Monday, June 24, 2013

Hali ya wasiwasi kuhusu afya ya Mandela

Mzee Nelson Mandela
Wananchi wa Afrika Kusini wanaelekea kazini asubuhi ya leo wakiwa na simanzi huku wakisubiri habari kuhusu afya ya rais mstaafu Nelson Mandela ambaye madaktari wanasema yuko mahututi.
Taarifa kutoka ikulu ya rais zilisema Jumapili jioni kuwa Mandela alikuwa amezidiwa ingawa madaktari wanafanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa anapata afueni.
Afisaa mmoja mkuu alisema kuwa raia wa Afrika Kusini wasiwe na maytumaini kupita kiasi.
Mandela ambye alikuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, akiwa na umri wa miaka 94,alipelekwa hospitalini mapema mwezi huu, ikiwa ni mara ya tatu kwake kulazwa hospitalini akiugua ugonjwa wa mapafu mwaka huu.
Rais Jacob Zuma alisema Jumapili kuwa alimzuru Mandela Hospitalini na kuzungumza na mkewe kuhusu hali ya rais mstaafu.
Madaktari wanaomtibu Mzee Nelson Mandela wamesema hali yake imekuwa sio nzuri kwa saa ishirini na nne zilizopita na sasa ni mahututi.
Habari hizo zimekuja kupitia taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais ya Afrika Kusini.
Taarifa hiyo imesema bado Mzee Mandela ameendelea kusalia hospitalini mjini Pretoria kwa siku ya kumi na sita akitibiwa mapafu yaliyosababisha tatizo kwenye mfumo wake wa upumuaji.
Rais Jacob Zuma amemtembelea Mzee Mandela na pia kuzungumza na jopo la matabibu wanaomtibu.
Baadaye bwana Zuma alirejea kauli yake ya kulitaka taifa na dunia kumuombea Mzee Mandela apate nafuu.

Friday, June 14, 2013

Uchaguzi kufanyika Julai 31 Zimbabwe

Mzozo wa kisiasa umeibuka nchini Zimbabwe baada ya rais Robert Mugabe kutoa agizo kuwa uchaguzi mkuu nchini humo utafanyika tarehe Thelathini na Moja Julai mwaka huu.
Waziri mkuu wa Zimbabwe, Morgan Tsvangirai, ametoa taarifa muda mfupi tu baada ya agizo hilo la rais, akisema kuwa rais Mugabe amekiuka sheria kwa kutoshirikisha bunge na ameapa kupinga uamuzi huo.

Morganb Tsvangirai
Katika kikao na waandishi wa habari, Tsvangirai, amemshutumu Bwana Mugabe kwa kukiuka mkataba wa ugavi wa mamlaka uliosainiwa miaka mitano iliyopita, baada ya mzozo kuhusu matokeo ya kura kusababisha ghasia nchini humo.
Tsvangirai ametaka uchaguzi huo kuhairishwa hadi mageuzi ya kikatiba yafanyike ili kuhakikisha zoezi hilo la uchaguzi linafanyika kwa njia huru na haki.
Bunge la nchi hiyo bado linajadili mswada wa sheria ambao utaruhusu vyama vyote vya kisiasa kupewa nafasi sawa katika shirika la habari la serikali wakati wa kampeini.
Lakini wiki mbili zilizopita mahakama ya kikatiba nchini humo iliagiza kuwa uchaguzi huo ni sharti ufanyike kabla ya mwisho wa Julai.

BREAKING NEWS: MSANII LANGA AFARIKI DUNIA

Langa Kileo (msanii wa Hip Hop Tanzania, pichani)

Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba msanii Langa amefariki dunia..
Habari zinadai  kuwa , Msanii huyu alikumbwa na Malaria kali sana hali iliyopelekea kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili jana.

Monday, June 10, 2013

Mbunge mahakamani kwa uchochezi TZ

 
Wananchi wa mtwara hawataki gesi asilia kusafirishwa popote
Mbunge wa jimbo la Mtwara, eneo ambalo limekumbwa na vurugu hivi karibuni kusini mwa Tanzania amefikishwa mahakamani leo akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi wa vurugu zilizo sababisha vifo vya watu watatu mwezi uliopita.
Hasnain Murji pamoja na watuhumiwa wengine 91 wamefikishwa kwenye mahakama ya wilaya ya Mtwara.
Kwa muda huu baadhi ya watuhumiwa wamepata dhamana huku wengine wakiendelea na taratibu za kukamilisha udhamini, wakati Mbunge huyo akisubiri kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayo mkabili.
Wananchi waliofika mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi zinazowakabili ndugu na jamaa zao wamelalamikia utaratibu wa kuwazuwia kuingia mahakamani hapo.
Mbunge huyo wa Chama kinacho tawala nchini humo CCM, alikamatwa na kushikiliwa na jeshi la Polisi mkoani humo siku ya Jumamosi.
Idadi kubwa ya wananchi wa Mtwara wamekuwa katika mvutano mkali na Serikali ya Tanzania ambayo imekusudia kujenga bomba la kusafirisha gesi asilia inayopatikana mkoani humo hadi Dar es Salaam , Hatua inayopingwa na wananchi hao ambao wanadai gesi hiyo isisafirishwe na kupelekwa popote.

Mbunge mahakamani kwa uchochezi TZ


Wananchi wa mtwara hawataki gesi asilia kusafirishwa popote
Mbunge wa jimbo la Mtwara, eneo ambalo limekumbwa na vurugu hivi karibuni kusini mwa Tanzania amefikishwa mahakamani leo akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi wa vurugu zilizo sababisha vifo vya watu watatu mwezi uliopita.
Hasnain Murji pamoja na watuhumiwa wengine 91 wamefikishwa kwenye mahakama ya wilaya ya Mtwara.
Kwa muda huu baadhi ya watuhumiwa wamepata dhamana huku wengine wakiendelea na taratibu za kukamilisha udhamini, wakati Mbunge huyo akisubiri kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayo mkabili.
Wananchi waliofika mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi zinazowakabili ndugu na jamaa zao wamelalamikia utaratibu wa kuwazuwia kuingia mahakamani hapo.
Mbunge huyo wa Chama kinacho tawala nchini humo CCM, alikamatwa na kushikiliwa na jeshi la Polisi mkoani humo siku ya Jumamosi.
Idadi kubwa ya wananchi wa Mtwara wamekuwa katika mvutano mkali na Serikali ya Tanzania ambayo imekusudia kujenga bomba la kusafirisha gesi asilia inayopatikana mkoani humo hadi Dar es Salaam , Hatua inayopingwa na wananchi hao ambao wanadai gesi hiyo isisafirishwe na kupelekwa popote.

Hali ya Mandela inasemekana kuwa tete


Mandela ndiye aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi
Rais mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela, angali katika hali mbaya ingawa imeweza kudhibitiwa. Mandela amelazwa katika hospitali moja mjini Pretoria.
"mzee Mandela yuko hospitalini na hali yake bado haijabadilika.''
Maombi yakekuwa yakifanywa makanisani kote nchini Afrika Kusini kumuombea Mandela ambaye anatibiwa kwa ugonjwa wa mapafu.
Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alipelekwa hospitalini mapema Jumamosi , ikiwa ni mara ya tatu kulazwa hospitalini mwaka huu.
Kwa mujibu wa duru za urais, Mandela amekuwa akiugua kwa muda mjini Johannesburg baada ya kukumbwa tena na ugonjwa wa mapafu.
Alilazwa hospitalini baada ya hali yake kuwa mbaya zaidi mnamo Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa za urais, Rais President Jacob Zuma, amerejelea wito wake kwa watu nchini Afrika Kusini kumuombea Madiba wakati huu anapougua.
Lakini mwandishi wa BBC mjini Pretoria, Karen Allen, anasema kuwa kuna matumaini amdogo kuwa Mandela aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, huenda kupona.
Anasema kuwa wengi walipata matumani baada ya bintiye Mandela Zindzi, kusema kuwa babake yuko salama na kuwa anaendelea kupata nafuu.
Mkewe Mandela Graca Machel, alifutilia mbali, ziara yake mjini London Jumamosi ili kuwa kando ya mumewe.
Mandela alikuwa Rais wa Afrika Kusini kati ya mwaka 1994 hadi 1999.
Alifungwa jela miaka 27 na anaaminika kuwahi kuugua ugonjwa wa mapafu alipokuwa akifanyishwa kazi ngumu katika machimbo ya mawe akiwa jela.
Sorry, there has been a problem displaying comments, we are working to fix this.

Winnie , amzuru Mandela hospitalini

 

Mandela na Winnie , katika siku za furaha
Mke wa zamani wa Nelson Mandela, Winnie amewasili katika hospitali nchini Afrika Kusini, ambako inaaminiwa rais huyo mstaafu anaendelea kupokea matibabu kwa ugonjwa wa homa ya mapafu.
Mtoto wao wa kike Zenani (mandela - Dlamini) pia amerejea nchini Afrika Kusini kutoka Argentina ambako anahudumu kama balozi wa Afrika Kusini, ili awe na babake.
Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alipelekwa hospitalini mapema Jumamosi , ikiwa ni mara ya tatu kulazwa hospitalini mwaka huu.
Kwa mujibu wa duru za urais, Mandela amekuwa akiugua kwa muda mjini Johannesburg baada ya kukumbwa tena na ugonjwa wa mapafu. Msemaji wa serikali Mac Maharaj amesema kuwa maafisa katika hospitali wanataka kudhibiti idadi ya watu wanaozuru hospitali hiyo ili wampunguzie bwana Mandela usumbufu.
risala za heri njema na afueni kwa rais mstaafu Nelson Mandela
Alilazwa hospitalini baada ya hali yake kuwa mbaya zaidi mnamo Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa za urais, Rais President Jacob Zuma, amerejelea wito wake kwa watu nchini Afrika Kusini kumuombea Madiba wakati huu anapougua.
Lakini mwandishi wa BBC mjini Pretoria, Karen Allen, anasema kuwa kuna matumaini madogo kuwa Mandela aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, huenda akapona.
Anasema kuwa wengi walipata matumani baada ya bintiye Mandela Zindzi, kusema kuwa babake yuko salama na kuwa anaendelea kupata nafuu.
Mkewe Mandela Graca Machel, alifutilia mbali, ziara yake mjini London Jumamosi ili kuwa kando ya mumewe.
Mandela alikuwa Rais wa Afrika Kusini kati ya mwaka 1994 hadi 1999.
Alifungwa jela miaka 27 na anaaminika kuwahi kuugua ugonjwa wa mapafu alipokuwa akifanyishwa kazi ngumu katika machimbo ya mawe akiwa jela.