Thursday, April 18, 2013

Watoto waathirika zaidi na vita (CAR)

 18 Aprili, 2013 - Saa 11:37 GMT

Maeneo wanayopigania waasi wa Seleka
Shirika la kuwahudumia watoto la umoja wa mataifa UNICEF, limeelezea hofu ya kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaouawa katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati.
UNICEF linasema kuwa watoto hao wanajipata katika maeneo ya vita wakati makundi yaliyojihami yanapopambana viwanjani na hata makanisani.
Aidha shirika hilo limesema kuwa takriban watoto watatu waliuawa na wengine zaidi ya ishirini kujeruhiwa vibaya siku ya ijumaa.
Linadai kuwa watoto hao wamesajiliwa kama wapiganaji katika makundi ya waasi.
Kumekuwa na mapigano pamoja na uporaji katika mji mkuu Bangui baada ya waasi kuuteka mji mkuu mwezi jana.
Wiki tatu baada ya waasi wa Seleka kutwaa mamlaka katika mapinduzi ya kijeshi,uporaji na ghasia zimekithiri nchini humo watoto wakiwa katika hatari kubwa zaidi.
Tangu makabiliano kuanza upya mwishoni mwa mwezi wa Machi, watoto wengine wengi zaidi wamekuwa waathiriwa wa risasi wakati wengine wakisajiliwa kama wapiganaji. Pia kumekuwa na taarifa za kuongezeka kwa visa vya ubakaji
“Tunaiona nchi hii ikikumbwa na ghasia huku watoto wakiwa waathiriwa wakubwa,'' alisema Souleymane Diabate afisaa mkuu wa shirika hilo katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati. ''Ghasia dhidi ya watoto lazima zisitishwe. Watu wasio na hatia wanauawa au kujeruhiwa na lazima zichunguzwe na maafisa wakuu,'' alisema Biabate
Wiki jana UNICEF ilitoa vifaa muhimu vya matibabu na hata kuweka kliniki ya muda kwa akina mama wajawazito ndani na nje ya mji wa Bangui. Watoto waliojeruhiwa pia wamepokea matibabu

Rais aunga mkono msamaha kwa Boko Haram

 18 Aprili, 2013 - Saa 09:20 GMT

Rais Jonathan alikuwa amepinga jambo la kuwapa msamaha wapiganaji hao
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amezindua kamati mpya itakayochunguza uwezo na utekelezwaji wa msahama kwa kundi la wapiganaji wa kiisilamu Boko Haram.
Kamati hiyo itakuwa na siku sitini kufikia uamuzi wake wa mazungumzo na kuwapokonya silaha wapiganaji hao , kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa ofisi ya rais.
Pia itaangazia nyenzo za kuwasaidia waathiriwa wa ghasia ambazo chanzo chake ni wapiganaji hao.
Boko Haram limewaacha maelfu wakiwa wamefariki kutokana na ghasia ambazo wamekuwa wakisababisha mara kwa mara tangu mwaka 2009.
Kamati hiyo ambayo wanachama wake 25 wanajumuisha maafisa wa kijeshi, wasomi na wanasiasa watajaribu kuangazia sababu zinazopelelea makundi kama Boko Haram kuafanya uasi na njia za kuwazuia.
Zaidi ya hayo, rais Jonathan ameidhinisha kuundwa kwa kamati nyingine ya serikali kuhusu kuwapokonya wapiganaji hao silaha katika jitihada zake za kuimarisha usalama na uthabiti wa nchi.

Hatua mwafaka

Viongozi wa kisiasa na kidini, kutoka Kaskazini mwa Nigeria, ambalo ndio kitovu cha uasi huo, hivi karibuni walipendekeza serikali kutoa msamaha kwa wapiganaji hao.
Rais Goodluck Jonathan alijibu kauli hiyo na mwanzoni mwa mwezi Aprili alikipa kikundi cha washauri wa usalama jukumu la kuangalia ambavyo msamaha unaweza kutolewa kwa wapiganaji hao.
Duru zinasema kuwa hoja hii ya msamaha ni muhimu kwani rais alikuwa ameipuuza mwanzoni.
Ni wazi kuwa rais ameitikia kuwa juhudi za kijeshi dhidi ya wapiganaji hao hazijazaa matunda.
Hata hivyo haijulikani ambavyo wapiganaji hao watatizama wazo la rais ikizingatiwa kuwa ni makundi mengi ya mirengo tofauti ya wapiganaji.
Wiki jana Boko Haram, ambao wanataka utawala wa kiisilamu Kaskazini mwa nchi limekataa pendekezo la msamaha kwao.


Tuesday, April 16, 2013

Karim Wade atiwa nguvuni kwa ulaghai

 16 Aprili, 2013 - Saa 08:07 GMT

Karim Wade
Mwanawe rais wa zamani wa Senegal Abdoulaye Wade, ametiwa nguvuni kwa kujipatia dola bilioni 1.4 wakati wa utawala wa baba yake .
Karim Wade ambaye alihudumu katika serikali ya baba yake alikuwa na nyadhifa mbali mbali wakati huo .
Wade aliwasilisha waraka wa orodha ya mali zake katika mahakama maalum ya senegali iliyopewa jukumu la kuchunguza kesi za ufisadi jana asubuhi.
Alipewa muda wa mwezi mmoja kuthibitisha kuwa alichukua zaidi ya dola dola bilioni kihalali wakati baba yake alipokuwa madarakani.
Karim Wade alipewa jina la bandia waziri wa anga na dunia , alipokuwa waziri wa miundo mbinu , mipango ya miji , usafiri wa anga na ushirikiano wa kimataifa kwa wakati mmoja.
Wakati huo pia alikuwa mkuu wa theluthi moja ya matumizi ya taifa . Mahakama ya Senegali bado haijaeleza sababu ya kumtia rumande na mawakili wa Karim Wade wamesema alichukuliwa kwa nguvu .

Karim Wade atiwa nguvuni kwa ulaghai

 
 Mwanawe rais wa zamani wa Senegal Abdoulaye Wade, ametiwa nguvuni kwa kujipatia dola bilioni 1.4 wakati wa utawala wa baba yake .

Karim Wade ambaye alihudumu katika serikali ya baba yake alikuwa na nyadhifa mbali mbali wakati huo .
Wade aliwasilisha waraka wa orodha ya mali zake katika mahakama maalum ya senegali iliyopewa jukumu la kuchunguza kesi za ufisadi jana asubuhi.
Alipewa muda wa mwezi mmoja kuthibitisha kuwa alichukua zaidi ya dola dola bilioni kihalali wakati baba yake alipokuwa madarakani.
Karim Wade alipewa jina la bandia waziri wa anga na dunia , alipokuwa waziri wa miundo mbinu , mipango ya miji , usafiri wa anga na ushirikiano wa kimataifa kwa wakati mmoja.
Wakati huo pia alikuwa mkuu wa theluthi moja ya matumizi ya taifa . Mahakama ya Senegali bado haijaeleza sababu ya kumtia rumande na mawakili wa Karim Wade wamesema alichukuliwa kwa nguvu .

Students in N Korea

Students march at a camping site in Pyongyang as the first term of camping commences nationwide, to commemorate the 101st anniversary of the birth of North Korea's founder Kim Il-sung, in this photo distributed by North Korea's official Korean Central News Agency (KCNA) on April 15, 2013. North Korea celebrated the anniversary of its founder's birth on Monday and abandoned its shrill threats of war against the United States and the South, easing tensions in a region that had seemed on the verge of conflict. REUTERS/KCNA (NORTH KOREA - Tags: ANNIVERSARY MILITARY POLITICS EDUCATION) ATTENTION EDITORS - THIS PICTURE WAS PROVIDED BY A THIRD PARTY. REUTERS IS UNABLE TO INDEPENDENTLY VERIFY THE AUTHENTICITY, CONTENT, LOCATION OR DATE OF THIS IMAGE. THIS PICTURE IS DISTRIBUTED EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS. NO THIRD PARTY SALES. NOT FOR USE BY REUTERS THIRD PARTY DISTRIBUTORS




Watu 17 wauawa Jamuhuri ya Afrika ya Kati

 15 Aprili, 2013 - Saa 13:58 GMT
Waasi wa Seleka
Takriban watu kumi na saba waliuawa katika makabiliano yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati.
Hii ni kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu, Red Cross.
Mapigano yalizuka baada ya waasi wa zamani waliokuwa wanashika doria katika Ikulu ya rais aliyeondolewa mamlakani
Francois Bozize kushambuliwa.
Msemaji wa serikali mpya alisema kuwa kiongozi wa waasi, Michel Djotodia alitangazwa kuwa rais wa mpito mnamo Jumamosi.
Kundi lake la waasi lilichukua mamlaka wiki tatu zilizopita.
Mapambano yaliyotokea Jumamosi na Jumapili yalikuwa mabaya zaidi kuwahi kushuhudiwa mjini
Bangui tangu kung'olewa mamlakani kwa bwana Bozize.
Kombora liliangukia kanisa la Baptist siku ya Jumapili na kuwaua watu watatu.
Kasisi wa kanisa hilo alikatwa mkono wake baada ya kujeruhiwa vibaya kwenye shambulio hilo.
Kundi la waasi la Seleka lililoipindua serikali ya Rais Fracois Bozize

Kaimu msemaji wa serikali ,generali Moussa Dhaffane, alisema kuwa makabiliano yalizuka wakati vijana waliwashambulia wanajeshi waasi, katika eneo Boy-Rabe, eneo linalosemekana kuwa ngome ya bwana Bozize.
Maafisa wa shirika la Red Cross walisema kuwa watu 17 waliuawa katika sehemu mbali mbali za mji mkuu.
Wenyeji walisema kuwa vijana wengi wanataabika kufuatia hali mbaya ya usalama mjini Bangui.
Baadhi wakiwatuhumu waasi hao kwa uporaji.
Baraza la kitaifa la mpito, lililoundwa baada ya kupinduliwa kwa rais Bozize lilimteua bwana Djotodia kama rais wa muda siku ya Jumapili.
Taarifa iliyotiwa saini na Francois Bozize kutoka kwa idara ya mawasiliano ililaani vikali mapinduzi hayo.
Aidha bwana Bozize alikimbilia Cameroon wakati waasi walipowasili Bangui.
Bwana Djotodia alisema kuwa ataandaa uchaguzi katika kipindi cha miezi 18
Kundi la waasi la Seleka, lilitwaa mamlaka, baada ya mkataba wa amani waliotia saini na rais Bozize kusambaratika.


Lashukiwa kuwa shambulio la kigaidi

 16 Aprili, 2013 - Saa 06:41 GMT

Milipuko miwili mikubwa iliyotokea kwenye mstari wa mwisho wa kumalizia mbio za Boston Marathon nchini Marekani imewauwa watu watatu na kuwajeruhi wengine zaidi ya mia moja.
Mlipuko wa pili ulitokea sekunde chache tu baada ya ule wa kwanza kutokea wakati mamia ya wanariadha wakikamilisha mbio zao huku wakishangiliwa na umati. Waliojeruhiwa walikimbizwa hospitalini huku wengi wao wakitokwa na damu.
Duru zinasema kuwa majasusi wa FBI wameanzisha uchunguzi katika kile wanachosema huenda yalikuwa mashambulizi ya kigaidi.
Rais Barack Obama amesisitiza kuwa serikali serikali itakahikisha kuwa washukiwa wa mashambulizi hayo lazima atakamatwa.
Picha na video kutoka Boston zilionyesha watu wakiwa wamechanganyikiwa wasijue pa kwenda, huku magari ya huduma za dharura yakielekea katika eneo la tukio na watu waliojeruhiwa vibaya wakipelekwa kwenye hema la matibabu ya haraka.
"Kuna watu wengi wamelala chini," alisema mwanariadha mmoja akinukuliwa na chombo cha habari cha AP.
Tukio hilo linaripotiwa kutokea saa tatu baada ya washindi kuvuka mstari wa ushindi.
"Kulikuwa na mlipuko, polisi, moto na EMS kwenye eneo la tukio. Hatuna namna ya kufahamu namna watu walivyojeruhiwa," msemaji wa Polisi Boston alisema.
Shirika la habari la AP linasema kulikuwa na sauti kubwa ya mlipuko upande wa kaskazini mwa mtaa wa Boylston Street, karibu tu daraja linaashiria mstari wa kumalizia mashindano. Mlipuko mwingine ukasikika dakika chache baadaye.
Mike Mitchell wa Vancouver kutoka Canada, mwanariadha aliyemaliza kukimbia alisema alikuwa akiangalia nyuma ya mstari wa kumalizia mashindano ndipo aliposikia ‘mlipuko mkubwa’
Inataarifiwa kuwa moshi ulipanda juu hewani kiasi cha futi 50 (mita 15),' aliliambia shirika la habari la Reuters , na watu wakaanza kukimbia wakipiga mayowe baada ya kusikia
Wanariadha waliomaliza mbio za Boston Marathon
"Kila mtu alichanganyikiwa,’ alisema.
Waliokuwa wakimalizia mbio hizo waliongozwa kuepuka eneo lenye moshi kwenye mlipuko wakati huo huo eneo hilo likifungwa.
Tawi la Msalaba Mwekundu la Mashariki mwa Massachusetts limetenga kituo cha kusaidia majeruhi.