, 2013 - Saa 14:49 GMT

Watu kama watatu wameuwawa nchini Guinea katika mapambano baina ya polisi na waandamanaji waliodai uchaguzi huru na wa haki.
Maandamano ya mwezi March mjini Conakry
Ghasia zimekuwa zikiendelea kwa siku ya pili katika mji mkuu, Conakry.
Afisa mmoja wa upinzani alieleza kuwa waliokufa walikuwa wafuasi wa upinzani.
Upinzani nchini Guinea unasema Rais Alpha Conde hakuwashauri kabla ya kutangaza siku ya uchaguzi wa wabunge kuwa tarehe 30 Juni.
Upinzani unataka wafuasi wake wafanye maandamano hadi rais afute uchaguzi huo.
Rais Conde alishika madaraka mwaka wa 2010 baada ya uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia tangu mwaka 1958.
Lakini uchaguzi wa wabunge uliopangwa kufanywa mwaka wa 2011 umekuwa ukiahirishwa kwa sababu wanasiasa wameshindwa kuwafikiana.

Kazi za uokozi zasimamishwa Darfur

 4 Mei, 2013 - Saa 13:53 GMT


Kazi za uokozi zilizokuwa zikifanywa Darfur, Sudan, kutafuta wafanyakazi 100 walionasa kwenye mgodi wa dhahabu ulioporomoka Jumatatu zimesimamishwa.
Darfur
Walioshuhudia tukio hilo wanasema msako katika mgodi wa Jebel Amir umesimamishwa kwa sababu ni hatari kuendelea na kazi za uokozi.
Hapo jana waokozi tisa piya walinasa kwenye mgodi huo.
Hakuna aliyenusurika.
Inaarifiwa kuwa migodi midogo-midogo ya Sudan ilitoa dhahabu ya thamani ya zaidi ya dola bilioni-mbili mwaka jana.
Madini hayo yanaipatia Sudan sarafu za kigeni ambazo zilipungua sana baada ya Sudan Kusini kujitenga mwaka wa 2011 na kubaki na visima vingi vya mafuta.

Israel yashambulia ghala ya silaha Syria

 4 Mei, 2013 


Serikali ya Syria bado haikusema kitu kuhusu taarifa kutoka wakuu wa Marekani kwamba ndege za Israel zimefanya mashambulio katika ardhi ya Syria, ambako inaarifiwa ghala ya silaha imeshambuliwa.
Ndege ya Israel

Wakuu wanasema makombora yalifyatuliwa kutoka ndege za Israel ambazo ziliruka kwenye anga ya Libnan, nchi ya jirani.
Huku nyuma kuna taarifa za mauaji zaidi katika miji ya pwani ya Syria kukiwa na tuhuma kuwa raia wengi wamechinjwa na wanajeshi wa serikali na wanamgambo.
Wanaharakati wanaripoti kuwa mauaji ya pili yamefuatia yale ya kwanza katika eneo hilo-hilo la mwambao kaskazini-magharibi mwa Syria.
Wanasema mauaji ya kwanza yalifanywa kwenye kijiji cha al-Beida cha Wasunni, ambacho kilivamiwa na wanajeshi wa serikali siku ya Alkhamisi.
Wanaharakati wamewataja watu 50 ambao wanasema walichinjwa kati yao wakiwemo wanawake na watoto.
Sasa wanaeleza kisa kama hicho kutokea katika mtaa wa Ras an-Naba wa mji wa pwani wa Banias ulio jirani na al-Beida.
Wameonesha picha kwenye internet kama ushahidi, lakini hakuna njia ya kuthibitisha ukweli wa picha hizo.
Picha zinaonesha maiti za wanawake na watoto zimelala ndani ya nyumbao zao, miili mengine imekeketwa na mengine imechomwa.
Mamia ya familia zimekimbia Banias kuelekea kusini kwenye mji wa Tartous, lakini wanaharakati wanasema wakimbizi hao wamezuwiliwa kupata hifadhi katika mji huo.

Friday, May 3, 2013

Serikali kukaza uzi timuatimua wanafunzi wakorofi vyuo vikuu


Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imesisitiza kuwa itaendeleza utaratibu wa kuwafukuza wanafunzi wa vyuo vikuu ambao watakuwa na tabia za utovu wa nidhamu na migomo isiyokuwa na lazima.
SHARE THIS STORY
Dodoma. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imesisitiza kuwa itaendeleza utaratibu wa kuwafukuza wanafunzi wa vyuo vikuu ambao watakuwa na tabia za utovu wa nidhamu na migomo isiyokuwa na lazima.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo.
Alisema Serikali haina kigugumizi cha kuona ni kwa nini isiwafukuze wanafunzi wa aina hiyo ambao wanakuwa ni kichocheo cha migogoro.
Alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), ambaye alitaka kujua mkakati wa Serikali kuwarudisha wanafunzi wa vyuo vikuu ambao walifukuzwa masomo yao kutokana na migogoro iliyoibuliwa vyuoni mwao.
Katika swali la msingi Mnyika alitaka kujua hatua za Serikali katika kuwarudisha wanafunzi hao kutoka vyuo vya Dodoma (Udom), Dar es Salaam na Chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi (MUHAS).
Mbali na hilo, aliomba ripoti ya Tume ya Rais iliyoundwa mwaka 2011 kwa ajili ya kuangalia migogoro hiyo kwa wanafunzi ambayo imedumu kwa muda mrefu ili ipelekwe bungeni na kujadiliwa kabla ya kumshauri Rais jambo la kufanya.
Naibu Waziri alisema katika migogoro hiyo, kuna maeneo ambayo wanafunzi walisimamishwa masomo na baadhi walirudishwa masomoni, lakini wengine bado hawajarudishwa.
“Mfano, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wanafunzi waliosimamishwa ni 99, lakini 78 walirudishwa na 21 hawajarudishwa, kwa Udom walisimamishwa 570 lakini 563 walirudishwa masomoni na 7 wamefukuzwa kabisa, kingine ni MUHAS ambapo walisimamishwa wanafunzi 115 wengine wamerudi na wengine watarudi Desemba mwaka huu wakati wanafunzi wawili wamefukuzwa kabisa,” alisema Mulugo.
Kuhusu ripoti ya Rais, Mulugo alisema ilikuwa ni tume maalumu kwa ajili ya kumsaidia Rais, hivyo siyo lazima ripoti yake kupelekwa bungeni kama ambavyo wabunge wanataka.

MFANYABIASHARA KARIAKOO AJIRUSHA TOKA GHOROFA YA TISA NA KUANGUKIA GARI MCHANA HUU

Muda mfupi uliopita,Mtu mmoja alietambulika kwa jina la Shirima ambaye ni Mfanyabiashara katika moja ya Maduka ya Kariakoo jijini Dar es Salaam,amejirusha toka ghorofa ya 9 ya Hoteli ya Concord iliopo Maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam na amekimbizwa hospitali kwa uangalizi zaidi maana haijafahamika kama kapoteza Maisha au bado yu hai.

Mfanyabiashara huyo alijirusha toka ghorofani na kuangukia Gari aina ya Toyota Corolla ambayo ni taxi iliyokuwa imepaki nje ya hoteli hiyo....chanzo cha kujirusha kwa mfanyabiashara huyo bado hakijafahamika mpaka sasa.

Mashuhuda wa tukio hilo lililotokea muda mfupi uliopita,wanaeleza kuwa walipatwa na mshuko baada ya kusikika kishindo cha kitu kilichokuwa kimeangukia gari hilo na waliposogea kushuhudia ndipo walipobaini kuwa alikuwa ni mtu huyo alietambulika kwa jina moja la Shirima.